Tulipe jukumu rasmi jeshi letu

Amanikwenu

Senior Member
Dec 1, 2009
187
0
Kutokana na ukweli kuwa hali ya amani na majirani zeu inazidi kuimarika, kuna haja kama nchi kuliwezesha Jeshi letu na kulipa Jukumu rasmi la Kuzalisha chakula cha kutosha kwa ajili ya taifa hili. Natumaini kukiwapatia vifaa vya kutosha na utaalam unaohitajika na kuwapa Bonde la Rufiji au Kilombero, tutaona mabadiliko makubwa katika uzalishaji wa chakula hapa nchini ndani ya kipindi kisichozidi miaka mitano. Tukumbuke kuwa zaidi ya asilimia 75% ya kupanda kwa mfumuko wa bei hapa nchini inatokana na kutokuwa na chakula cha kutosha.
 
Hivi wakati ambapo hatuna vita, tuna amani asilia na hali za kisiasa ni shwari jeshi letu na wanajeshi hawa ambao wanalipwa mshahara na resheni kwa hela zetu walipa kodi hua wanafanya kazi gani?

Tukijua kazi zao ndio twawezajua kama wako underutilized au sivyo
 
Hivi wakati ambapo hatuna vita, tuna amani asilia na hali za kisiasa ni shwari jeshi letu na wanajeshi hawa ambao wanalipwa mshahara na resheni kwa hela zetu walipa kodi hua wanafanya kazi gani?

Tukijua kazi zao ndio twawezajua kama wako underutilized au sivyo

jeshi JWTZ, muda wote linatakiwa kuwa standby, huwezi kujua jirani yako anapanga nini au nani anataka kumtumia ili haiharibu amani ya nchi yako, na maana ya kuwa alert ni lazima wawe fit kwa llolotwe na wakati wowote, pili kwa dunia ya sasa kila siku kuna silaha mpya na mbinu mpya za kivita hivyo muda wote wanajeshi lazima wawe aware na hiyo new technology hivyo ni lazima wafanye mazoezi

kuhusu kilimo labda ungezungumzia JKT kwa sababu hao ndio wajenzi wa taifa
 
Nakubaliana nawe. Ila ukweli ni kuwa uwezekano wa kutokea vita na jirani zetu ni mdogo sana hata kwa miaka 100 ijayo. Binafsi naamini jeshi letu linaweza kuwa standby muda wote na wakati huohuo kutusaidia sana katika kilimo na hata kwenye masuala ya ICT kama tukiamua kuwatumia wanajeshi wetu ipasavyo na kuwapatia mafunzo maalum.
 
We unakaribisha ufisadi mwingine. JKT ilikuaje manpower ya bure na bado waliishia kutumia hela nyingi kuliko walichozalisha. Practically haiwezekani kwa system iliyopo.
 
Nakubaliana nawe. Ila ukweli ni kuwa uwezekano wa kutokea vita na jirani zetu ni mdogo sana hata kwa miaka 100 ijayo. Binafsi naamini jeshi letu linaweza kuwa standby muda wote na wakati huohuo kutusaidia sana katika kilimo na hata kwenye masuala ya ICT kama tukiamua kuwatumia wanajeshi wetu ipasavyo na kuwapatia mafunzo maalum.

Ndugu yangu sijui unatoa hoja hii kwa uelewa gani ulio nao kuhusu masuala ya ulinzi wa nchi. Nakuona wewe ni mtanzania/mwafrika halisi ambao kawaida yao huwa wanafikiria leo, ya kesho mungu atajua.

Katika sheria za ulinzi wa nchi yaani jeshi la ulinzi la nchi, hakuna muda ambao wako idle, they are on guard every hour, every minute and every second. Issue kama za uzalishaji wa vitu mbali mbali kama chakula na vitu vingine ktk viwanda, hilo linaweza kufanywa na na kuna kuwepo na units for that purpose.

Kwa Tanzania ktk JWTZ tuna idara za ujenzi wa barabara, nyumba n.k. ingawaje ni idara ya ujenzi wanyumba ndo angalau inatumika. Lakini ukweli ni kwamba huwezi kusema eti hatutarajii kuwa na vita kwani majirani wametulia.

Nikikuuliza, mgogoro wa wafanya biashara wa tanzania waliokwama malawi, unajua wanaweza wakapelekea nchi husika zikawa ktk mgogoro? Je, unajua kagame, mseven leo wanawaza nini juu ya TZ?

