Tumshauri Naibu Waziri wa Kilimo Hussein Bashe

Mungo Park

JF-Expert Member
Sep 14, 2010
2,112
1,831
Nimefungua huu uzi ili kuweza kumshauri Naibu Waziri Hussein Bashe katika Wizara yake ya Kilimo. Kama alivyosema Kilimo ni Biashara lakini Kilimo kina changamoto za kutosha ambazo Watendaji na Mawaziri ama hawazielewi au hawazitilii maanani.
Huu ni ushauri tu kwa Naibu Waziri Bashe. Akiuzingatia tutakwenda mbele, akipuuza atakuwa kama Mawaziri wengine waliopita.
Katika Tanzania Kilimo kinachangia asilimia karibu 29% katika GDP na Watanzania karibu asilimia 65.5% - 70% ni Wakulima ama wanajishughulisha na bidhaa za Kilimo. Nitatumia neno Asababishe kwani najua Waziri ndiyo yupo juu yake.
Ushauri wenyewe ni huu..
  1. Asababishe kufanyika kwa sensa ya maeneo ya Kilimo Tanzania(kwa kiwango cha kata) na mahitaji yao.
  2. Asababishe yale maeneo maarufu kwa Kilimo yana angalau matrekta 2 kwa kila kata yakiwa na vifaa vyake kama majembe,'planters','harrows',harvesters',n.k. ili wakulima waweze kulima kwa bei nafuu na kwa haraka Zaidi.
  3. Asababishe Mbolea inafika maeneo ya mashambani kwa wakati kabla ya msimu wa kupanda.
  4. Asababishe mawasiliano na Wizara ya Nishati ili kujua ni kwa nini Mbolea ya Minjingu haipendwi na Wakulima na madhara yake.
  5. Asababishe utoaji wa haraka wa Pembejeo za Kilimo Bandarini ili kuwahi misimu ya Kilimo.
  6. Asababishe kuanzishwa kwa ofisi ndogo za Wizara ya Kilimo Mipakani ili kurahisisha utoaji wa Vibali vya mauzo ya mazao nje.
  7. Asababishe kurahisisha biashara ya Mazao nje hasa nchi jirani.
  8. Asababishe kuangaliwa kwa utaratibu mzuri wa kurudisha hela za Sukari('15% Import Duty Refunds') kwa viwanda vikubwa kwa kuwa Viwanda vinataabika sana na vingine viko mbioni kusimama. Hili ni kubwa kwani linaathiri utendaji wa baadhi ya Viwanda.
  9. Asababishe kuundwa kwa Kamati ya Uratibu ya Wizara ya Kilimo, Viwanda(SIDO) na Fedha ili kutatua changamoto zinazojitokeza katika shughuli za Ujasiriamali na Viwanda vidogovidogo.
  10. Asababishe kuanzishwa kwa Idara ya Masoko ambayo itafanyanya kazi na Bodi za Tumbaku, Sukari, Chai, Korosho, Pamba, Kahawa, Katani, Pareto, Nafaka na Mazao Mchanganyiko ili kupata masoko katika Nchi Jirani na penginepo na taarifa kupatikana mtandaoni - E-Masoko.
  11. Asababishe upitiaji upya wa ufanisi na uongozi wa Bodi hizi.
  12. Asababishe upatikanaji wa mapema na kwa haraka kwa Takwimu za Mazao ya Kilimo kwa mtandao - E-Takwimu.
  13. Asababishe Uondoshaji/Upunguzaji wa vizuizi vya barabarani kwa mazao ya Kilimo.
  14. Asababishe elimu zaidi, matumizi na matangazo kuihusu 'Tanzania Mercantile Exchange Plc'.
  15. Asababishe Serikali kununua ziada ya mazao toka kwa Wakulima.
  16. Asababishe uangaliwaji kwa jicho la upendeleo Sekta ya 'Horticulture' kwani inataabika sana hasa biashara ya maua n.k.
  17. Asababishe uanzishwaji wa utaratibu wa mara kwa mara wa kukutana na Wakulima ('Round Table') ili kufanya utatuzi wa haraka wa matatizo yao.
Kwa sasa haya yanatosha,nafikiri wengine wataongezea...
 
