Ntambaswala
JF-Expert Member
- Dec 7, 2008
- 255
- 78
Kibanda aliwahi kuandika hivi hapa J
''Kwanza napenda kuwafahamisha wachangiaji wa JF kwamba niliandika makala ya uchambuzi (analysis) iliyochapishwa katika ukurasa wa 11 wa maoni na mawazo ya watu binafsi. Baadhi ya watu wamenihukumu kwa kuwa bias wakati yale ni maoni na si habari kama inavyodaiwa na kuelezwa na wachangiaji mbalimbali.
Pili haikuwa lengo langu kuanika udhaifu wa mtu yeyote katika ile makala bali lengo langu lilikuwa ni kumuonyesha Zitto athari za kuitumia ndivyo sivyo haki yake ya kikatiba ya kugombea uenyekiti. Mimi binafsi naamini katika demokrasia lakini pia natambua kwamba demokrasia ikitumika vibaya inaweza kutumika vibaya.
Pengine nilichokisahau ni kuandika pia kwamba, Zitto, Mbowe na wana Chadema walipaswa kutambua kuwa wanakwenda katika uchaguzi wa ndani katika chama chao wakati wakiwa tishio kubwa kwa CCM na katika kipindi kifupi sana kabla ya kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu.
Kwa sababu hiyo basi, wote wanapaswa kuwa makini kuepuka kuzalisha vidonda ambavyo vinaweza kusababisha chama hicho kikawa dhaifu sana badala ya kuwa imara wakati huu. Ni kwa mantiki hiyo nilitumia neno 'anguko' nikionyesha hofu ya kupwaya kwa chama hicho.
Hata hivyo nikiwa mwanahabari, natambua baadhi ya maoni ya wachangiaji wanaojifanya wakimtetea Zitto ni vijana wa CCM ambao tumewasikia mitaani wakisema 'acha Zitto apewe tuwaonyesha jeuri ya CCM'.
Niseme wazi nimekuwa nikiamini siku zote kwamba Zitto ni 'visionary leader' na ambaye kwake yeye hutanguliza maslahi ya chama chake kabla ya yake binafsi. Naamini anaweza akatimiza malengo yake yote mengine ya kisiasa pasipo kuwa mwenyekiti.
Tunaweza kusema lolote tunalolipenda lakini wako watu ambao wanao uwezo wa kujisifu kwamba wameifikisha Chadema na Zitto hapo walipo leo, miongoni mwa watu hao ni sisi 'Wahariri wa Tanzania Daima' ambao siku zote tume-shape ajenda za huyu kijana shupavu.
Nautambua ujasiri wake, nauenzi uwezo wake lakini pia nautambua udhaifu wake kama kiongozi. Anao uhuru wa kukataa au kuukubali ushauri. Ni jambo la bahati mbaya sana kwamba, ndani ya Chadema anaungwa mkono na vijana wajinga.
''Kwanza napenda kuwafahamisha wachangiaji wa JF kwamba niliandika makala ya uchambuzi (analysis) iliyochapishwa katika ukurasa wa 11 wa maoni na mawazo ya watu binafsi. Baadhi ya watu wamenihukumu kwa kuwa bias wakati yale ni maoni na si habari kama inavyodaiwa na kuelezwa na wachangiaji mbalimbali.
Pili haikuwa lengo langu kuanika udhaifu wa mtu yeyote katika ile makala bali lengo langu lilikuwa ni kumuonyesha Zitto athari za kuitumia ndivyo sivyo haki yake ya kikatiba ya kugombea uenyekiti. Mimi binafsi naamini katika demokrasia lakini pia natambua kwamba demokrasia ikitumika vibaya inaweza kutumika vibaya.
Pengine nilichokisahau ni kuandika pia kwamba, Zitto, Mbowe na wana Chadema walipaswa kutambua kuwa wanakwenda katika uchaguzi wa ndani katika chama chao wakati wakiwa tishio kubwa kwa CCM na katika kipindi kifupi sana kabla ya kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu.
Kwa sababu hiyo basi, wote wanapaswa kuwa makini kuepuka kuzalisha vidonda ambavyo vinaweza kusababisha chama hicho kikawa dhaifu sana badala ya kuwa imara wakati huu. Ni kwa mantiki hiyo nilitumia neno 'anguko' nikionyesha hofu ya kupwaya kwa chama hicho.
Hata hivyo nikiwa mwanahabari, natambua baadhi ya maoni ya wachangiaji wanaojifanya wakimtetea Zitto ni vijana wa CCM ambao tumewasikia mitaani wakisema 'acha Zitto apewe tuwaonyesha jeuri ya CCM'.
Niseme wazi nimekuwa nikiamini siku zote kwamba Zitto ni 'visionary leader' na ambaye kwake yeye hutanguliza maslahi ya chama chake kabla ya yake binafsi. Naamini anaweza akatimiza malengo yake yote mengine ya kisiasa pasipo kuwa mwenyekiti.
Tunaweza kusema lolote tunalolipenda lakini wako watu ambao wanao uwezo wa kujisifu kwamba wameifikisha Chadema na Zitto hapo walipo leo, miongoni mwa watu hao ni sisi 'Wahariri wa Tanzania Daima' ambao siku zote tume-shape ajenda za huyu kijana shupavu.
Nautambua ujasiri wake, nauenzi uwezo wake lakini pia nautambua udhaifu wake kama kiongozi. Anao uhuru wa kukataa au kuukubali ushauri. Ni jambo la bahati mbaya sana kwamba, ndani ya Chadema anaungwa mkono na vijana wajinga.