Tulimpenda lakini Mungu kampenda zaidi

Enkulu

Member
Sep 29, 2022
17
57
"Tulikupenda/Tulimpenda lakini Mungu kakupenda/kampenda zaidi" hii kauli, au sentensi au msemo umekuwa ukisikika sana katika misiba ya Wakristo. Sina hakika kwa upande wa Waislam ila kama pia hutumika mimi sijui.

Imekuwa ni sentensi ya kawaida sana kutamkwa misibani. Lakini sentensi hii fupi imenifikirisha na imenifanya kuibua maswali mengi kichwani mwangu.

Msiba si jambo jema, hasa kwa wanadamu. Hakuna mtu anaependa kufa, japo tunataka kwenda mbinguni lakini kufa au kumuona yule ampendae akifa; Hapana kwakweli.

Msiba huleta huzuni, majonzi, vilio, migogoro, uadui, na mambo mengine mengi. Sasa iweje upendo wa Mungu udhiirike pale mtu akifa? Mpaka ifikie hatua tuseme "...Mungu alikupenda zaidi".

Yaani Mungu akikupenda ndo unakufa?

Swali hili lilinifanya nijiulize kwanini tunakufa? Kama kifo sio kitu kizuri kwanini basi tunakufa?

Katika biblia kifo kilitajwa kwa mara ya kwanza katika kitabu cha Mwanzo 2:17. Adam na Hawa wanapewa maagizo ya kutokula matunda ya mti wa katikati la sivyo watakufa.

Adam na Hawa wakafanya kinyume, na kile kilichonenwa kikawa, Abeli akawa binadamu wa kwanza Kufa. Kumbe kifo ni matokeo yaliyokuja baada kwenda kinyume na maagizo ya Mungu.

Je kifo ni adhabu?

Kwa namna moja au nyengine twaweza kusema kifo ni adhabu. Adhabu ambayo Adam na Hawa waliileta kwa wanadamu wote baada ya kwenda kinyume na matakwa ya Muumba. Sasa kama kifo ni adhabu, iweje upendo wa Mungu udhiirike kwa mtu anapokufa? Ukiadibiwa ndo unapendwa?

"Tulimpenda lakini Mungu kampenda ziadi"

Kifo si adhabu, kifo ni ishara ya kuwa Mungu anatupenda bado, kifo ni pendo la Mungu. Mwanzo 3:22 "Bwana Mungu akasema, Basi, huyu mtu amekuwa kama mmoja wetu, kwa kujua mema na mabaya; na sasa asije akanyosha mkono wake akatwaa matunda ya mti wa uzima, akala, akaishi milele;"

Kumbe katika bustani ya Eden palikuwako na mti wa uzima, mti ambao ukila matunda yake unaishi milele. Na endapo Adam na Hawa wangekula matunda ya mti huu wangeishi milele.

Je Mungu hakutaka Adam na Hawa waishi milele hata akawafukuza? Jibu ni "HAPANA" Mungu alitaka Adam na Hawa waishi milele ndio maana hapakuwepo na kifo kabla ya wao kwenda kinyume nae. Sasa kwanini hakutaka wale tunda la mti wa uzima?

Kitendo cha Adam na Hawa kula tunda la mti wa katikati kilitia doa roho zao, wakawa wadhambi tayari. Mungu alitaka binadamu hawa waishi milele, lakini waishi milele wakiwa si wadhambi. Waishi milele roho zao zikiwa swafi kama theluji.

Mungu hapatani dhambi, sasa ili binadamu akombolewe na aje kuishi maisha yale aliyotakiwa kuishi ni lazima afe

Kumbe kifo ni utakaso? Kifo ni ukombozi? Soma Yohana 3:16 "Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele."

Tunaona Mungu anamtoa mwanae (Yesu Kristo) aje kufa msalabani, kwanini anafanya hivyo? Kwasababu Mungu aliupenda ulimwengu na yoyote atakae mwamini huyo mwanae atakuwa na uzima wa milele.