Unampaje uwazili bashe, ili asiwachalenji, uwaziri wape kina simmnbchaene au kubajaji akili ndogo ili sisi wenye kufikiri sawasawa tuwape challenge nchi isonge. Unadhani kwa mfumo uliopo bashe atatoboa? Njaa tu inamuuma nayeye somalilqnd. Chuma kile cha tigo kiligomea ukurugenzi wa jiwe, hawa ndio miamba very rare. Hatuzaliwi mala mbili, njaa mbaya.

Pangu Pakavu
 
Cheo cha Naibu Waziri ni ceremonial post

Hana Majukumu ya kimsingi

Naibu Waziri hata kwny Vikao vya Baraza la Mawaziri haingii hata kama Waziri hayupo

Yaani Naibu Katibu Mkuu wa Wizara anaweza kuwa na Majukumu muhimu kuliko Naibu hivyo Msimbebeshe matumaini ambayo hayapo
 
Cheo cha Naibu Waziri ni ceremonial post

Hana Majukumu ya kimsingi

Naibu Waziri hata kwny Vikao vya Baraza la Mawaziri haingii hata kama Waziri hayupo

Yaani Naibu Katibu Mkuu wa Wizara anaweza kuwa na Majukumu muhimu kuliko Naibu hivyo Msimbebeshe matumaini ambayo hayapo
Ijapokuwa Cheo cha Naibu Waziri kinaweza kuwa 'Ceremonial' lakini Waziri anaweza kuwa 'clueless' na akategemea 'inputs' kutoka kwa Naibu Waziri..
 
