Tuliowahi okota embe dodo tukutane hapa

Tuliowahi okota embe dodo tukutane hapa

Mie nilikua sehemu na mshkaji wangu tunapiga stori mara txt ikaingia, ile kucheki naona nimetumiwa laki mbili, kujaribu kuiangalia ile namba siijui.
Mshkaji akanishawishi bhna akasemaitakua kuna mtu kakosea namba tu.
Basi tukaitoa haoooo tukaenda kuitumia( si unajua tena pesa ambayo hujaitarajia)
Nakumbuka siku hiyo tulitumia 150, kesho yake nipo kwa mama ntilie napiga supu simu ikaita kuchek boss wangu, akaniambia jana alinitumia hela kwa ajili ya kununulia materials na nauli ya kwenda site,.
Niliishiwa pozi nikamjibu tu niliipata boss
 
Mie nilikua sehemu na mshkaji wangu tunapiga stori mara txt ikaingia, ile kucheki naona nimetumiwa laki mbili, kujaribu kuiangalia ile namba siijui.
Mshkaji akanishawishi bhna akasemaitakua kuna mtu kakosea namba tu.
Basi tukaitoa haoooo tukaenda kuitumia( si unajua tena pesa ambayo hujaitarajia)
Nakumbuka siku hiyo tulitumia 150, kesho yake nipo kwa mama ntilie napiga supu simu ikaita kuchek boss wangu, akaniambia jana alinitumia hela kwa ajili ya kununulia materials na nauli ya kwenda site,.
Niliishiwa pozi nikamjibu tu niliipata boss
Hahaha
Pole sana boss
 
...kuna mtu alinpa pesa yke nkamlimpie ada bank nmb,ilikuwa ni laki na 80 hv zikiwepo elfu 5 nyingi.Nikafika bank nikajaza ile form ya kudeposit nkahesabu pesa nikaelekea counter,counter akapokea pesa akaingiza ktk ile machine yao ya kuhesabu pesa nkashangaa narudishiwa elfu 5 nilitaka kumwambia ahesabu vizuri nkasema nitakuwa kama namdharau kwamba hajui kutumia machine.
 
mwenzenu sijui nina gundu,yaani iliwahi tokea siku moja tu mtu kakosea katuma kwangu elfu 23,wakati nashangaa shangaa nastukia muamala umebatilishwa.

niko kazini na wafanyakazi wenzangu wanazidishiwa mara pesa kwenye acc zaomimi sijui nakosea wapi.
 
Ww ulikiwa na bahati je wakat unatoa lakin 4 ungezirudia kama mara 4 kutoa hiv ungekiwa mbali sana
Nilishawahi kuwekewa sh. Milioni nane kwenye account yangu ya bank ambayo salio langu halisi lilikuwa halizidi laki tano maana pesa yote niliimaalizia kwenye ujenzi. Nilikuja kugundua baada ya kutoa pesa kwenye ATM na kuangalia kiasi kilichobaki. Ile hela ilikaa kama miezi miwili hivi nilikuwa naogopa kuitoa maana bank wana full information kuhusu mimi kama according to process zao za kufungua account. Baadae nikaanza kuchukua kidogo kidogo mpaka nikatumia milioni tatu, siku hiyo nipo kazini sina hili wala lile napigiwa simu na ofisa wa ile bank kutoka makao makuu kuwa na kuambiwa kuwa kwenye account yako kuna hela sh. Milioni nane imeingia kimakosa na umeshatumia sh. Milioni tatu hivyo unatakiwa uirudishe. Nikawajibu nitakwenda kwenye branch yangu niliofungulia account ili wanifanyie reconciliation kabla ya kulipa hilo deni. Jumamosi moja nikaenda pale branch nikaonyeshwa full evidence, nilikuwa nataka kukwepa kulipa hivyo nilikuwa naangalia kweli wana ushahidi wa kutosha. Halafu nikawauliza tatizo hili ni kwangu tu au kuna wenzangu, nikajibiwa wapo wenzio mpo kama mia moja hivi. Nikataka kujua ilikuwaje mpaka tatizo likatokea, wakanijibu kuwa kuna tarehe wakaitaja kuanzia saa moja usiku mpaka saa moja na nusu system ya bank kwenye ATM machine ilijichanganya na kufanya kila anaetoa hela kwa muda huo inazidisha mara ishirini ya ile pesa aliotoa na inaweka kwenye account. Nikakumbuka kuwa ni kweli siku hiyo nilitoa kwenye ATM shilingi laki nne. Nikauliza mbona mmekaa zaidi ya miezi miwili ndio mnatutafuta, wakanijibu kuwa hata wao wenyewe walichelewa kugundua hilo tatizo. Nikawajibu hiyo pesa nimeshatumia nitawalipa kidogo kidogo, nikaambiwe niandike kwa mkono wangu kuwa nitalipa hiyo pesa kama ushahidi. Sijalipa mpaka leo ni mwaka wa tatu sasa na ile account nimeichilia mbali, mwanzoni walisumbua sana kwenye simu ila kwa sasa nadhani watakuwa wameshakata tamaa na kuniorodhesha kwenye bad debts.
 