Uzima wa milele umeletwa na kifo cha Yesu Kristo, kifo chake ni juu ya upendo wa Mungu kwa wanadamu. Kama Mungu asingependa huu ulimwengu Yesu Kristo asingekufa.

Kumbe kifo ni upendo. Basi tuko sahihi tukisema "Tulimpenda lakini Mungu kampenda zaidi"

Upendo ni nini?

Biblia inasema Mungu ni pendo, 1 Yohana 4:8 "Yeye asiyependa hakumjua Mungu kwa maana Mungu ni pendo"

Upendo ni kitendo cha kuonyesha hisia pengine umeridhishwa na mtu huyo, au umemkubali, au umemuhurumia, au unataka kumkaribia uwe karibu naye n.k

Mungu ameridhika nasi, ametukubali kama wanae (soma "Wagalatia 3:26") ,ametuhurumia na anataka kumkaribia tuwe karibu nae. Ili haya yote haya yatimie ni lazima tufe.

Binadamu hawezi kumkaribia Mungu kama hatokufa. Zamani Adam aliweza kuonana na Mungu ana kwa ana, unajua kwanini? Kwasababu roho yake ilikuwa nyeupe pasipo na dhambi. Leo hii Mungu huwasiliana na binadamu kwa namna ya tofauti (maombi).

Basi mtu anapokufa tusihuzunike sana bali tuwe na matumaini, tuamini kwamba hilo limemtokea yeye nasi pia litatutokea na yote ni kwasababu Mungu alitupenda anatupenda na ataendelea kutupenda.

Mungu katumia kifo kumkomboa binadamu, binadamu aliowapenda. Basi tusikiogope kifo bali tujiandae ili tutakapo kufa tuwe na matumaini ya kufufuliwa na kuishi Mbinguni.

Yatupasa kujiandaa wakati wote, kila mtu kwa imani yake. Kifo huja wakati wowote, siku yoyote, hakuna anayejua atakufa lini.
 
Kufa ni Sakramenti,
Kuzaliwa ni Sakramenti,
Kufufuka ni Sakramenti (wale Watakatifu )
Kuzikwa ni Sakramenti.

Bwana Yesu mwenyewe Alikufa, ila Mungu alimfufua

Tunatiana moyo kwa maneno mazuri hii ni kawaida, but we should die.

Sijui nimejibu,
 
Kufa ni Sakramenti,
Kuzaliwa ni Sakramenti,
Kufufuka ni Sakramenti (wale Watakatifu )
Kuzikwa ni Sakramenti.

Bwana Yesu mwenyewe Alikufa, ila Mungu alimfufua

Tunatiana moyo kwa maneno mazuri hii ni kawaida, but we should die.

Sijui nimejibu,
Kabisa, umejibu na upo sawa 100%
 
Kifo nirafiki nzuri na jirani nzuri tuponae kila siku tunakulanae tunaishi nae anatujua tunamjua tunapaswa kuzoeana nae tusimchukie

tumjue tabiazake na dalili za ujio wake kusudi siku anapo kuja tumjue na tujiandae

ili siku anapokuja kutuchukua tufurahie kuja kuchukuliwa na rafiki yetu wa yangu utoto Kifo

Kifo hakitishi tuna jitisha sisi
 
"Tulikupenda/Tulimpenda lakini Mungu kakupenda/kampenda zaidi" hii kauli, au sentensi au msemo umekuwa ukisikika sana katika misiba ya Wakristo. Sina hakika kwa upande wa Waislam ila kama pia hutumika mimi sijui.

Imekuwa ni sentensi ya kawaida sana kutamkwa misibani. Lakini sentensi hii fupi imenifikirisha na imenifanya kuibua maswali mengi kichwani mwangu.

Msiba si jambo jema, hasa kwa wanadamu. Hakuna mtu anaependa kufa, japo tunataka kwenda mbinguni lakini kufa au kumuona yule ampendae akifa; Hapana kwakweli.

Msiba huleta huzuni, majonzi, vilio, migogoro, uadui, na mambo mengine mengi. Sasa iweje upendo wa Mungu udhiirike pale mtu akifa? Mpaka ifikie hatua tuseme "...Mungu alikupenda zaidi".