Nimefungua huu uzi ili kuweza kumshauri Naibu Waziri Bashe katika Wizara yake ya Kilimo. Kama alivyosema Kilimo ni Biashara lakini Kilimo kina changamoto za kutosha ambazo Watendaji na Mawaziri ama hawazielewi au hawazitilii maanani.
Huu ni ushauri tu kwa Naibu Waziri Bashe. Akiuzingatia tutakwenda mbele, akipuuza atakuwa kama Mawaziri wengine waliopita.
Katika Tanzania Kilimo kinachangia asilimia karibu 29% katika GDP na Watanzania karibu asilimia 65.5% - 70% ni Wakulima ama wanajishughulisha na bidhaa za Kilimo. Nitatumia neno Asababishe kwani najua Waziri ndiyo yupo juu yake.
Ushauri wenyewe ni huu..
  1. Asababishe kufanyika kwa sensa ya maeneo ya Kilimo Tanzania(kwa kiwango cha kata) na mahitaji yao.
  2. Asababishe yale maeneo maarufu kwa Kilimo yana angalau matrekta 2 kwa kila kata yakiwa na vifaa vyake kama majembe,'planters','harrows',harvesters',n.k. ili wakulima waweze kulima kwa bei nafuu na kwa haraka Zaidi.
  3. Asababishe Mbolea inafika maeneo ya mashambani kwa wakati kabla ya msimu wa kupanda.
  4. Asababishe mawasiliano na Wizara ya Nishati ili kujua ni kwa nini Mbolea ya Minjingu haipendwi na Wakulima na madhara yake.
  5. Asababishe utoaji wa haraka wa Pembejeo za Kilimo Bandarini ili kuwahi misimu ya Kilimo.
  6. Asababishe kuanzishwa kwa ofisi ndogo za Wizara ya Kilimo Mipakani ili kurahisisha utoaji wa Vibali vya mauzo ya mazao nje.
  7. Asababishe kurahisisha biashara ya Mazao nje hasa nchi jirani.
  8. Asababishe kuangaliwa kwa utaratibu mzuri wa kurudisha hela za Sukari('15% Import Duty Refunds') kwa viwanda vikubwa kwa kuwa Viwanda vinataabika sana na vingine viko mbioni kusimama. Hili ni kubwa kwani linaathiri utendaji wa baadhi ya Viwanda.
  9. Asababishe kuundwa kwa Kamati ya Uratibu ya Wizara ya Kilimo, Viwanda(SIDO) na Fedha ili kutatua changamoto zinazojitokeza katika shughuli za Ujasiriamali na Viwanda vidogovidogo.
  10. Asababishe kuanzishwa kwa Idara ya Masoko ambayo itafanyanya kazi na Bodi za Tumbaku, Sukari, Chai, Korosho, Pamba, Kahawa, Katani, Pareto, Nafaka na Mazao Mchanganyiko ili kupata masoko katika Nchi Jirani na penginepo na taarifa kupatikana mtandaoni - E-Masoko.
  11. Asababishe upitiaji upya wa ufanisi na uongozi wa Bodi hizi.
  12. Asababishe upatikanaji wa mapema na kwa haraka kwa Takwimu za Mazao ya Kilimo kwa mtandao - E-Takwimu.
  13. Asababishe Uondoshaji/Upunguzaji wa vizuizi vya barabarani kwa mazao ya Kilimo.
  14. Asababishe elimu zaidi, matumizi lizoweka na matangazo kuihusu 'Tanzania Mercantile Exchange Plc'.
  15. Asababishe Serikali kununua ziada ya mazao toka kwa Wakulima.
  16. Asababishe uangaliwaji kwa jicho la upendeleo Sekta ya 'Horticulture' kwani inataabika sana hasa biashara ya maua n.k.
  17. Asababishe uanzishwaji wa utaratibu wa mara kwa mara wa kukutana na Wakulima ('Round Table') ili kufanya utatuzi wa haraka wa matatizo yao.
Kwa sasa haya yanatosha,nafikiri wengine wataongezea...
Bashe wewe upo Kilimo peke yake,ni vema.
Hizo asilimia ulizoweka za uchangiaji wa pato la Taifa unazihusisha na sekta ya
Mifugo,Uvuvi Misitu na Huduma za ughani.
Na kwa maana hiyo shughuli ndogo ya uzalishaji mazao ambayo ndo utashughulika nayo inachangia pato la Taifa chini sana ya hizo asilimia ulizoandika.
Kwa mujibu wa Kitabu cha Hali ya Uchumi Tanzania 2018,sekta ya Kilimo(mazao,misitu,uvuvi,ufugaji na ugani) inachangia asilimia 28.2 katika Pato la Taifa.
Ili kuondoa umaskini wa watu wetu ni lazima hii sekta ikue kwa asilimi 8 hadi 10 kwa miaka 10 fululizo.
Kwa sasa ukuaji wake inasuasua na ukuaji wake unacheza kwenye asilimia 5.3.
Mkihakikisha kuwa kwenye maeneo yenye mito mikubwa skimu za umwagiliaji zitatengenezwa ili kuimarisha kilimo cha umwagiliaji basi mtakuwa mmefanya jambo jema sana.
Tengenezeni pia mabwawa makubwa ya kuvunia maji kwa ajili ya kutumia nyakati za kiangazi kwa kilimo.
Mbolea ziwafikie wakulima kwa wakati.
Masoko kwa wakulima yatafutwe,na hili ni kwa mazao yote.
Ikiwezekana muimarishe hifadhi ya chakula na mazao.
 
