Tume ya Taifa ya Uchaguzi ni Tume huru

Tume ya Taifa ya Uchaguzi ni Tume huru

sanshinda

Member
Joined
Sep 25, 2017
Posts
79
Reaction score
33
Ibara ya 74 (1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977 inatamka kwamba,

“Kutakuwa na Tume ya Uchaguzi ya Jamhuri ya Muungano ambayo itakuwa na wajumbe wafuatao watakaoteuliwa na Rais:

(a) Jaji wa Mahakama Kuu au Jaji wa Mahakama ya Rufani, ambaye atakuwa mwenyekiti;
(b) Makamu Mwenyekiti ambaye atakuwa mtu anayeshika, aliyewahi kushika au anayestahili
kuteuliwa kushika madaraka ya Jaji wa Mahakama Kuu au Jaji wa Mahakama ya Rufani;
(c) Wajumbe wengine watakaotajwa na sheria iliyotungwa na Bunge”.

Ibara ya 74 (7) ya Katiba inasema kwa madhumuni ya utekelezaji bora wa majukumu yake yaliyoainishwa katika ibara hii, Tume ya Uchaguzi itakuwa ni idara huru inayojitegemea, itafanya maamuzi yake rasmi kuhusu utekelezaji wa majukumu yake kwa vikao, na mtendaji wake mkuu atakuwa ni Mkurugenzi wa Uchaguzi ambaye atateuliwa na kufanya kazi kwa mujibu wa masharti ya sheria iliyotungwa na Bunge.
 
Ituambie wasimamizi wa uchaguzi waliitwa kufanya nini ikulu na mwenyekiti wa ccm.
 
Sasa kama Tume ni huru hao wanaodai wanadai nini? Au hawasomi Katiba?
 
Sasa hapa umeonesha uhuru wa tume au muundo wa tume ndugu
 
Kwani Jafo ana mamlaka gani ndani ya tume hadi aweze kutengua maamuzi ya Tume ya uchaguzi?
 
Hii Ibara ni ya 1977 wakati tuna utawala wa chama kimoja, au vyama vingi vilikuwepo mkuu?
 
Ibara ya 74 (1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977 inatamka kwamba,

“Kutakuwa na Tume ya Uchaguzi ya Jamhuri ya Muungano ambayo itakuwa na wajumbe wafuatao watakaoteuliwa na Rais:

(a) Jaji wa Mahakama Kuu au Jaji wa Mahakama ya Rufani, ambaye atakuwa mwenyekiti;
(b) Makamu Mwenyekiti ambaye atakuwa mtu anayeshika, aliyewahi kushika au anayestahili
kuteuliwa kushika madaraka ya Jaji wa Mahakama Kuu au Jaji wa Mahakama ya Rufani;
(c) Wajumbe wengine watakaotajwa na sheria iliyotungwa na Bunge”.

Ibara ya 74 (7) ya Katiba inasema kwa madhumuni ya utekelezaji bora wa majukumu yake yaliyoainishwa katika ibara hii, Tume ya Uchaguzi itakuwa ni idara huru inayojitegemea, itafanya maamuzi yake rasmi kuhusu utekelezaji wa majukumu yake kwa vikao, na mtendaji wake mkuu atakuwa ni Mkurugenzi wa Uchaguzi ambaye atateuliwa na kufanya kazi kwa mujibu wa masharti ya sheria iliyotungwa na Bunge.

Na hii ndio tume huru?

Aisee tumeisha!
 
Back
Top Bottom