Tuliopanga Uswahilini tuna vituko na maswahibu mengi, tuambiane hapa

Ndugu wadau,

Najua humu JF tupo wengi sana tuliopanga katika hizi nyumba zilizopo Uswahilini, mtasema wenyewe kama upo Uswazi. Basi narudi madani na nitaanza ni hichi kitabia kinachonikera sana mpaka roho inapasukaga ila haifi.

Umeme katika nyumba hizi hua ni ugomvi usioisha, yaani unakuta kama kuna wapangaji zaidi ya wawili panatokea choko za watu kutaka kuhesabiana vyombo vya umeme na wanakupimia matumizi kupitia midomo ooh Mara we una Friji oooh unavaa nguo smart unatumia Pasi ooh Mara juisi kila siku sana anatumalizia umeme.
Na Mara zoote Umeme ukikatika unalaumiwa mwenye kauchumi oooh bila flani huu umeme tungemaliza mwezi.

Naamua kuishia hapa ili na waswazi wenzangu waulize, waseme vijitabia hovyo tujirekebishe au tushauriane ila kaswali; "kama unaona nina vyombo vingi vya umeme nani kakuzuia usiwe navyo wewe pia?".
Nmepanga pango la biashara,wapangaji wenzangu ni waislam,wakristo nikiwepo mm na walokole.
Changamoto kubwa tuliyonayo ni katika ulipaji wa hela ya umeme na mlinzi,mara nyng wanaotukwamisha ni hawa walokole yaan ukiwapa taarifa kuhusu ulipaji wa umeme wanakuwa wakali vbaya na wanaingia ndani wanafunga milango wanaanza kusali na kulia.Huwa najiuliza kanisani huwa wanafundishwa nn?hawajui kumkwaza mtu ni dhambi?kwann mlinzi ahatarishe maisha yake kwa kulinda mali zako kisha usimpe pesa yake?kwann wenzako watoe pesa ya umeme ww usitoe?taabu kweli
 
Ingine watoto wakigombana kesho yake wakubwa tumenuniana pia kuna mashindano ya vyakula mi ndio maana naendaga kuokota maganda ya mayai kwa mchoma chips ili niwaumize wakati wa kufagia twende sawa maana unaweza onekana mnyonge kwenye compound nzima
 
Kati ya mambo yanayofurahisha uswahilini hasa kwenye nyumba za kupanga ni tabia ya kuazimana hata visivyoazimwa..
1. Mtu anasonga ugali huko kwake anakuja kwako na bakuli umuazime mboga!
2. Mtu ana TV ila deki hana, anaenda kuazima muvi kisha anakuja kuazima deki. Na akichukua harudishi hadi uifate
3. Ukiwa na friji utahifadhi nyama, maziwa, samaki, wa nyumba nzima
4. Jirani akipata wageni, wengine anakuja kuwaombea walale kwako..
5. Ratiba ya usafi
Hiii noma kwakwwli
 
Hamia nyumba zenye kila chumba na metre yake kuepuka usumbufu coz huo umeme wa kushare ni majanga aise
 
Muziki wa kisingeli ni kero
Vilabu vya pombe, komoni na banana
Matusi muda wowote, kwa makuzi ya watoto ni hatari
Mama Amina, hapo ni kero za mitaa ya uswazi bado nyumba zetu sasa
Kufuatiliana watu wanajua unakula nini wewe nunua mihogo yako ficha na magazeti mifuko hata kwenye salfet watu watajua kama umekula mihogo mitatu
Foleni ya kwenda chooni asubuhi ni kero
Karo la kuoshea vyombo kuwa karibu na mlango wa choo au bafu,
Nyumba nyingi maji ni shida, na yakitoka ni ya chumvi ( dar ) na ngumi lazma zitatokea tuu
Ukivusha ka demu mke wa jirani akaona anaona wivuuuu utatangaziwa malaya, utategwa tegwa na ukimbandua tu kosa mama mwenye nyumba naye atataka au mtoto wake
Usijerogwa ikatokea siku ukajamba kwa nguvu ukiwa toilet huku nje wawepo mabinti wa kiswazi, utajuta kwa vicheko
Umemtegea Kama walivyosema wachangiaji waliopita
 
Halafu cha kushangaza ukienda kuishi sehemu ambayo imetulia maeneo kama Kigamboni Mji Mwema, Mbeya Forest, Gangilonga, Mbweni, Bahari Beach kule ambapo kumetulia unajikuta unapamiss uswazi vibaya mno (sijui peke yangu?)
Ulipo itaja gangilonga umenikumbusha mbali sana mitaa Fulani ya iringa
 
Uswazi...
ae32f366c7fa8b0a6f44c2340e8f2818.jpg



Cc: mahondaw
 
1.Utapeli wa wenyeviti wa serikali za mitaa na mabalozi kwenye michango ya ulinzi wa sungususungu na uzoaji wa taka.Wanachangisha pesa lakini huduma inayotolewa ni sawa na hakuna.
2.Kwa jirani kukiwa na shughuli ya kigodoro au kuchezwa mwari usiombe.Maana muziki hufunguliwa kwa sauti ya juu siku hiyo kulala no na vibaka wote wa mtaani na maeneo ya jirani huhamia hapo.
3.Kero nyingine pale mpangaji mwenzio anapoamka alfajiri na kuanza kujiandaa kwenda kuswali au kibaruani
huku akiongea kwa Sauti ya juu akiacha maagizo kwa familia yake pasipo kujali kama kuna watu wengine bado wamelala muda huo.
 
Kati ya mambo yanayofurahisha uswahilini hasa kwenye nyumba za kupanga ni tabia ya kuazimana hata visivyoazimwa..
1. Mtu anasonga ugali huko kwake anakuja kwako na bakuli umuazime mboga!
2. Mtu ana TV ila deki hana, anaenda kuazima muvi kisha anakuja kuazima deki. Na akichukua harudishi hadi uifate
3. Ukiwa na friji utahifadhi nyama, maziwa, samaki, wa nyumba nzima
4. Jirani akipata wageni, wengine anakuja kuwaombea walale kwako..
5. Ratiba ya usafi
Wengine poti la mavi ya mtoto wake anakuja kukuwekea mlangoni pako
 
Back
Top Bottom