Kigarama
JF-Expert Member
- Apr 23, 2007
- 2,492
- 1,238
Kwa takribani miaka thelathini sasa nchi yetu imekuwa katika upungufu mkubwa sana wa wanasiasa, Nchi yetu imeichukulia siasa kama sehemu ya mtu yeyote aliyepoteza mwelekeo kuwa au chimbo la kujipatia utajiri wa haraka haraka. Hali ilianza kuwa na wanasiasa uchwara mpaka sasa tulipo kuna wasiasa watapia Hatima walio kwenye siasa kwa ajili ya kuchaguliwa tu badala ya kutekeleza vile wanavyoahidi.
Tanzania tuna Dira ya Taifa (Vission 2025) kama kiongozi cha kufanya mambo yetu kuelekea kwenye mafanikio. Lakini ni nadra sana kwa "wanasiasa" wetu kuwakuta kwenye mabishano yao wakibishania kilichomo kwenye dira hiyo. Hadi wakati mwingine unajiuliza nchi yetu inaendeshwaje??
Tanzania tuna Dira ya Taifa (Vission 2025) kama kiongozi cha kufanya mambo yetu kuelekea kwenye mafanikio. Lakini ni nadra sana kwa "wanasiasa" wetu kuwakuta kwenye mabishano yao wakibishania kilichomo kwenye dira hiyo. Hadi wakati mwingine unajiuliza nchi yetu inaendeshwaje??