Kilio changu bank ya maendeleo ya kilimo TADB wapokee dhamana ya hati ya shamba hata kama
(1) Shamba atakalo lima mkulima lipo mkoa tofauti na shamba analowekea dhamana ya mkopo.
(2) Shamba linalotumika kama dhamana halina nyumba.Hili shariti sio lenye tija.
Kwanini namba 1.
Mtu anaweza kuwa anataka kulima zao flani linalohitaji hali ya hewa flani tofauti na shamba lake lilipo.
Anaweza kulima kwa mkataba na watu wa soko hivyo amepewa shariti mazao afikishe kwa kampuni aliyoingia nayo mkataba mkoa tofauti na anakomiliki shembe lenye hati. Kwa kupunguza gharama za usafiri anaweza kulima karibu na masoko.
Mfano mwingine unakuta mkulima anaishi Dar, shamba lenye hati lipo Arusha, Anataka kulima Morogoro au Pwani sababu ya ukaribu aweze kusimamia vizuri mwenyewe huku akiendelea na shughuli zingine Dar.
Kwanini nambari 2?
Kuna mashamba ya mabondeni ambayo masika yanafurika maji, huwa yanalimwa kiangazi tu kwa umwagiliaji.
Kutokana na kufurika maji haiwezekani kujenga nyumba ya kudumu.
Ombi la mwisho kwa leo
Serikali ifanye jitihada kuleta wawekezaji na yenyewe itoe vibali kirahisi vya maduka ya kemikali za kuboresha usindikaji ili kuzuia bidhaa zisioze haraka.
Pia ningeomba serikali ifute tozo/kodi kwenye hizo kemikali na vifungashio.
Sijafuatlia bajeti mpya ya 2019/2020 huenda wamefanya hivyo.
Kwanini wafanye hivyo?
Tuna mazao ya matunda na mboga mboga ambazo tunaweza kuongeza thamani.
Mazao yanaoza kirahisi wakulima wanakula hasara wakati watu tuna ujuzi wa kuchakata na kuongeza thamani.
Mfano nyanya zinaoza nyingi mno kila mwaka hasa kuanzia mwezi wa 8 hadi wa 9. Rahisi sana kutengeneza tomato paste, tomato pulp, chilli sauce n.k. Tatizo kupata kemikali ya kuifanya tomato iwe nzito sio rahisi kwa mjasiriamali wa kawaida.
Ombi la kodi ya kemikali na vifungashio liambatane na msamaha wa kodi kwenye mashine ndogo ndogo za kuchakata na kuongeza thamani mazao.
Hizi mashine zitawalenga wajasiriamali wadogo wadogo wanaoweza kutawanyika hadi vijijini mikoani kwa wakulima ambao hawafikiwi na akina Azam, Dabaga, Red Gold.
Haiwezekani mwezi wa 8 au 9 mkulima auze ndoo ya nyanya 3000/- zingine anafukia kwa kukosa soko kisha mwezi wa 12 auze ndoo hiyo hiyo kwa 20,000/-.
 
Chief Instigator umeongelea maeneo muhimu sana.. Hasa umilikaji wa mashamba. Inabidi iwe rahisi sana kusajili na kupata hati hasa za mashamba ili iwe rahisi kukopa.
Pia suala la kuongeza thamani. Mfano 'paste' au 'pulp' za matunda kama maembe na machungwa kwa ajili ya kutengeneza vinyaji vya 'Juice' zinatoka Kenya ijapokuwa Tanzania kuna matunda yanaozea mashambani..
 
Wajasiriamali wenye viwanda vidogo nilivyo gusia juu ndio wakombozi kwa maeneo ambayo wawekezaji wakubwa hawawezi kwenda kujenga viwanda kutokana na uzalishaji wa wakulima wadowadogo kuto kidhi mahitaji ya kiwanda kikubwa.

Hao wakubwa wanakwepa hasara miezi ambayo watakosa malighafi(mazao). Hasa ukuzingatia wakulima wengi wadogo wadogo nchini hutegemea kilimo cha mvua za msimu.
 