Yaani Mungu akikupenda ndo unakufa?

Swali hili lilinifanya nijiulize kwanini tunakufa? Kama kifo sio kitu kizuri kwanini basi tunakufa?

Katika biblia kifo kilitajwa kwa mara ya kwanza katika kitabu cha Mwanzo 2:17. Adam na Hawa wanapewa maagizo ya kutokula matunda ya mti wa katikati la sivyo watakufa.

Adam na Hawa wakafanya kinyume, na kile kilichonenwa kikawa, Abeli akawa binadamu wa kwanza Kufa. Kumbe kifo ni matokeo yaliyokuja baada kwenda kinyume na maagizo ya Mungu.

Je kifo ni adhabu?

Kwa namna moja au nyengine twaweza kusema kifo ni adhabu. Adhabu ambayo Adam na Hawa waliileta kwa wanadamu wote baada ya kwenda kinyume na matakwa ya Muumba. Sasa kama kifo ni adhabu, iweje upendo wa Mungu udhiirike kwa mtu anapokufa? Ukiadibiwa ndo unapendwa?

"Tulimpenda lakini Mungu kampenda ziadi"

Kifo si adhabu, kifo ni ishara ya kuwa Mungu anatupenda bado, kifo ni pendo la Mungu. Mwanzo 3:22 "Bwana Mungu akasema, Basi, huyu mtu amekuwa kama mmoja wetu, kwa kujua mema na mabaya; na sasa asije akanyosha mkono wake akatwaa matunda ya mti wa uzima, akala, akaishi milele;"

Kumbe katika bustani ya Eden palikuwako na mti wa uzima, mti ambao ukila matunda yake unaishi milele. Na endapo Adam na Hawa wangekula matunda ya mti huu wangeishi milele.

Je Mungu hakutaka Adam na Hawa waishi milele hata akawafukuza? Jibu ni "HAPANA" Mungu alitaka Adam na Hawa waishi milele ndio maana hapakuwepo na kifo kabla ya wao kwenda kinyume nae. Sasa kwanini hakutaka wale tunda la mti wa uzima?

Kitendo cha Adam na Hawa kula tunda la mti wa katikati kilitia doa roho zao, wakawa wadhambi tayari. Mungu alitaka binadamu hawa waishi milele, lakini waishi milele wakiwa si wadhambi. Waishi milele roho zao zikiwa swafi kama theluji.

Mungu hapatani dhambi, sasa ili binadamu akombolewe na aje kuishi maisha yale aliyotakiwa kuishi ni lazima afe

Kumbe kifo ni utakaso? Kifo ni ukombozi? Soma Yohana 3:16 "Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele."

Tunaona Mungu anamtoa mwanae (Yesu Kristo) aje kufa msalabani, kwanini anafanya hivyo? Kwasababu Mungu aliupenda ulimwengu na yoyote atakae mwamini huyo mwanae atakuwa na uzima wa milele.

Uzima wa milele umeletwa na kifo cha Yesu Kristo, kifo chake ni juu ya upendo wa Mungu kwa wanadamu. Kama Mungu asingependa huu ulimwengu Yesu Kristo asingekufa.

Kumbe kifo ni upendo. Basi tuko sahihi tukisema "Tulimpenda lakini Mungu kampenda zaidi"

Upendo ni nini?

Biblia inasema Mungu ni pendo, 1 Yohana 4:8 "Yeye asiyependa hakumjua Mungu kwa maana Mungu ni pendo"

Upendo ni kitendo cha kuonyesha hisia pengine umeridhishwa na mtu huyo, au umemkubali, au umemuhurumia, au unataka kumkaribia uwe karibu naye n.k

Mungu ameridhika nasi, ametukubali kama wanae (soma "Wagalatia 3:26") ,ametuhurumia na anataka kumkaribia tuwe karibu nae. Ili haya yote haya yatimie ni lazima tufe.

