Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 4,783
- 14,975
Dodoma: Zoezi la Utiaji Saini Kanuni za Maadili ya Uchaguzi Aprili 12, 2025
Vyama 18 vya Siasa Vyasaini Kanuni za Maadili ya Uchaguzi 2025
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Ramadhan Kailima, amesema kuwa jumla ya vyama 18 vya siasa vimeridhia na kusaini Kanuni za Maadili ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani kwa mwaka 2025.
Vyama vilivyosaini kanuni hizo ni:
Vyama ambavyo havijasaini havitashiri uchaguzi
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele, ametangaza kuwa vyama vya siasa ambavyo havitasaini au vitakataa kusaini kanuni za maadili ya uchaguzi havitaruhusiwa kushiriki katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.
Akizungumza katika kikao kilichofanyika Jumamosi, Aprili 12, 2025 jijini Dodoma, ambacho kilihusisha utiaji saini wa kanuni hizo, Jaji Mwambegele alieleza kuwa kifungu cha 162(2) cha Sheria ya Uchaguzi ya mwaka 2024 kimeweka sharti la lazima kwa kila chama na mgombea kusaini na kutekeleza kanuni za maadili kabla ya kuwasilisha fomu za uteuzi.
“Kabla ya mgombea yeyote au chama chochote kuwasilisha fomu za uteuzi, ni lazima wawe wamesaini kanuni za maadili ya uchaguzi, pamoja na kuonyesha dhamira ya kuzifuata katika kipindi chote cha kampeni na mchakato mzima wa uchaguzi,” alibainisha Jaji Mwambegele.
Ameeleza kuwa hatua ya kusaini kanuni hizo si ya hiari bali ni hitaji la kisheria linalolenga kuhakikisha kuwa kila mdau wa uchaguzi anazingatia misingi ya maadili, kwa ajili ya kuendesha kampeni na uchaguzi kwa njia ya haki, amani na usawa.
“Lengo kuu ni kuthibitisha kwa pamoja kuwa vyama vyote na wagombea wapo tayari kuendesha uchaguzi kwa kuzingatia maadili, taratibu na sheria zilizowekwa,” aliongeza.
Kikao hicho ni sehemu ya mchakato wa maandalizi ya Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika baadaye mwaka huu, ambapo vyama vya siasa vilialikwa kushiriki katika tukio hilo muhimu mbele ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi, kama ishara ya mshikamano na uwajibikaji katika kuhakikisha uchaguzi huru na wa haki.
Vyama 18 vya Siasa Vyasaini Kanuni za Maadili ya Uchaguzi 2025
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Ramadhan Kailima, amesema kuwa jumla ya vyama 18 vya siasa vimeridhia na kusaini Kanuni za Maadili ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani kwa mwaka 2025.
Vyama vilivyosaini kanuni hizo ni:
- AAFP
- ACT-Wazalendo
- ADA-TADEA
- ADC
- CCK
- CCM
- CHAUMA
- CUF
- MAKINI
- DP
- NCCR-Mageuzi
- NLD
- NRA
- SAU
- TLP
- UDP
- UMD
- UPDP
Vyama ambavyo havijasaini havitashiri uchaguzi
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele, ametangaza kuwa vyama vya siasa ambavyo havitasaini au vitakataa kusaini kanuni za maadili ya uchaguzi havitaruhusiwa kushiriki katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.
Akizungumza katika kikao kilichofanyika Jumamosi, Aprili 12, 2025 jijini Dodoma, ambacho kilihusisha utiaji saini wa kanuni hizo, Jaji Mwambegele alieleza kuwa kifungu cha 162(2) cha Sheria ya Uchaguzi ya mwaka 2024 kimeweka sharti la lazima kwa kila chama na mgombea kusaini na kutekeleza kanuni za maadili kabla ya kuwasilisha fomu za uteuzi.
“Kabla ya mgombea yeyote au chama chochote kuwasilisha fomu za uteuzi, ni lazima wawe wamesaini kanuni za maadili ya uchaguzi, pamoja na kuonyesha dhamira ya kuzifuata katika kipindi chote cha kampeni na mchakato mzima wa uchaguzi,” alibainisha Jaji Mwambegele.
Ameeleza kuwa hatua ya kusaini kanuni hizo si ya hiari bali ni hitaji la kisheria linalolenga kuhakikisha kuwa kila mdau wa uchaguzi anazingatia misingi ya maadili, kwa ajili ya kuendesha kampeni na uchaguzi kwa njia ya haki, amani na usawa.
“Lengo kuu ni kuthibitisha kwa pamoja kuwa vyama vyote na wagombea wapo tayari kuendesha uchaguzi kwa kuzingatia maadili, taratibu na sheria zilizowekwa,” aliongeza.
Kikao hicho ni sehemu ya mchakato wa maandalizi ya Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika baadaye mwaka huu, ambapo vyama vya siasa vilialikwa kushiriki katika tukio hilo muhimu mbele ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi, kama ishara ya mshikamano na uwajibikaji katika kuhakikisha uchaguzi huru na wa haki.