Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) ikiendelea kuboresha Daftari la Kudumu la Wapigakura mkoani Dar es Salaam, imesema kumejitokeza changamoto ya baadhi ya watu kujiandikisha zaidi ya mara moja katika vituo tofauti.
View attachment 3277465
INEC imesema hayo leo Machi 20, 2025 katika taarifa kwa umma kuhusu uandikishaji wapigakura mkoani Dar es Salaam, iliyosainiwa na Mkurugenzi wa Uchaguzi, Ramadhani Kailima.
Amesema baada ya uandikishaji kukamilika katika vituo, Tume huchakata taarifa za watu wote walioandikishwa kupitia mfumo maalumu (Automatic Fingerprint Identification System-AFIS), ambao una uwezo wa kuwabaini wapigakura wote waliojiandikisha zaidi ya mara moja.
Soma, Pia:
Tume ya Uchaguzi: Wapigakura milioni 34.7 wanatarajiwa kushiriki Uchaguzi mkuu Oktoba
Kailima amesema Tume pia hufanya kazi ya kulinganisha sura za watu wote waliopo kwenda daftari lengo likiwa kubaini iwapo kuna waliojiandikisha zaidi ya mara moja.
Amesema iwapo itabainika mtu amejiandikisha zaidi ya mara moja jina na taarifa za mtu huyo, hufutwa na mfumo katika vituo vingine na kubakizwa katika kituo cha mwisho alichojiandikisha katika daftari, hivyo, taarifa nyingine zote za awali hufutwa.
Chanzo: Mwananchi