Dr Adam Francis
JF-Expert Member
- Aug 12, 2011
- 464
- 687
Tujikumbushe kidogo ahadi 10 za wana CCM kwa chama chao. Zamani za Mwl. Nyerere kabla ya kupata kadi, wana CCM walitakiwa kuhitimu kwanza darasa la itikadi ya Ujamaa na Kujitegemea. Siku ya kukabidhiwa kadi, ilihitimishwa kwa tamko la mwanachama mpya kuunga mkono ahadi 10 za mwana CCM. Hapa chini, ndizo ahadi zenyewe.
1. Binadamu wote ni ndugu zangu na Afrika ni moja.
2. Nitaitumikia nchi yangu na watu wake wote
3. Nitajitolea nafsi yangu kuondoa umaskini, ujinga, magonjwa na dhuluma.
4. Rushwa ni adui wa haki. Sitapokea wala kutoa rushwa.
5. Cheo ni dhamana. Sitakitumia cheo changu wala cha mtu mwingine kwa faida yangu.
6. Nitajielimisha kwa kadiri ya uwezo wangu na kutumia elimu yangu kwa faida ya wote.
7. Nitashirikiana na wenzangu wote kuijenga nchi yetu.
8. Nitasema kweli daima, fitina kwangu mwiko.
9. Nitakuwa mwanachama mwaminifu wa CCM na raia mwema wa Tanzania na Afrika.
10. Nitakuwa mtiifu na mwaminifu kwa Rais wa Serikali ya Tanzania
1. Binadamu wote ni ndugu zangu na Afrika ni moja.
2. Nitaitumikia nchi yangu na watu wake wote
3. Nitajitolea nafsi yangu kuondoa umaskini, ujinga, magonjwa na dhuluma.
4. Rushwa ni adui wa haki. Sitapokea wala kutoa rushwa.
5. Cheo ni dhamana. Sitakitumia cheo changu wala cha mtu mwingine kwa faida yangu.
6. Nitajielimisha kwa kadiri ya uwezo wangu na kutumia elimu yangu kwa faida ya wote.
7. Nitashirikiana na wenzangu wote kuijenga nchi yetu.
8. Nitasema kweli daima, fitina kwangu mwiko.
9. Nitakuwa mwanachama mwaminifu wa CCM na raia mwema wa Tanzania na Afrika.
10. Nitakuwa mtiifu na mwaminifu kwa Rais wa Serikali ya Tanzania