Binadamu hawezi kumkaribia Mungu kama hatokufa. Zamani Adam aliweza kuonana na Mungu ana kwa ana, unajua kwanini? Kwasababu roho yake ilikuwa nyeupe pasipo na dhambi. Leo hii Mungu huwasiliana na binadamu kwa namna ya tofauti (maombi).

Basi mtu anapokufa tusihuzunike sana bali tuwe na matumaini, tuamini kwamba hilo limemtokea yeye nasi pia litatutokea na yote ni kwasababu Mungu alitupenda anatupenda na ataendelea kutupenda.

Mungu katumia kifo kumkomboa binadamu, binadamu aliowapenda. Basi tusikiogope kifo bali tujiandae ili tutakapo kufa tuwe na matumaini ya kufufuliwa na kuishi Mbinguni.

Yatupasa kujiandaa wakati wote, kila mtu kwa imani yake. Kifo huja wakati wowote, siku yoyote, hakuna anayejua atakufa lini.
Huyo Mungu hayupo.

Mungu ni dhana fulani inayotumika kama chaka la kusukumia mambo tusiyoyaelewa, na kujifariji.

Watu wanataka kujifanya wana majibu ya maswali ambayo hawana majibu yake. Wanapenda kujiona wana control kupitia kujua nini kinatokea baada ya kifo. Wanajipa majibu kwamba wanajua nini kinatokea baada ya kifo, hata kama hawajui.

Kuna saikolojia kubwa ya "coping mechanism" katika dhana ya kuwapo Mungu. Saikolojia hii imetusaidia kuwa na matumaini na kuweza kufika hapa. Ukimsoma Yuval Noah Harari katika "Sapiens: A Brief History of Humankind" kaandika sana haya mambo.

Watu tunataka kuishi kwa matumaini kwamba wapendwa wetu waliofariki tutakutana nao siku moja mbinguni.

Lakini, ukweli ni kwamba hakuna mtu anayeweza kuthibitisha Mungu yupo, hakuna anayeweza kuthibitisha mbinguni kupo, na hakuna anayeweza kuthibitisha watu wanaendelea kuishi baada ya kufa.

Kwa sababu, Mungu hayupo, mbinguni hakupo, na hakuna maisha wanayoishi watu baada ya kifo. Kifo ndiyo mwisho wa maisha kwa watu.

Kama unabisha, thibitisha Mungu yupo, thibitisha mbinguni kupo, na thibitisha kwamba kuna maishabya watu baada ya kifo.
 
Huyo Mungu hayupo.

Mungu ni dhana fulani inayotumika kama chaka la kusukumia mambo tusiyoyaelewa, na kujifariji.

Watu wanataka kujifanya wana majibu ya maswali ambayo hawana majibu yake. Wanapenda kujiona wana control kupitia kujua nini kinatokea baada ya kifo. Wanajipa majibu kwamba wanajua nini kinatokea baada ya kifo, hata kama hawajui.

Kuna saikolojia kubwa ya "coping mechanism" katika dhana ya kuwapo Mungu. Saikolojia hii imetusaidia kuwa na matumaini na kuweza kufika hapa. Ukimsoma Yuval Noah Harari katika "Sapiens: A Brief History of Humankind" kaandika sana haya mambo.

Watu tunataka kuishi kwa matumaini kwamba wapendwa wetu waliofariki tutakutana nao siku moja mbinguni.

Lakini, ukweli ni kwamba hakuna mtu anayeweza kuthibitisha Mungu yupo, hakuna anayeweza kuthibitisha mbinguni kupo, na hakuna anayeweza kuthibitisha watu wanaendelea kuishi baada ya kufa.

Kwa sababu, Mungu hayupo, mbinguni hakupo, na hakuna maisha wanayoishi watu baada ya kifo. Kifo ndiyo mwisho wa maisha kwa watu.

Kama unabisha, thibitisha Mungu yupo, thibitisha mbinguni kupo, na thibitisha kwamba kuna maishabya watu baada ya kifo.
Sitaki kupingana ma wewe moja kwa moja kwasababu ndicho ulichochagua kuamini. Binafsi naamini Mungu yupo na vya kuthibitisha kuwa Mungu yupo vipo vingi, vithibitisho cya kiimani, kisayansi, kiroho na kila kitu.