Nimefungua huu uzi ili kuweza kumshauri Naibu Waziri Hussein Bashe katika Wizara yake ya Kilimo. Kama alivyosema Kilimo ni Biashara lakini Kilimo kina changamoto za kutosha ambazo Watendaji na Mawaziri ama hawazielewi au hawazitilii maanani.
Huu ni ushauri tu kwa Naibu Waziri Bashe. Akiuzingatia tutakwenda mbele, akipuuza atakuwa kama Mawaziri wengine waliopita.
Katika Tanzania Kilimo kinachangia asilimia karibu 29% katika GDP na Watanzania karibu asilimia 65.5% - 70% ni Wakulima ama wanajishughulisha na bidhaa za Kilimo. Nitatumia neno Asababishe kwani najua Waziri ndiyo yupo juu yake.
Ushauri wenyewe ni huu..
  1. Asababishe kufanyika kwa sensa ya maeneo ya Kilimo Tanzania(kwa kiwango cha kata) na mahitaji yao.
  2. Asababishe yale maeneo maarufu kwa Kilimo yana angalau matrekta 2 kwa kila kata yakiwa na vifaa vyake kama majembe,'planters','harrows',harvesters',n.k. ili wakulima waweze kulima kwa bei nafuu na kwa haraka Zaidi.
  3. Asababishe Mbolea inafika maeneo ya mashambani kwa wakati kabla ya msimu wa kupanda.
  4. Asababishe mawasiliano na Wizara ya Nishati ili kujua ni kwa nini Mbolea ya Minjingu haipendwi na Wakulima na madhara yake.
  5. Asababishe utoaji wa haraka wa Pembejeo za Kilimo Bandarini ili kuwahi misimu ya Kilimo.
  6. Asababishe kuanzishwa kwa ofisi ndogo za Wizara ya Kilimo Mipakani ili kurahisisha utoaji wa Vibali vya mauzo ya mazao nje.
  7. Asababishe kurahisisha biashara ya Mazao nje hasa nchi jirani.
  8. Asababishe kuangaliwa kwa utaratibu mzuri wa kurudisha hela za Sukari('15% Import Duty Refunds') kwa viwanda vikubwa kwa kuwa Viwanda vinataabika sana na vingine viko mbioni kusimama. Hili ni kubwa kwani linaathiri utendaji wa baadhi ya Viwanda.
  9. Asababishe kuundwa kwa Kamati ya Uratibu ya Wizara ya Kilimo, Viwanda(SIDO) na Fedha ili kutatua changamoto zinazojitokeza katika shughuli za Ujasiriamali na Viwanda vidogovidogo.
  10. Asababishe kuanzishwa kwa Idara ya Masoko ambayo itafanyanya kazi na Bodi za Tumbaku, Sukari, Chai, Korosho, Pamba, Kahawa, Katani, Pareto, Nafaka na Mazao Mchanganyiko ili kupata masoko katika Nchi Jirani na penginepo na taarifa kupatikana mtandaoni - E-Masoko.
  11. Asababishe upitiaji upya wa ufanisi na uongozi wa Bodi hizi.
  12. Asababishe upatikanaji wa mapema na kwa haraka kwa Takwimu za Mazao ya Kilimo kwa mtandao - E-Takwimu.
  13. Asababishe Uondoshaji/Upunguzaji wa vizuizi vya barabarani kwa mazao ya Kilimo.
  14. Asababishe elimu zaidi, matumizi na matangazo kuihusu 'Tanzania Mercantile Exchange Plc'.
  15. Asababishe Serikali kununua ziada ya mazao toka kwa Wakulima.
  16. Asababishe uangaliwaji kwa jicho la upendeleo Sekta ya 'Horticulture' kwani inataabika sana hasa biashara ya maua n.k.
  17. Asababishe uanzishwaji wa utaratibu wa mara kwa mara wa kukutana na Wakulima ('Round Table') ili kufanya utatuzi wa haraka wa matatizo yao.
Kwa sasa haya yanatosha,nafikiri wengine wataongezea...
18.. Ahakikishe Soko la Mbaazi, choroko, Korosho linarudi kama zamani.Afanyie kazi failure ya MOU kati ya Tanzania na India juu ya Mbaazi..Kwanini Mlawai na Msumbiji waweze sisi tunashindwa nini kunegotiate??
 
