Tume Huru ya Uchaguzi anayotaka Mkapa & Wapinzani ni ipi? Au kama hii ya Ghana? Nani anatupatia?

Isike Moses

JF-Expert Member
Feb 12, 2013
2,789
4,243
Ghana ndiyo Taifa linalo tolewa mfano wa kuwa na Demokrasia safi ya Uchaguzi wa kisiasa Africa. Hoja hii inatokana na kile kinachoelezwa kuwa uwepo wa Tume Huru ya Uchaguzi (EC). Kwa mujibu wa Katiba ya Ghana ya 1992 imeweka namna tume hiyo inaundwa, majukumu yake, chanzo chake cha fedha na ukomo wa wajumbe. Rais kwa kushirikisha Baraza Kuu la Nchi (Council of State) na Bunge ndiyo mamlaka zinazofanya kazi ya kuunda Tume yenye wajumbe saba (7). Baraza Kuu hilo linajumuisha wajumbe kutoka taaisisi mbalimbali binafsi, asasi za kiraia, vyama vyote vya siasa na watu binafasi. Lazima mchakato uwe wa majadiliano ya kina,kwa hiyo Rais siyo mwenye maamuzi ya mwisho ya uteuzi wa wajumbe hao.

Baada ya Tume yenye wajumbe 7 kuundwa, katiba inaeleza kinga kwa wajumbe wote kuwa; 1. Kila mjumbe akishateuliwa, hawezi kuondolewa hadi atimize umri wa miaka sabini. 2. Ikiwa mjumbe ataumwa basi chombo huru cha madaktari kitaundwa ili kuchunguza na kutoa taarifa kama anafaa kuendelea au hapana (incapacity) 3. Kama mjumbe ametenda kosa kwa mujibu wa sheria, pia chombo huru cha kimahakama kitaundwa na kutoa taarifa 4. Fedha za kuendesha shughuri za Tume hazitoki kwa huruma /hisani ya Rais bali kuna Consolidated Account ya Tume ambayo Rais hana mamlaka nayo. Hii ni akaunti ambayo sehemu ya mapato ya nchi yanaingizwa moja kwa moja kama makusanyo ya kodi n.k kama yanavyoingizwa Hazina ya Taifa (Treasure).Mishahara na gharama zingine zinatoka kwenye akaunti hiyo ya pamoja. Yani Rais hawezi kusema msiingize pesa kule au punguzeni pesa za Tume. 5. Wajumbe hawalazimishwi kutenda kwa maelekezo au shurti toka kwa mtu au chombo chochote. Yani Mfano Rais aseme 'Ole wenu mumtangaze mpinzani mshindi'! Kwao Ghana hili ni kosa na linatosha kuondoa uhalali wa matokeo ya uchaguzi.

Katika kuipa Tume uhuru na uwezo zaidi wa kiutendaji, Ghana wakaunda kamati maalumu yenye wajumbe kutoka vyama vyote vya siasa (Inter-Party Advisory Committee). Moja ya jukumu kubwa ni kufanya vikao kujadili madhaifu na kushauri Tume namna bora zaidi ya kuendesha uchaguzi. Mwaka 2012, IPAC ilishauri kuwa Tume ione umuhimu wa kuendelea kuandikisha wapiga kura hata kama kampeni tayari zimeanza,hii ilifanya raia wengi zaidi kushiriki upigaji kura.

…………………………………………..
TUME YETU

Kwa mujibu wa Katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, sura ya tatu, sehemu ya pili ibara ya 74 (1-15) inataja uwepo wa Tume ya Taifa ya uchaguzi,muundo na majukumu yake. Inaeleza kuwa Rais ndiye mwenye mamlaka ya kuteua wajumbe (Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti, Mkurugenzi Mkuu wa uchaguzi na wengine) wa Tume na ndiye mwenye mamlaka ya kutengua teuzi zao. Katiba imeweka sababu zinazoweza kutumiwa na Rais kumuondoa madarakani mjumbe/wajumbe wa Tume; Ibara ya 74 (5) inataja kuwa Rais aweza tu kumwondoa katika madaraka Mjumbe wa Tume ya Uchaguzi kwa sababu ya kushindwa kutekeleza kazi zake, ama kutokana na maradhi au sababu nyingine yoyote, au kwa sababu ya tabia mbaya au kupoteza sifa za kuwa mjumbe.