Leo hii tunaona ndege zinaruka, magari yanatembea, pikipiki, meli na vyote vilivyotengenezwa na binadamu (man made). Hivi vyote havijatokea tu from nowhere, kuna mtu ali'invent na vikawa. Vyengine vilianza na wazo akatengeneza mtu mwengine, vyengine mtoa wazo ndo huyo huyo alitengeneza maboresho yakafanywa na mwengine.

Concept yangu hapo juu ni hii; hakuna kitu chochote hapa duniani kilichotokea tu kutoka kusikojulikana, lazima vina first source tena being yenye nguvu ya ajabu. Huyo first source ndo Mungu.

Ukisoma creations theories zipo nyingi sana lakini vyote vinakosa majibu ya kuthibitika kuonesha mwanzo wa yote hayo. Big bang theory inasema kulikuwako na mlipo, hicho kilicholipuka kilitokea wapi? Charles Darwin anasema tuli'evolve kutoka primates mpaka homo sapiens sapiens. Hao primates walitokea wapi?

Atheist wengi niliowasoma na kukutana nao wengi hawana vithibitisho vya hoja zao. Watakwambia nithibitishie Mungu yupo? Lakini Muulize yeye akuthibitishie kuwa Mungu hayupo..

Ili uthibitishe kuwa Kitu fulani hakipo ni lazima umekitafuta na umekikosa sindio? Wewe jamaa Mungu ulimtafutia wapi ukamkosa?

Waulize wachawi, waulize Mungu yupo au hayupo, waulize watakwambia. Hata kabla ya kuja wakoloni Africa tulikuwa na hii dhana ya Mungu na watu waliabudu kile waluchokiamini.

Hata uende kwa Hadzabe au kabila zozote huko ambazo hazina ushirikiano na jamii za sasa lazima utakuta concept ya Mungu ipo.

Huwezi Mungu hayupo alafu ukawa na akili timamu. Lazima uwe na shida kidogo kichwani. Unaweza usiamini Mungu anayeabudiwa na Wakristo, Waislamu, Wahindu, Wabudha lakini lazima uamini Mungu yupo.

NITHIBITISHIE KUWA MUNGU HAYUPO
 
Sitaki kupingana ma wewe moja kwa moja kwasababu ndicho ulichochagua kuamini. Binafsi naamini Mungu yupo na vya kuthibitisha kuwa Mungu yupo vipo vingi, vithibitisho cya kiimani, kisayansi, kiroho na kila kitu.

Leo hii tunaona ndege zinaruka, magari yanatembea, pikipiki, meli na vyote vilivyotengenezwa na binadamu (man made). Hivi vyote havijatokea tu from nowhere, kuna mtu ali'invent na vikawa. Vyengine vilianza na wazo akatengeneza mtu mwengine, vyengine mtoa wazo ndo huyo huyo alitengeneza maboresho yakafanywa na mwengine.

Concept yangu hapo juu ni hii; hakuna kitu chochote hapa duniani kilichotokea tu kutoka kusikojulikana, lazima vina first source tena being yenye nguvu ya ajabu. Huyo first source ndo Mungu.

Ukisoma creations theories zipo nyingi sana lakini vyote vinakosa majibu ya kuthibitika kuonesha mwanzo wa yote hayo. Big bang theory inasema kulikuwako na mlipo, hicho kilicholipuka kilitokea wapi? Charles Darwin anasema tuli'evolve kutoka primates mpaka homo sapiens sapiens. Hao primates walitokea wapi?

Atheist wengi niliowasoma na kukutana nao wengi hawana vithibitisho vya hoja zao. Watakwambia nithibitishie Mungu yupo? Lakini Muulize yeye akuthibitishie kuwa Mungu hayupo..

Ili uthibitishe kuwa Kitu fulani hakipo ni lazima umekitafuta na umekikosa sindio? Wewe jamaa Mungu ulimtafutia wapi ukamkosa?

