mwanamichakato
JF-Expert Member
- Mar 20, 2015
- 1,208
- 1,109
Nikikumbuka biashara ya utumwa na jinsi gani ndugu zetu,jamaa zetu,makabila yetu walivyoteswa ;dhalilika'nyanyaswa'uwawa....,Nikikumbuka ukoloni ulivyodidimiza maendeleo ya nchi nyingi za inayoitwa dunia ya tatu au nchi maskini duniani..nikikumbuka vuguvugu la kudai uhuru na jinsi ndugu zetu/babu zetu walivyopinga/pata vikwazo/fungwa...
Nchi nyingi za kiafrika zinapita katika mapito makubwa kuekelea kupata maendeleo makubwa kijamii,kiuchumi na kisayansi..Mataifa yenye kuidoea Africa huku Tanzania ikiwa moja ya nchi lengwa hayafurahii na hayatakaa yafurahie kuona nchi hizi zikiendelea na kuacha kuwa tegemezi wa misaada ya vyandarua vyenye dawa,dawa za kusafisha maji,sindano za kinga ya pepopunda,tohara,vilainishi,etc etc..
Misimamo thabiti ya viongozi wetu ni kitu kisichotegemewa na mataifa yenye njaa ya unyonyaji ,ukwapuaji rasilimali,utekaji wa uhuru,haki,umoja ili kufanikisha kiu ya wizi wa rasilimali mafuta,madini,gas,vito,maji,n.k...Wapo tayari kufadhiri makundi wanayoyatengeneza kati yetu kwa kutugawa kwa misingi ya itikadi za vyama/dini /ukabila pasipo sisi kujua kwamba twatumika kwa faida ya mataifa husika yenye uroho wa rasilimali..
Sitoshangaa kuona tunapingwa kila kona,sitoshangaa kuona hukumu nyingi za kutukandamiza,sitoshangaa tukiwekewa vikwazo kama vya kwa Mugabe,Gaddafi,...,Sitoshangaa kuona hujuma dhidi ya uchumi wetu,Hujuma dhidi ya Sarafu yetu..Umoja wetu ni kitu muhimu sana katika wakati huu na tuendako..yatupasa kuweka itikadi zetu pembeni,yatupasa kuweka chuki zetu pembeni,yatupasa kuweka kiu zetu za madaraka pambeni huku uzalendo na maslahi mapana ya taifa yakiwekwa mbele zaidi.
Tuitetee Nchi,Tuinenee mema nchi yetu,Tukatae Kuivua Nguo Nchi Yetu,Tuisitiri nchi yetu,Tuhubiri habari njema dhidi ya taifa letu...Tanzania ni mali yetu na vizazi vijavyo.
Nchi nyingi za kiafrika zinapita katika mapito makubwa kuekelea kupata maendeleo makubwa kijamii,kiuchumi na kisayansi..Mataifa yenye kuidoea Africa huku Tanzania ikiwa moja ya nchi lengwa hayafurahii na hayatakaa yafurahie kuona nchi hizi zikiendelea na kuacha kuwa tegemezi wa misaada ya vyandarua vyenye dawa,dawa za kusafisha maji,sindano za kinga ya pepopunda,tohara,vilainishi,etc etc..
Misimamo thabiti ya viongozi wetu ni kitu kisichotegemewa na mataifa yenye njaa ya unyonyaji ,ukwapuaji rasilimali,utekaji wa uhuru,haki,umoja ili kufanikisha kiu ya wizi wa rasilimali mafuta,madini,gas,vito,maji,n.k...Wapo tayari kufadhiri makundi wanayoyatengeneza kati yetu kwa kutugawa kwa misingi ya itikadi za vyama/dini /ukabila pasipo sisi kujua kwamba twatumika kwa faida ya mataifa husika yenye uroho wa rasilimali..
Sitoshangaa kuona tunapingwa kila kona,sitoshangaa kuona hukumu nyingi za kutukandamiza,sitoshangaa tukiwekewa vikwazo kama vya kwa Mugabe,Gaddafi,...,Sitoshangaa kuona hujuma dhidi ya uchumi wetu,Hujuma dhidi ya Sarafu yetu..Umoja wetu ni kitu muhimu sana katika wakati huu na tuendako..yatupasa kuweka itikadi zetu pembeni,yatupasa kuweka chuki zetu pembeni,yatupasa kuweka kiu zetu za madaraka pambeni huku uzalendo na maslahi mapana ya taifa yakiwekwa mbele zaidi.
Tuitetee Nchi,Tuinenee mema nchi yetu,Tukatae Kuivua Nguo Nchi Yetu,Tuisitiri nchi yetu,Tuhubiri habari njema dhidi ya taifa letu...Tanzania ni mali yetu na vizazi vijavyo.