Nimefungua huu uzi ili kuweza kumshauri Naibu Waziri Hussein Bashe katika Wizara yake ya Kilimo. Kama alivyosema Kilimo ni Biashara lakini Kilimo kina changamoto za kutosha ambazo Watendaji na Mawaziri ama hawazielewi au hawazitilii maanani.
Huu ni ushauri tu kwa Naibu Waziri Bashe. Akiuzingatia tutakwenda mbele, akipuuza atakuwa kama Mawaziri wengine waliopita.
Katika Tanzania Kilimo kinachangia asilimia karibu 29% katika GDP na Watanzania karibu asilimia 65.5% - 70% ni Wakulima ama wanajishughulisha na bidhaa za Kilimo. Nitatumia neno Asababishe kwani najua Waziri ndiyo yupo juu yake.
Ushauri wenyewe ni huu..
  1. Asababishe kufanyika kwa sensa ya maeneo ya Kilimo Tanzania(kwa kiwango cha kata) na mahitaji yao.
  2. Asababishe yale maeneo maarufu kwa Kilimo yana angalau matrekta 2 kwa kila kata yakiwa na vifaa vyake kama majembe,'planters','harrows',harvesters',n.k. ili wakulima waweze kulima kwa bei nafuu na kwa haraka Zaidi.
  3. Asababishe Mbolea inafika maeneo ya mashambani kwa wakati kabla ya msimu wa kupanda.
  4. Asababishe mawasiliano na Wizara ya Nishati ili kujua ni kwa nini Mbolea ya Minjingu haipendwi na Wakulima na madhara yake.
  5. Asababishe utoaji wa haraka wa Pembejeo za Kilimo Bandarini ili kuwahi misimu ya Kilimo.
  6. Asababishe kuanzishwa kwa ofisi ndogo za Wizara ya Kilimo Mipakani ili kurahisisha utoaji wa Vibali vya mauzo ya mazao nje.
  7. Asababishe kurahisisha biashara ya Mazao nje hasa nchi jirani.
  8. Asababishe kuangaliwa kwa utaratibu mzuri wa kurudisha hela za Sukari('15% Import Duty Refunds') kwa viwanda vikubwa kwa kuwa Viwanda vinataabika sana na vingine viko mbioni kusimama. Hili ni kubwa kwani linaathiri utendaji wa baadhi ya Viwanda.
  9. Asababishe kuundwa kwa Kamati ya Uratibu ya Wizara ya Kilimo, Viwanda(SIDO) na Fedha ili kutatua changamoto zinazojitokeza katika shughuli za Ujasiriamali na Viwanda vidogovidogo.
  10. Asababishe kuanzishwa kwa Idara ya Masoko ambayo itafanyanya kazi na Bodi za Tumbaku, Sukari, Chai, Korosho, Pamba, Kahawa, Katani, Pareto, Nafaka na Mazao Mchanganyiko ili kupata masoko katika Nchi Jirani na penginepo na taarifa kupatikana mtandaoni - E-Masoko.
  11. Asababishe upitiaji upya wa ufanisi na uongozi wa Bodi hizi.
  12. Asababishe upatikanaji wa mapema na kwa haraka kwa Takwimu za Mazao ya Kilimo kwa mtandao - E-Takwimu.
  13. Asababishe Uondoshaji/Upunguzaji wa vizuizi vya barabarani kwa mazao ya Kilimo.
  14. Asababishe elimu zaidi, matumizi na matangazo kuihusu 'Tanzania Mercantile Exchange Plc'.
  15. Asababishe Serikali kununua ziada ya mazao toka kwa Wakulima.
  16. Asababishe uangaliwaji kwa jicho la upendeleo Sekta ya 'Horticulture' kwani inataabika sana hasa biashara ya maua n.k.
  17. Asababishe uanzishwaji wa utaratibu wa mara kwa mara wa kukutana na Wakulima ('Round Table') ili kufanya utatuzi wa haraka wa matatizo yao.
Kwa sasa haya yanatosha,nafikiri wengine wataongezea...
KOROSHOOO KOROSHOO KOROSHO KOROSHOOOOOK
 
18.. Ahakikishe Soko la Mbaazi, choroko, Korosho linarudi kama zamani.Afanyie kazi failure ya MOU kati ya Tanzania na India juu ya Mbaazi..Kwanini Mlawai na Msumbiji waweze sisi tunashindwa nini kunegotiate??
Bashe amekuwepo 'Private sector' na anafahamu changamoto za biashara na anaweza kuwa 'negotiator' mzuri.. Basi amsaidie Waziri wake kuongea na hawa Wafanyabiashara... Kama 'limits' za kisiasa na kiitifaki katika Wizara zitakuwa huru, hii inaweza kuwa 'winning team'..
 