Unafahamu ni nani amesaidia hicho kikundi cha UN-DRC kupata baadhi ya taarifa juu ya issues za silaha kwenda kwa FDLR?

Ndugu, JWTZ pamoja na kufikiria kujishughulisha na shughuli zingine za uzalishaji mali lazima wawe tayari kwa mazoezi ya kivita kila mara kwani hujui adui atatokea wapi na lini.

Kwanza hata hatuhitaji kuwa bebesha mizigo isiyo yao wanajeshi wetu, tatizo la Tanzania kukosa chakula kila mwaka ni kuwa na watawa (mawaziri) bomu na ufisadi uliokithiri. Pesa yote ya kilimo inaiishia kwenye mikutano, semina, safari, chai, na matumizi binafsi ya watawala.
 
Kutokana na ukweli kuwa hali ya amani na majirani zeu inazidi kuimarika, kuna haja kama nchi kuliwezesha Jeshi letu na kulipa Jukumu rasmi la Kuzalisha chakula cha kutosha kwa ajili ya taifa hili. Natumaini kukiwapatia vifaa vya kutosha na utaalam unaohitajika na kuwapa Bonde la Rufiji au Kilombero, tutaona mabadiliko makubwa katika uzalishaji wa chakula hapa nchini ndani ya kipindi kisichozidi miaka mitano. Tukumbuke kuwa zaidi ya asilimia 75% ya kupanda kwa mfumuko wa bei hapa nchini inatokana na kutokuwa na chakula cha kutosha.

Haya ni mawazo yako lakini ni kuto kufikiria, tukiacha ufisadi pesa ya kuendeleza kilimo itapatikana. Hivi Barrick wanalipa kodi kiasi gani? IPTL walikuwa wanalipwa ngapi vile? Dowans? wabunge milioni......,
 
Kutokana na ukweli kuwa hali ya amani na majirani zeu inazidi kuimarika, kuna haja kama nchi kuliwezesha Jeshi letu na kulipa Jukumu rasmi la Kuzalisha chakula cha kutosha kwa ajili ya taifa hili. Natumaini kukiwapatia vifaa vya kutosha na utaalam unaohitajika na kuwapa Bonde la Rufiji au Kilombero, tutaona mabadiliko makubwa katika uzalishaji wa chakula hapa nchini ndani ya kipindi kisichozidi miaka mitano. Tukumbuke kuwa zaidi ya asilimia 75% ya kupanda kwa mfumuko wa bei hapa nchini inatokana na kutokuwa na chakula cha kutosha.

Safi!!!!

 
Pamoja na mahitaji yote na sababu zote za kiusalama zilizoainishwa hapa, je hakuna haja ya kuwahusisha hawa watu kwenye majukumu zaidi ya kijamii na kiuchumi?

Kweli kuna haja ya kuwa na wanajeshi na brigedi zote ktk kila kanda, vikosi na kambi kila mkoa wote wakiwa standbuy? Kwanini baadhi ya haya makambi pamoja na kujiweka standbuy lakini wakawa wanafasha kazi za utafiti, wakafundishwa wakawa washauri wa kilimo hasa ukizingatia kambi nyingi ziko nje ya miji na hata walimu kwenye shule zetu hizi za kata zilizoanzishwa bila mipango madhubuti ya kulinda ubora wa elimu inayotolewa.

Tuna vipaji vingi ndani ya majeshi yetu na vinaenda zaidi ya kushika mtutu na kucheza kwata siku ya uhuru na mapinduzi. Tukiwa na mikakati na nia ya dhati naimani hawa ndugu tunaweza kuwatumia kwa manufaa zaidi kuliko ilivyo sasa.
 
Ama Kweli shukurani ya punda mateke,miaka yote umelala usingizi mnono leo hii kweli hutambui JWTZ wanafanya nini?I wish ungeona yalitokea Congo, Rwanda,Msumbiji, angola,Sudan,na Uganda,then usinge kuja na hoja ya kutofikirika kama hii.
kwa taarifa tuu ni kuwa wakati wa amani jeshi linatakiwa kufanya kazi ngumu kuliko hata wakati wa vita,kuna notion inasema bleed during peace and sweat during the war.kama unaona wanafaidi na wewe ni mtanzania na natumaini kuwa unasifa za kutosha basi nenda kajiunge ili na wewe ufaidi.
 
Back
Top Bottom