Kuna wakati hadi unashukuru Mungu hata ulie machozi kwa jinsi ulivyo na bahati.

Wengine wamewahi okota fedha, wangine wachumba, wengine kazi.. etc.

Kuna mengine yanatokea kwa uzuri upande wako lakini sio mazuri kwa wengine.

Mfano huna pesa.. unampa mwuza duka buku ununue kitu cha buku ila ajabu anakurudishia elfu 9 akidhani umempa buku 10..

Mimi niliwahi rushiwa laki 5 na wakala wa mpesa hadi leo hawaja ulizia.. na unajua ukitumiwa fedha na wakala haina namba ya simu.. hivyo nipo nasubiri voda wanipigie leo ni mwaka wa 3.


Ebu twambie jambo gani ambalo ulijiona kama mtu mwenye bahati.View attachment 1131288
Niliokota pesa nyingi sana njiani, kila nikitembea naokota.

Dah, nikaamka kutoka usingizini kumbe ilikuwa ndoto.
 
Hilo dodo lilikuwa kama LA masanja mkandamizaji,
Kwani huchumwa nyakati za mchana tu
Niliwahi kuokota dodo mida ya jioni kabisa nikiwa nimeshakata tamaa kbs leo nalalaje na njaa baridi yote hii ya june Arusha. Kila alieniona nalo alilitamani nami nikalilinda lisiniponyoke.
Nilikuja kugundua sio dodo baada ya kufika geto maana tangu naanza kuchapa mzigo mpaka namaliza alikuwa anapokea simu kama yupo kitengo cha huduma kwa wateja vodacom, hamu iliisha na sikurudia tena.
 
Niliwai tumiwa laki 3 halafu nilikuwa sina hela nikaona si huu ungwana nikapigiwa simu nikarudisha yote baadae nikaona laki 2 kwenye simu hapo nikasema uhaminifu ni muhimu zaidi katika maisha
Vyema saana
 
Mi binafsi mara kadhaa tangu kwetu kijijini wenye maduka wamekuwa wakinirudishia chenji zaidi,nilipokuwa mdogo nilidhani wananitega,ila hata nilipohama ktk harakati za maisha hilo jambo likaendelea,hadi makondakta wa daladala vilevile wananizidishia mara kadhaa.