Moja ya sifa kuu ya kuwa mjumbe wa Tume ni sharti usiwe mwanachama wa chama chochote cha siasa bali unabakiza HAKI ya kupiga kura; Ibara ndogo ya (14) inataja kuwa itakuwa ni marufuku kwa watu wanaohusika na uchaguzi kujiunga na chama chochote cha siasa, isipokuwa tu kwamba kila mmoja wao atakuwa na haki ya kupiga kura iliyotajwa katika ibara ya 5 ya Katiba hii. Ibara ya 15 inaendelea kueleza kuwa kwa madhumuni ya ibara ndogo ya (14) watu wanaohusika na uchaguzi ni-
(a) Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi,
(b) Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi,
(c) Wajumbe wote wa Tume ya Uchaguzi,
(d) Mkurugenzi wa Uchaguzi pamoja na watumishi wote wa Tume ya Uchaguzi,
(e) Wasimamizi wote wa Uchaguzi katika miji na wilaya zote.

NOTE: Wakurugenzi wa wilaya (DED) ndiyo wasimamizi wa shughuri za uchaguzi kwa Tanzania. Hawa ni makada wa chama cha siasa na ni wateule wa Rais wa moja kwa moja.


Tujadili…….
 
Aina hii ya tume ya uchaguzi inaweza kupatikana pale tu wale wanaoamini kuwa hawawezi kuondolewa kwa mujibu wa matakwa ya wananchi madarakani kwa njia ya makaratasi watakapoondolewa kwa bunduki. Wakishanyan'ganywa madaraka kwa mtutu ndipo akili zao zitafunguliwa na kuelewa unuhimu wa kuheshimu maamuzi ya wananchi ambao ndio wenye nchi yao.
 
Aina hii ya tume ya uchaguzi inaweza kupatikana pale tu wale wanaoamini kuwa hawawezi kuondolewa kwa mujibu wa matakwa ya wananchi madarakani kwa njia ya makaratasi watakapoondolewa kwa bunduki. Wakishanyan'ganywa madaraka kwa mtutu ndipo akili zao zitafunguliwa na kuelewa unuhimu wa kuheshimu maamuzi ya wananchi ambao ndio wenye nchi yao.
Kwa namna awamu ya 5 inavyojinasibu kufanya mambo makubwa kwa wananchi, sioni kwa nini kuwe na mkwamo wa kukubali kutekeleza hili.
 
Kwa wapinzani tuliokuwa watanzania hatuwezi kupata tume huru makosa waliyoyafanya wapinzani mwaka na mwaka 1995 ndo chanzo kikuu cha kukosekana tume guru.

Mchungaji Christopher mtikila aliwaahi kuzungumza ya kwamba wapinzani tusishiriki uchaguzi wowote ule iwe Zanzibar au bara mpka vipengele kadhaa kuhusu tume na katiba virekebishe ila wapinzani

Kwa kuwa walikuwa wana uchu na pesa za ruzuku wakashiriki matokeo yake ndo Haya mnayoyaonaa

Kwa kifupi kwa wapinzani tulionao tusahau kabisa kuhusu tume huru kwani wameshakula sana pesa za ruzuku toka serikalini na wanaendelea kula mapesa na pesa
 
Hahahah CCM sisi tukubalianr na tume ya hivi, tunakichaa ama..
emoji23.png
emoji23.png
emoji23.png
 
Kwa wapinzani tuliokuwa watanzania hatuwezi kupata tume huru makosa waliyoyafanya wapinzani mwaka na mwaka 1995 ndo chanzo kikuu cha kukosekana tume guru...

Mchungaji Christopher mtikila aliwaahi kuzungumza ya kwamba wapinzani tusishiriki uchaguzi wowote ule iwe Zanzibar au bara mpka vipengele kadhaa kuhusu tume na katiba virekebishe ila wapinzani
Kwa kuwa walikuwa wana uchu na pesa za ruzuku wakashiriki matokeo yake ndo Haya mnayoyaonaa

Kwa kifupi kwa wapinzani tulionao tusahau kabisa kuhusu tume huru kwani wameshakula sana pesa za ruzuku toka serikalini na wanaendelea kula mapesa na pesa

Sent using Jamii Forums mobile app
Tunahitaji wapinzani gani sasa ili kupata Tume Huru?
 
Kwa namna awamu ya 5 inavyojinasibu kufanya mambo makubwa kwa wananchi, sioni kwa nini kuwe na mkwamo wa kukubali kutekeleza hili.
Hakuna wakati katika historia ya Taifa hili ambapo uchaguzi huru na wa haki umegeuka kuwa adui mkubwa wa Taifa kama wakati huu. Adui mkuu wa Taifa awamu hii ni 1. Uchaguzi huru na wa haki, 2. Mfumo wa Vyama vingi vya siasa, na 3. Kukosoa matendo ya serikali hii.. Hao ndio maadui wakubwa kwa Taifa kwa sasa kwa mujibu wa huyu mungu mtu.
 
