Nilikuwa Pemba wakati wa uchaguzi. Mvua ilikuwa ikinyesha wakati wa kupiga kura. Lakini akina mama hawakuondoka kituoni na kila mmoja alikuwa na hamu ya kumpigia kura Maalim Seif. Nilishangaa maana ingekuwa bara hali ingekuwa tofauti. Niliwauliza hamasa hiyo wanaitoa wapi, wakasema hali halisi ya maisha magumu ndo inawafanya wananchi watumie turufu yao ya kura kubadilisha mfumo uliopo. Sisi wabara haya hatuyaoni? Kweli tumeridhika na mfumo uliopo hatutaki kutumia kura zetu kuleta mabadiliko? Tujiulize.