Nashukuru Mungu sijawahi ondoka na chenji ya mtu
 
Nilishawahi kuwekewa sh. Milioni nane kwenye account yangu ya bank ambayo salio langu halisi lilikuwa halizidi laki tano maana pesa yote niliimaalizia kwenye ujenzi. Nilikuja kugundua baada ya kutoa pesa kwenye ATM na kuangalia kiasi kilichobaki. Ile hela ilikaa kama miezi miwili hivi nilikuwa naogopa kuitoa maana bank wana full information kuhusu mimi kama according to process zao za kufungua account. Baadae nikaanza kuchukua kidogo kidogo mpaka nikatumia milioni tatu, siku hiyo nipo kazini sina hili wala lile napigiwa simu na ofisa wa ile bank kutoka makao makuu kuwa na kuambiwa kuwa kwenye account yako kuna hela sh. Milioni nane imeingia kimakosa na umeshatumia sh. Milioni tatu hivyo unatakiwa uirudishe. Nikawajibu nitakwenda kwenye branch yangu niliofungulia account ili wanifanyie reconciliation kabla ya kulipa hilo deni. Jumamosi moja nikaenda pale branch nikaonyeshwa full evidence, nilikuwa nataka kukwepa kulipa hivyo nilikuwa naangalia kweli wana ushahidi wa kutosha. Halafu nikawauliza tatizo hili ni kwangu tu au kuna wenzangu, nikajibiwa wapo wenzio mpo kama mia moja hivi. Nikataka kujua ilikuwaje mpaka tatizo likatokea, wakanijibu kuwa kuna tarehe wakaitaja kuanzia saa moja usiku mpaka saa moja na nusu system ya bank kwenye ATM machine ilijichanganya na kufanya kila anaetoa hela kwa muda huo inazidisha mara ishirini ya ile pesa aliotoa na inaweka kwenye account. Nikakumbuka kuwa ni kweli siku hiyo nilitoa kwenye ATM shilingi laki nne. Nikauliza mbona mmekaa zaidi ya miezi miwili ndio mnatutafuta, wakanijibu kuwa hata wao wenyewe walichelewa kugundua hilo tatizo. Nikawajibu hiyo pesa nimeshatumia nitawalipa kidogo kidogo, nikaambiwe niandike kwa mkono wangu kuwa nitalipa hiyo pesa kama ushahidi. Sijalipa mpaka leo ni mwaka wa tatu sasa na ile account nimeichilia mbali, mwanzoni walisumbua sana kwenye simu ila kwa sasa nadhani watakuwa wameshakata tamaa na kuniorodhesha kwenye bad debts.
Wale wapigaji ni mbinu yao hiyo asante kwa kuwapiga nawe pia
 
Mara mbili, kwanza niliiwekea pesa 200,000 kwenye mashine ya selcom, pesa ikaingia kwenye mashine na bado kwenye airtel money ikabaki na nikaitoa.
Pili jiran yangu dukan alikuja kutoa mpesa 100,000 kabla ya kuchukua pesa akaitwa dukan kwake akaenda nikijua atarudia pesa yake ajabu hakurudi na hata siku zingine alipokuja dukan alikuja kwa mishe zingine tu.
Unamuibia mpaka jirani yako? Duh
 
Dodo langu halikuleta manufaa kutokana na kua mgeni wa pesa.Nilipoajiriwa tu nimekua mishahara ya miezi kama sita ya watu wawili na wangu wa tatu mfululizo bila kufanyia lolote la msingi.Ila nilikuja lima kwa meno
 
Ww ulikiwa na bahati je wakat unatoa lakin 4 ungezirudia kama mara 4 kutoa hiv ungekiwa mbali sana
Sikuweza kujua siku ile nilikuja kugundua kuwa salio limeongezeka siku nyingine na hata kama ningejua kwa siku ile nisingejua kwanini imeongezeka!
 
Hua na mchezo wa kuhamishia pesa kwenye akaunti za watu kutoka zile zilizonona kwenda kwenye akaunti zingine kisha baadae mpunga huu upiga wao ,
Hapo nimekuelewa sasa, ila kwangu mimi ilikuwa ni tatizo la system maana hela ilikaa kwenye account yangu kwa zaidi ya miezi miwili ndio nikaanza kuichukua kidogokidogo. Na nilikuwa sipo peke yangu tulikuwa na wateja wenzangu kama mia hivi wote walipitiwa na hili zali. Kuna wengine ambao sio waoga walichukua pesa yote na kuingiza kwenye biashara na bank wakakubali kulipwa deni kidogokidogo tena bila riba maana sio kosa la mteja ni la kwao.
 
Back
Top Bottom