Hakuna wakati katika historia ya Taifa hili ambapo uchaguzi huru na wa haki umegeuka kuwa adui mkubwa wa Taifa kama wakati huu. Adui mkuu wa Taifa awamu hii ni 1. Uchaguzi huru na wa haki, 2. Mfumo wa Vyama vingi vya siasa, na 3. Kukosoa matendo ya serikali hii.. Hao ndio maadui wakubwa kwa Taifa kwa sasa kwa mujibu wa huyu mungu mtu.
Changamoto kubwa ni adui huyo wa 1. Tusubiri naona ACT /CHADEMA wamezindua kampeni ya kupata tume huru 😂
 
Kenya walikuja na kile kinaitwa muundo wa tume huru, yet Raila akaangukia pua. Mahakama ikatengua matokeo, akina Raila wakasusia, huku Uhuru akaendelea "kula".

Marekani ambao wanajinasibu kama mabingwa wa demokrasia, mwaka 2000 alikuwa mgombea wa Democrat Al Gore ni kama alishinda kwa wingi wa kura (popular votes). Ila tofauti ya kura 537 za jimbo la Florida pekee zikafanya Bush Jr, mgombea wa Rupublican kushinda.

Al Gore akakimbilia mahakama ya Florida kuomba kura kuhesabiwa, akina Bush wakakimbilia mahakama kuu Marekani kupinga kura kuhesabiwa.

Ni tume hii hii ambayo akina Freeman, Sugu, Msigwa, ZZK imewafanya kuwa wabunge na kupata madiwani ikiwamo kura mil 6 za Urais za EL.
Labda tuzungumze mode of staff ya tume.

Suala la msingi, mpaka sasa baadhi ya shule hazina waalimu, hatuna madaktari wa kutosha kutibu wanetu. Hatuna maafisa kilimo ambao watafanya Tanzania iwe na surplus kubwa kwenye kuzalisha mazao ya kilimo. Hatuna maafisa uvuvi wa kutosha kuhakikisha tunatosheleza soko la ndani la samaki na ikiwezekana ku-export.

Tume ikija, itajibu masuala ya huduma za maji au kuhesabu kura ambayo hata sasa kura zinahesabiwa kila kituo chini ya usimamizi wa mawakala wa vyama vya siasa, na tume hupokea karatasi kwa ajili ya majumuisho.

Tume huru tunayotaka, hata Marekani mama Clinton alipigwa kwenye uchaguzi kwa kile kinasemwa Russian intrusion
 
Kwanza kabisa naomba nikupongeze sana kwa kuwa na kiwango kikubwa cha kumeza maneno ya kukaririshwa na wale ambao kwao tume huru ya uchaguzi sio jambo la muhimu kwa kuwa tu ya sasa inawabeba. Kwa mtu mwenye uelewa wa kawaida sana anatakiwa kujua kwamba msingi wa utawala wa nchi ni wananchi wenyewe hivyo suala la kuamua nani awe kiongozi wa nchi ni suala la wananchi na sio suala la watawala. Mahitaji ya Maji, Shule na mahitaji mengine ambayo unadhani ndio mahitaji ya wananchi msingi wa utatuzi wake ni viongozi ambao wanawekwa na wananchi hivyo ili kuwa na viongozi wenye kuweza kutatua hayo kwa kiwango kikubwa na kinachoridhisha ni lazima viongozi hao wapatikane kwa uchaguzi huru na wa haki unaosimamiwa na tume huru ya uchaguzi sio vinginevyo. Ni haramu kupata huduma hizo za maji, shule NK kama tu wanaosimamia kuleta huduma hizo hawakupatikana kwa njia halali na kwa matokeo huru
Kenya walikuja na kile kinaitwa muundo wa tume huru, yet Raila akaangukia pua. Mahakama ikatengua matokeo, akina Raila wakasusia, huku Uhuru akaendelea "kula".

Marekani ambao wanajinasibu kama mabingwa wa demokrasia, mwaka 2000 alikuwa mgombea wa Democrat Al Gore ni kama alishinda kwa wingi wa kura (popular votes). Ila tofauti ya kura 537 za jimbo la Florida pekee zikafanya Bush Jr, mgombea wa Rupublican kushinda.

Al Gore akakimbilia mahakama ya Florida kuomba kura kuhesabiwa, akina Bush wakakimbilia mahakama kuu Marekani kupinga kura kuhesabiwa.