Waulize wachawi, waulize Mungu yupo au hayupo, waulize watakwambia. Hata kabla ya kuja wakoloni Africa tulikuwa na hii dhana ya Mungu na watu waliabudu kile waluchokiamini.

Hata uende kwa Hadzabe au kabila zozote huko ambazo hazina ushirikiano na jamii za sasa lazima utakuta concept ya Mungu ipo.

Huwezi Mungu hayupo alafu ukawa na akili timamu. Lazima uwe na shida kidogo kichwani. Unaweza usiamini Mungu anayeabudiwa na Wakristo, Waislamu, Wahindu, Wabudha lakini lazima uamini Mungu yupo.

NITHIBITISHIE KUWA MUNGU HAYUPO

Kwanza siongelei imani naongelea falsafa na mantiki. Imani haina uzito kwangu, kwa sababu unaruhusiwa kuamini chochote, cha uongo au ukweli. Mimi najadili kipi ni cha ukweli.

Ukweli kwamba kila kitu kina mwanzo hauthibitishi Mungu ndiye mwanzo.

Kama vile ukweli kwamba kila mtu ana baba usivyothibitisha kwamba baba yako ni Donald Trump.

Ukisema baba yako ni Donald Trump, inabidi uthibitishe kwa kutuonesha kuwa baba yako ni Donald Trump. Tuoneshe angalau DNA evidence.

Sasa wewe muafrika mweusi tii, Donald Trump mzungu. Unasema Donald Trump ni baba yako wa kibaiolojia. Tunakwambia tupe uthibitisho, unasema kila mtu ni lazima awe na baba, hivyo wewe lazima baba yako ni Donald Trump.

Huoni tatizo na hiyo hoja?

Huelewi kwamba ukweli kwamba kila mtu ni lazima awe na baba hauthibitishi Donald Trump ni baba yako mzazi?

Huoni kwamba ukweli kwamba kila kitu ni lazima kiwe na chanzo hauthibitishi chanzo ni Mungu?

Pia hiyo habari yako ya "first source" inaonesha tu kuwa hujui Physics. Katika Physics "first source" si kitu cha lazima.

Kwenye Quantum Physics kitu A kinaweza kusababisha kitu B, na hapo hapo hicho kitu B kikawa ndiyo kinachosababisha kitu A, katika "quantum loop" ambayo haina first cause.

Soma zaidi hapa.


So habari nzima ya "first cause" imepitwa na wakati.

Uthibitisho kwamba Mungu hayupo.

1.Mungu, mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote, kwa sifa zake hizo, si mchoyo na ni mwenye kugawa mazuri, si mwenye kugawa mabaya.

2. Mungu huyo, kwa sifa zake hizo, aliweza kuumba ulimwengu wowote, hata ulimwengu ambao hauruhusu mabaya, hauna magonjwa, hauna njaa, kifo etc. Angeumba hivyo asingepungukiwa na kitu, na in fact ulimwengu huo uko logically consistent na sifa zake. Hau contradict sifa zake.

3. In fact, Mungu huyo, kwa sifa zake, hawezi kuwapo sambamba na ulimwengu unaoruhusu mabaya.

Ama ulimwengu unaoruhusu mabaya upo na Mungu huyo hayupo, au Mungu huyo yupo na ulimwengu unaoruhusu mabaya haupo. Vyote viwili haviwezi kuwapo sambamba.

4. Tunaona ulimwengu unaoruhusu mabaya upo.

5. Hivyo, kwa kuwa ulimwengu unaoruhusu mabaya kuwepo maana yake ni kwamba Mungu huyo hayupo, Mungu huyo hayupo.

Yani ni hivi, Mungu huyo angekuwepo, hata huu mjadala wa kuhoji kama Mungu yupo au hayupo usingewezekana kufanyika.

Kila mtu angekuwa ana uelewa usio na utata wowote kwamba Mungu huyo yupo kwa namna ambayo mjadala huu usingewezekana kufanyika.