Nimefungua huu uzi ili kuweza kumshauri Naibu Waziri Hussein Bashe katika Wizara yake ya Kilimo. Kama alivyosema Kilimo ni Biashara lakini Kilimo kina changamoto za kutosha ambazo Watendaji na Mawaziri ama hawazielewi au hawazitilii maanani.
Huu ni ushauri tu kwa Naibu Waziri Bashe. Akiuzingatia tutakwenda mbele, akipuuza atakuwa kama Mawaziri wengine waliopita.
Katika Tanzania Kilimo kinachangia asilimia karibu 29% katika GDP na Watanzania karibu asilimia 65.5% - 70% ni Wakulima ama wanajishughulisha na bidhaa za Kilimo. Nitatumia neno Asababishe kwani najua Waziri ndiyo yupo juu yake.
Ushauri wenyewe ni huu..
  1. Asababishe kufanyika kwa sensa ya maeneo ya Kilimo Tanzania(kwa kiwango cha kata) na mahitaji yao.
  2. Asababishe yale maeneo maarufu kwa Kilimo yana angalau matrekta 2 kwa kila kata yakiwa na vifaa vyake kama majembe,'planters','harrows',harvesters',n.k. ili wakulima waweze kulima kwa bei nafuu na kwa haraka Zaidi.
  3. Asababishe Mbolea inafika maeneo ya mashambani kwa wakati kabla ya msimu wa kupanda.
  4. Asababishe mawasiliano na Wizara ya Nishati ili kujua ni kwa nini Mbolea ya Minjingu haipendwi na Wakulima na madhara yake.
  5. Asababishe utoaji wa haraka wa Pembejeo za Kilimo Bandarini ili kuwahi misimu ya Kilimo.
  6. Asababishe kuanzishwa kwa ofisi ndogo za Wizara ya Kilimo Mipakani ili kurahisisha utoaji wa Vibali vya mauzo ya mazao nje.
  7. Asababishe kurahisisha biashara ya Mazao nje hasa nchi jirani.
  8. Asababishe kuangaliwa kwa utaratibu mzuri wa kurudisha hela za Sukari('15% Import Duty Refunds') kwa viwanda vikubwa kwa kuwa Viwanda vinataabika sana na vingine viko mbioni kusimama. Hili ni kubwa kwani linaathiri utendaji wa baadhi ya Viwanda.
  9. Asababishe kuundwa kwa Kamati ya Uratibu ya Wizara ya Kilimo, Viwanda(SIDO) na Fedha ili kutatua changamoto zinazojitokeza katika shughuli za Ujasiriamali na Viwanda vidogovidogo.
  10. Asababishe kuanzishwa kwa Idara ya Masoko ambayo itafanyanya kazi na Bodi za Tumbaku, Sukari, Chai, Korosho, Pamba, Kahawa, Katani, Pareto, Nafaka na Mazao Mchanganyiko ili kupata masoko katika Nchi Jirani na penginepo na taarifa kupatikana mtandaoni - E-Masoko.
  11. Asababishe upitiaji upya wa ufanisi na uongozi wa Bodi hizi.
  12. Asababishe upatikanaji wa mapema na kwa haraka kwa Takwimu za Mazao ya Kilimo kwa mtandao - E-Takwimu.
  13. Asababishe Uondoshaji/Upunguzaji wa vizuizi vya barabarani kwa mazao ya Kilimo.
  14. Asababishe elimu zaidi, matumizi na matangazo kuihusu 'Tanzania Mercantile Exchange Plc'.
  15. Asababishe Serikali kununua ziada ya mazao toka kwa Wakulima.
  16. Asababishe uangaliwaji kwa jicho la upendeleo Sekta ya 'Horticulture' kwani inataabika sana hasa biashara ya maua n.k.
  17. Asababishe uanzishwaji wa utaratibu wa mara kwa mara wa kukutana na Wakulima ('Round Table') ili kufanya utatuzi wa haraka wa matatizo yao.
Kwa sasa haya yanatosha,nafikiri wengine wataongezea...
Kabla hajaanza kuyapitia hayo mapendekezo yako usishangae katumbuliwa au kahamishwa wizara
 
tatizo yeye ni naibu waziri sio waziri kamili hana mamlaka yote hayo
Tatizo siyo mamlaka bali Ushawishi... kabla ya kwenda kwenye vikao vya Baraza la Mawaziri, Waziri lazima akae na timu yake na kuelewa kuwa ni Sera gani hasa anaenda kutetea na kwa nini.. Hivyo mamlaka ya Naibu Waziri hayamfanyi asishawishi..
 
Back
Top Bottom