Civilian Coin
JF-Expert Member
- Dec 2, 2012
- 2,305
- 4,334
Katika hali isiyo ya kawaida, uchaguzi mdogo wa marudio wa Udiwani kata ya Nyampulukano, jimbo la Sengerema mwaka 2013. Uchaguzi huo mdogo ulikuwa na kashkash nyingi sana na za kukatana na mapanga, siku ya jumapili ambayo ilikuwa ni ndio siku ya kupiga kura, kila chama kilikuwa kinazunguukia vituo vya kupiga kura.
Gari ndogo iliyokuwa inatumiwa na viongozi wa chama cha NCCR Mageuzi ambayo ilikuwa na Katibu wa wilaya wa Nccr Mageuzi wa Sengerema, pia alikuwemo Katibu wa Uenezi wa Vijana Taifa wa NCCR Mageuzi Ndugu Deogratius Kisandu, kwasasa yuko CCM. Na mwanachama mmoja na dreva. Walisimamishwa kona ya kuingia eneo la kupigia kura na waandishi wa habari na maaskari wawili tuliokuwa nao katika uchaguzi huo.
Waandishi waliuliza mbona mnaingia eneo hili, tukawaambia sisi ndio wenye uchaguzi na wasimamizi kupitia chama huku wakichukua video kwa kurekodi mazungumzo.
Cha kushangaza kesho yake Star Tv wakarusha kwenye Taarifa ya habari kwamba wale walikuwa ni Magaidi na majambazi, tena wakimtaja ndg. Deogratius Kisandu ambaye alikuwa msimamizi mkuu wa Uchaguzi kutoka Taifa upande wa chama cha Nccr Mageuzi.
Kitendo hiki cha udhalilishaji kuna haja Tume ya Uchaguzi kufungua kesi kudhalilishwa kwa wasimamizi wa uchaguzi, na Wanasiasa kuishitaki Star Tv kwa kupotosha Umma kwa kuzusha Mtanzania mwenzetu ni Gaidi na jambazi, kumbe anasimamia uchaguzi.
Deogratius Kisandu, yeye amekwisha jiandaa kufungua kesi ya udhalilishaji na anataka kulipwa Trioni 5 kama fidia za kumfezehesha kwa jamii.
Taifa linaenda wapi
Gari ndogo iliyokuwa inatumiwa na viongozi wa chama cha NCCR Mageuzi ambayo ilikuwa na Katibu wa wilaya wa Nccr Mageuzi wa Sengerema, pia alikuwemo Katibu wa Uenezi wa Vijana Taifa wa NCCR Mageuzi Ndugu Deogratius Kisandu, kwasasa yuko CCM. Na mwanachama mmoja na dreva. Walisimamishwa kona ya kuingia eneo la kupigia kura na waandishi wa habari na maaskari wawili tuliokuwa nao katika uchaguzi huo.
Waandishi waliuliza mbona mnaingia eneo hili, tukawaambia sisi ndio wenye uchaguzi na wasimamizi kupitia chama huku wakichukua video kwa kurekodi mazungumzo.
Cha kushangaza kesho yake Star Tv wakarusha kwenye Taarifa ya habari kwamba wale walikuwa ni Magaidi na majambazi, tena wakimtaja ndg. Deogratius Kisandu ambaye alikuwa msimamizi mkuu wa Uchaguzi kutoka Taifa upande wa chama cha Nccr Mageuzi.
Kitendo hiki cha udhalilishaji kuna haja Tume ya Uchaguzi kufungua kesi kudhalilishwa kwa wasimamizi wa uchaguzi, na Wanasiasa kuishitaki Star Tv kwa kupotosha Umma kwa kuzusha Mtanzania mwenzetu ni Gaidi na jambazi, kumbe anasimamia uchaguzi.
Deogratius Kisandu, yeye amekwisha jiandaa kufungua kesi ya udhalilishaji na anataka kulipwa Trioni 5 kama fidia za kumfezehesha kwa jamii.
Taifa linaenda wapi