Ni tume hii hii ambayo akina Freeman, Sugu, Msigwa, ZZK imewafanya kuwa wabunge na kupata madiwani ikiwamo kura mil 6 za Urais za EL.
Labda tuzungumze mode of staff ya tume.

Suala la msingi, mpaka sasa baadhi ya shule hazina waalimu, hatuna madaktari wa kutosha kutibu wanetu. Hatuna maafisa kilimo ambao watafanya Tanzania iwe na surplus kubwa kwenye kuzalisha mazao ya kilimo. Hatuna maafisa uvuvi wa kutosha kuhakikisha tunatosheleza soko la ndani la samaki na ikiwezekana ku-export.

Tume ikija, itajibu masuala ya huduma za maji au kuhesabu kura ambayo hata sasa kura zinahesabiwa kila kituo chini ya usimamizi wa mawakala wa vyama vya siasa, na tume hupokea karatasi kwa ajili ya majumuisho.

Tume huru tunayotaka, hata Marekani mama Clinton alipigwa kwenye uchaguzi kwa kile kinasemwa Russian intrusion

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kenya walikuja na kile kinaitwa muundo wa tume huru, yet Raila akaangukia pua. Mahakama ikatengua matokeo, akina Raila wakasusia, huku Uhuru akaendelea "kula".

Marekani ambao wanajinasibu kama mabingwa wa demokrasia, mwaka 2000 alikuwa mgombea wa Democrat Al Gore ni kama alishinda kwa wingi wa kura (popular votes). Ila tofauti ya kura 537 za jimbo la Florida pekee zikafanya Bush Jr, mgombea wa Rupublican kushinda.

Al Gore akakimbilia mahakama ya Florida kuomba kura kuhesabiwa, akina Bush wakakimbilia mahakama kuu Marekani kupinga kura kuhesabiwa.

Ni tume hii hii ambayo akina Freeman, Sugu, Msigwa, ZZK imewafanya kuwa wabunge na kupata madiwani ikiwamo kura mil 6 za Urais za EL.
Labda tuzungumze mode of staff ya tume.

Suala la msingi, mpaka sasa baadhi ya shule hazina waalimu, hatuna madaktari wa kutosha kutibu wanetu. Hatuna maafisa kilimo ambao watafanya Tanzania iwe na surplus kubwa kwenye kuzalisha mazao ya kilimo. Hatuna maafisa uvuvi wa kutosha kuhakikisha tunatosheleza soko la ndani la samaki na ikiwezekana ku-export.

Tume ikija, itajibu masuala ya huduma za maji au kuhesabu kura ambayo hata sasa kura zinahesabiwa kila kituo chini ya usimamizi wa mawakala wa vyama vya siasa, na tume hupokea karatasi kwa ajili ya majumuisho.

Tume huru tunayotaka, hata Marekani mama Clinton alipigwa kwenye uchaguzi kwa kile kinasemwa Russian intrusion
Kumbe hitaji muhimu ni kutatuliwa shida za maji, hata kama kuna uvunjifu wa utawala wa sheria, hatupaswi kushughurikia kwa kuwa shida zetu za maji zinatatuliwa!
 
Sidhani kama unajitambua

SGR inaleta nini nchini kwa t.7 zinazotumika.

Ndege zimeleta hizo ajira, mishahara, nk

Tume huru na hayo kimsingi in tofauti.

Kenya walikuja na kile kinaitwa muundo wa tume huru, yet Raila akaangukia pua. Mahakama ikatengua matokeo, akina Raila wakasusia, huku Uhuru akaendelea "kula".

Marekani ambao wanajinasibu kama mabingwa wa demokrasia, mwaka 2000 alikuwa mgombea wa Democrat Al Gore ni kama alishinda kwa wingi wa kura (popular votes). Ila tofauti ya kura 537 za jimbo la Florida pekee zikafanya Bush Jr, mgombea wa Rupublican kushinda.

Al Gore akakimbilia mahakama ya Florida kuomba kura kuhesabiwa, akina Bush wakakimbilia mahakama kuu Marekani kupinga kura kuhesabiwa.

Ni tume hii hii ambayo akina Freeman, Sugu, Msigwa, ZZK imewafanya kuwa wabunge na kupata madiwani ikiwamo kura mil 6 za Urais za EL.
Labda tuzungumze mode of staff ya tume.

Suala la msingi, mpaka sasa baadhi ya shule hazina waalimu, hatuna madaktari wa kutosha kutibu wanetu. Hatuna maafisa kilimo ambao watafanya Tanzania iwe na surplus kubwa kwenye kuzalisha mazao ya kilimo. Hatuna maafisa uvuvi wa kutosha kuhakikisha tunatosheleza soko la ndani la samaki na ikiwezekana ku-export.

