Tukio gani litafuata mwezi April?

Tukio gani litafuata mwezi April?

Kaguta

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2013
Posts
414
Reaction score
504
Kuna mijadala inaendelea kwenye magazeti, vijiweni, kwenye mitandao nk, kuwa serikali inahusika na matukio yanayoendelea nchini ili kuhamisha mijadala ya umma ingawa unatakiwa kiujiuliza kwa nini matukio yamekuwa mengi hivo?

Mwezi January kulikuwa na ghasia za Mtwara, Februari kulikuwa na mauaji ya viongozi wa dini na kutekwa kwa Kibanda, March imegubikwa na suala la Rwakatare na sasa ghorofa lililoporomoka na kuua watu Dar! Mtanzania anayeipenda nchi yake na anayetaka kuona nchi yake ikendelea anaanza kujiuliza tukio gani litafuata mwezi unaokuja?

Serikali ya hawamu hii imeongoza kwa matukio ya kusikitisha! Kumbuka huko myuma matukio kama mabomu ya Mbagala na baadae Gongolamboto, kuzama kwa meli, mafuriko ya Dar nk. Mi huwa nadhani ndiyo maana serikali hii imeshindwa ku-perfoam maana kila wakati wako kwenye misukosuko na hali inapotaulia kidogo muda huo badala ya kuutumia kupanga na kufanya mambo ya maendeleo wao wanaamua kuzunguka dunia!
 
Kuna mijadala inaendelea kwenye magazeti, vijiweni, kwenye mitandao nk, kuwa serikali inahusika na matukio yanayoendelea nchini ili kuhamisha mijadala ya umma ingawa unatakiwa kiujiuliza kwa nini matukio yamekuwa mengi hivo?

Mwezi January kulikuwa na ghasia za Mtwara, Februari kulikuwa na mauaji ya viongozi wa dini na kutekwa kwa Kibanda, March imegubikwa na suala la Rwakatare na sasa ghorofa lililoporomoka na kuua watu Dar! Mtanzania anayeipenda nchi yake na anayetaka kuona nchi yake ikendelea anaanza kujiuliza tukio gani litafuata mwezi unaokuja?

Serikali ya hawamu hii imeongoza kwa matukio ya kusikitisha! Kumbuka huko myuma matukio kama mabomu ya Mbagala na baadae Gongolamboto, kuzama kwa meli, mafuriko ya Dar nk. Mi huwa nadhani ndiyo maana serikali hii imeshindwa ku-perfoam maana kila wakati wako kwenye misukosuko na hali inapotaulia kidogo muda huo badala ya kuutumia kupanga na kufanya mambo ya maendeleo wao wanaamua kuzunguka dunia!
kwani yake maandamano ya kumngoa waziri wa elimu na naibu wake vipi! hayapo tena?
 
Ghadhabu ya Mungu imeiangukia Tanzania baada ya kuona mmemsahau na kuanza kuabudu miungu mingine. Viongozi wa juu wanatamuka jina la BWANA mdomoni lakini usiku wakifunikwa na kuta wanaabudu miungu mingine. Hii imesababisha hasira na ghadhabu kwa Mungu juu ya nchi na Tazama BWANA wa majeshi anasema nitakiadhibu kizazi hiki na cha tatu na cha nne mpaka wageuke na kujua kwa mimi ndimi BWANA wa majeshi. Usiseme kitafuata nini, kaa chini muombe Mungu ili ashusha hasira yake juu ya nnchi ili kizazi hiki kipone. Na ninawaambia kunamatukia makubwa yanakuja wala hamtaamini nafsi zenu kwa kuwa kizazi hiki kimeshalaaniwa. Mwachagua viongozi na kujisemea wenyewe eti chaguo la Mungu wakati Mungu mwenyewe hajasema kuwa ni chaguo lake. Sasa ebu jiulize kwa nini tunakiongozi ambaye ni chaguo la Mungu lakini utawala wake ni Majanga matupo ambayo hatujawahi kushuhudia toka nnchi ipate uhuru eg udini. MUNGU BARIKI TANZANIA
 
mtoa! nenda kwenye ofisi ya msajili wa vifo na uzazi ndiyo utajua statistics ya kupungua au kuongezeka kwa vifo, usiongee bila data, matukio yapo kila siku, kila mwezi na nyakati zote hapa tz. tusidanganyane.
 
mtoa mada! nenda kwenye ofisi ya msajili wa vifo na uzazi ndiyo utajua statistics ya kupungua au kuongezeka kwa vifo, usiongee bila data, matukio yapo kila siku, kila mwezi na nyakati zote hapa tz. tusidanganyane.
 
Kuna mijadala inaendelea kwenye magazeti, vijiweni, kwenye mitandao nk, kuwa serikali inahusika na matukio yanayoendelea nchini ili kuhamisha mijadala ya umma ingawa unatakiwa kiujiuliza kwa nini matukio yamekuwa mengi hivo?

Mwezi January kulikuwa na ghasia za Mtwara, Februari kulikuwa na mauaji ya viongozi wa dini na kutekwa kwa Kibanda, March imegubikwa na suala la Rwakatare na sasa ghorofa lililoporomoka na kuua watu Dar! Mtanzania anayeipenda nchi yake na anayetaka kuona nchi yake ikendelea anaanza kujiuliza tukio gani litafuata mwezi unaokuja?

Serikali ya hawamu hii imeongoza kwa matukio ya kusikitisha! Kumbuka huko myuma matukio kama mabomu ya Mbagala na baadae Gongolamboto, kuzama kwa meli, mafuriko ya Dar nk. Mi huwa nadhani ndiyo maana serikali hii imeshindwa ku-perfoam maana kila wakati wako kwenye misukosuko na hali inapotaulia kidogo muda huo badala ya kuutumia kupanga na kufanya mambo ya maendeleo wao wanaamua kuzunguka dunia!


Kipaji cha uongozi kinapimwa kwa kutatua matatizo Mkuu. Kipaji cha uongozi hakipimwi kwa miteremko katika mipango, bali katika uwezo wa kuhimili milima unayoikuta.

Hii ilikuwa nafasi nzuri ya Serikali hii kuuthibitishia ulimwengu kuwa pale kuna uongozi imara. Haya unayoyaeleza yamemalizwa kivipi ndiyo kipimo chenyewe cha uongozi hicho.

Nikurudishe Nyuma. Ali Hassan Mwinyi alikumbana na changamoto nyingi sana katika medani ya Democrasia. Ulisikia kang'oa mtu kucha? No. Magazeti yalikuwa mengi sana yakimpinga na kumkebehi. Ulisikia Mhariri kamwagiwa tindikali? No. Viongozi wanatofautiana sana katika mbinu za kuendesha nchi, lakini ni kwa namna wanavyo-deal na challenges ndipo tunajua kama ni viongozi Imara au dhaifu.

Kujibu swali lako. Kutumia uwezo wa serikali ambao tunaujua sasa, nashawishika kuamini kuwa Mwezi wa nne anaweza mtu mwingine akakamatwa kwa ajili ya kung'olewa kucha. Hebu tusubiri tuone kipi kinakuja. Mungu wanguuuu...kucha zetu sijui tupeleke wapi maskini sie watu wa Mbeya!!!

Kucha zetu jamani wenzenu...kucha, kucha. Sijui tukafiche wapi!
 
Limeshatokea mkuu tukio la April,ni watu waliokufa mgodini Arusha...bado tukio la May
 
Back
Top Bottom