Tumbo la bandia labuniwa Marekani

Kurzweil

JF-Expert Member
May 25, 2011
6,622
8,397
_95788973_160705160612_foetus_babay_in_the_womb_640x360_alamy_nocredit.jpg

Wanasayansi nchini Marekani wamebuni tumbo bandia la kutengeneza ambalo katika siku zijazo linaweza kutumiwa kuwekea watoto wanaozaliwa kabla ya muda wao, maarufu kama njiti.

Kifaa hicho ambacho kipo katika mfumo wa tumbo kimejaribiwa kwa mimba ya kondoo.

Watafiti katika hospitali ya watoto ya Philadephia wanasema lengo lao ni kuweka mazingira ambayo watoto wanaozaliwa kabla muda wao kutimia wanaweza kukuza viungo vyao vya mwilini kama vile mapafu na viungo vyengine.

Kifaa hicho kimetengezwa kwa kutumia mfuko wa plastiki, uliojazwa maji ya kutengeza yanayoigiza mazingira ya tumbo la uzazi.

Wanasayansi wanaamini mfuko huo unaweza kuwa tayari kwa majaribio ya binadamu baada ya miaka mitatu mpaka mitano kuanzia sasa.

Chanzo: BBC
 
Sishangai maana wazungu hamna walichokishindwa,wameweza kila kitu isipokua kumpa roho tu mwanadamu
 
Back
Top Bottom