Tume ikija, itajibu masuala ya huduma za maji au kuhesabu kura ambayo hata sasa kura zinahesabiwa kila kituo chini ya usimamizi wa mawakala wa vyama vya siasa, na tume hupokea karatasi kwa ajili ya majumuisho.

Tume huru tunayotaka, hata Marekani mama Clinton alipigwa kwenye uchaguzi kwa kile kinasemwa Russian intrusion

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa namna awamu ya 5 inavyojinasibu kufanya mambo makubwa kwa wananchi, sioni kwa nini kuwe na mkwamo wa kukubali kutekeleza hili.

Tena awamu hii ya tano ndio haitaki kabisa hiyo tume huru, maana wanajua watu wamechoka ile mbaya, na hayo wanayotekeleza yanaweza kutekelezwa na mtu au chama chochote.
 
Changamoto kubwa ni adui huyo wa 1. Tusubiri naona ACT /CHADEMA wamezindua kampeni ya kupata tume huru 😂

Mkuu ni lini wamezindua hiyo kampeni na utaratibu ukoje? Na hilo walifanye kwa dhati sio kwa ubabaishaji, na sisi wengine tuko tayari kulipa gharama kwa hilo.
 
Kenya walikuja na kile kinaitwa muundo wa tume huru, yet Raila akaangukia pua. Mahakama ikatengua matokeo, akina Raila wakasusia, huku Uhuru akaendelea "kula".

Marekani ambao wanajinasibu kama mabingwa wa demokrasia, mwaka 2000 alikuwa mgombea wa Democrat Al Gore ni kama alishinda kwa wingi wa kura (popular votes). Ila tofauti ya kura 537 za jimbo la Florida pekee zikafanya Bush Jr, mgombea wa Rupublican kushinda.

Al Gore akakimbilia mahakama ya Florida kuomba kura kuhesabiwa, akina Bush wakakimbilia mahakama kuu Marekani kupinga kura kuhesabiwa.

Ni tume hii hii ambayo akina Freeman, Sugu, Msigwa, ZZK imewafanya kuwa wabunge na kupata madiwani ikiwamo kura mil 6 za Urais za EL.
Labda tuzungumze mode of staff ya tume.

Suala la msingi, mpaka sasa baadhi ya shule hazina waalimu, hatuna madaktari wa kutosha kutibu wanetu. Hatuna maafisa kilimo ambao watafanya Tanzania iwe na surplus kubwa kwenye kuzalisha mazao ya kilimo. Hatuna maafisa uvuvi wa kutosha kuhakikisha tunatosheleza soko la ndani la samaki na ikiwezekana ku-export.

Tume ikija, itajibu masuala ya huduma za maji au kuhesabu kura ambayo hata sasa kura zinahesabiwa kila kituo chini ya usimamizi wa mawakala wa vyama vya siasa, na tume hupokea karatasi kwa ajili ya majumuisho.

Tume huru tunayotaka, hata Marekani mama Clinton alipigwa kwenye uchaguzi kwa kile kinasemwa Russian intrusion

Huenda hujui unaloongea au unapotosha ili kutupoteza lengo. Kwanza uwepo wa tume huru lengo lake sio ili chama fulani kishinde au kushindwa, bali ni ili mgombea halali atangazwe bila shinikizo au hofu yoyote kutoka popote. Hizo nchi ulizotaja kuhusu tume huru umewahi kuona huu uhuni wa chama kushinda kwa kishindo? Huko kwenye vituo vya kura tena chini ya awamu hii, tumeona viongozi wa tume wakitangaza mshindi kwa hofu iitwayo Magufuli. Tumeona kwa macho yetu uhayawani na ukatili wa wazi dhidi ya wapinzani na bado Tume ikatangaza mshindi katika mazingira hayo. Hao akina Sugu, Mbowe nk walitangazwa wakati wa JK wakati huo kulikuwa na aibu kwa mbali. Chini ya Magufuli tume inafanya kazi kwa maagizo yake.

Ukosefu wa walimu, maji nk itaathiriwa vipi na uwepo wa tume huru ya uchaguzi? Ili waalimu, maji na huduma mbalimbali za jamii zipatikane, ni kuaacha kununua magari ya gharama kubwa (VX) kwa shughuli za serikali, misafara mikubwa ya viongozi wa serikali tena wa magari ya bei mbaya.
 
Back
Top Bottom