MKWEAMINAZI
JF-Expert Member
- May 28, 2023
- 930
- 1,299
Wenye Akili kubwa tulijua tu kuwa mkutano wa CHADEMA Temeke utapata vizingiti tu kutoka kwa watawala kama sio polisi basi ni CCM au msajili wa vyama. Hatimae yameanza kutokea.
Wahuni wametumwa wakapandishe bendera za CCM eneo la mkutano wa CHADEMA ili kuwe na vurugu zionekane ni za CHADEMA.
Waandishi wa habari wamefanyiwa vurugu za kipigwa na kuibiwa na hao hao wahuni ili ionekane ni CHADEMA.
Sasa kajitokeza msajili wa vyama nae kaja na hadithi zake za Alinacha eti CHADEMA wanachanganya dini na siasa. Namuuliza msajili wa vyama je viongozi wa dini hawaruhusiwi kuhudhuria mikutano ya vyama vya siasa? Je viongozi wa dini sio wananchi? Je ni sheria gani inayowakataza? Mbona Askofu GWAJIMA ni mbunge wa CCM, ile sio siasa?
Wenye akili kubwa tulijua tu kwa kuwa agenda kuu ya huu mkutano ni mkataba mbovu wa bandari, na CCM haitaki sakata la bandari. Wananchi waelezwe ni wazi huu mkutano utapingwa na CCM kwa kupeleka wahuni, na kisha msajili wa vyama auzuie kwa kigezo cha kuwa CHADEMA ndio imesababisha hizo vurugu.
CCM inaonekana inataka yanayotokea Kenya yatokee na Tanzania.
Wahuni wametumwa wakapandishe bendera za CCM eneo la mkutano wa CHADEMA ili kuwe na vurugu zionekane ni za CHADEMA.
Waandishi wa habari wamefanyiwa vurugu za kipigwa na kuibiwa na hao hao wahuni ili ionekane ni CHADEMA.
Sasa kajitokeza msajili wa vyama nae kaja na hadithi zake za Alinacha eti CHADEMA wanachanganya dini na siasa. Namuuliza msajili wa vyama je viongozi wa dini hawaruhusiwi kuhudhuria mikutano ya vyama vya siasa? Je viongozi wa dini sio wananchi? Je ni sheria gani inayowakataza? Mbona Askofu GWAJIMA ni mbunge wa CCM, ile sio siasa?
Wenye akili kubwa tulijua tu kwa kuwa agenda kuu ya huu mkutano ni mkataba mbovu wa bandari, na CCM haitaki sakata la bandari. Wananchi waelezwe ni wazi huu mkutano utapingwa na CCM kwa kupeleka wahuni, na kisha msajili wa vyama auzuie kwa kigezo cha kuwa CHADEMA ndio imesababisha hizo vurugu.
CCM inaonekana inataka yanayotokea Kenya yatokee na Tanzania.