Kwa sababu, Mungu huyo mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote, kwa sifa zake, si mchoyo, angetupa sote elimu ya kumjua vizuri, bila kuhitaji msahafu wala tafsiri, kuanzia sekunde tunayozaliwa.

Mungu huyo kutunyima elimu isiyo utata kuhusu uwepo wake, mpaka watu wakauana katika vita vya kidini kwa sababu wanabishana kuhusu Mungu yukoje, wengine wanasema hayupo, wengine wanasema yupo, hata wanaosema yupo wana dini tofauti, hata dini moja ina madhehebu tofauti, hata katika dhehebu moja watu wanatofautiana, kuwepo kwa tofauti hizi kunainesha Mungu huyo hayupo.

Angekuwepo, kwa sifa zake hizo, Mungu huyo si mkatili hivyo aachie watu wauane mamilioni kwa mamilioni kwenye Crusades na vita nyingine za kidini kupigana kwa sababu ya utata wa Mungu yupo vipi.

Kwa maneno mengine, hata huu mjadala wa kuhojiana kuhusu uwepo wa Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na uoendo wote ni ushahidi kwamba Mungu huyo hayupo.

Angekuwepo isingewezekana kuwapo na mjadala wa kuhoji uwepi wake, kika mtu angejua Mungu yupi kwa namna ambayo ingeindia utata wiwote.
 
Sitaki kupingana ma wewe moja kwa moja kwasababu ndicho ulichochagua kuamini. Binafsi naamini Mungu yupo na vya kuthibitisha kuwa Mungu yupo vipo vingi, vithibitisho cya kiimani, kisayansi, kiroho na kila kitu.

Leo hii tunaona ndege zinaruka, magari yanatembea, pikipiki, meli na vyote vilivyotengenezwa na binadamu (man made). Hivi vyote havijatokea tu from nowhere, kuna mtu ali'invent na vikawa. Vyengine vilianza na wazo akatengeneza mtu mwengine, vyengine mtoa wazo ndo huyo huyo alitengeneza maboresho yakafanywa na mwengine.

Concept yangu hapo juu ni hii; hakuna kitu chochote hapa duniani kilichotokea tu kutoka kusikojulikana, lazima vina first source tena being yenye nguvu ya ajabu. Huyo first source ndo Mungu.

Ukisoma creations theories zipo nyingi sana lakini vyote vinakosa majibu ya kuthibitika kuonesha mwanzo wa yote hayo. Big bang theory inasema kulikuwako na mlipo, hicho kilicholipuka kilitokea wapi? Charles Darwin anasema tuli'evolve kutoka primates mpaka homo sapiens sapiens. Hao primates walitokea wapi?

Atheist wengi niliowasoma na kukutana nao wengi hawana vithibitisho vya hoja zao. Watakwambia nithibitishie Mungu yupo? Lakini Muulize yeye akuthibitishie kuwa Mungu hayupo..

Ili uthibitishe kuwa Kitu fulani hakipo ni lazima umekitafuta na umekikosa sindio? Wewe jamaa Mungu ulimtafutia wapi ukamkosa?

Waulize wachawi, waulize Mungu yupo au hayupo, waulize watakwambia. Hata kabla ya kuja wakoloni Africa tulikuwa na hii dhana ya Mungu na watu waliabudu kile waluchokiamini.

Hata uende kwa Hadzabe au kabila zozote huko ambazo hazina ushirikiano na jamii za sasa lazima utakuta concept ya Mungu ipo.

Huwezi Mungu hayupo alafu ukawa na akili timamu. Lazima uwe na shida kidogo kichwani. Unaweza usiamini Mungu anayeabudiwa na Wakristo, Waislamu, Wahindu, Wabudha lakini lazima uamini Mungu yupo.

NITHIBITISHIE KUWA MUNGU HAYUPO
Kwa nini hiyo first source unasema ni Mungu?

Mungu ni nini?

Kwa nini iitwe hiyo first source iitwe jina "Mungu"?

Aliye ita hii first source "Mungu" ni nani? Au hii first source alie kwambia inaitwa "Mungu" ni nani???????
 
Back
Top Bottom