Tujadiliane kuhusu Uhuru, Haki na Mendeleo

Tujadiliane kuhusu Uhuru, Haki na Mendeleo

kifupi kirefu

JF-Expert Member
Joined
Oct 29, 2018
Posts
539
Reaction score
3,507
Watanzania yameletwa kwetu maneno matatu ambayo yanatoa tafsiri ya Tanzania ya kesho chini ya Chadema. Tujiulize maswali haya na tuyataftie majibu kabla ya siku ya kupiga kura.

1. Je, Tanzania hatupo huru? Kwanini tuamini baada ya miaka mingi ya kushangilia na kusherekea siku ya Uhuru bado sisi siyo huru? Uhuru gani tunataka kwa maana ya watumishi, wakulima,wafanyabiashara, wanafunzi na makundi mengine?

2. Haki ni neno gumu na zito kidogo, linapotajwa kwenye ilani ya chama maana yake wamebaini hakuna haki hivyo wanakwenda kuisimamia. Je, Tanzania hakuna haki? Nani anayetakiwa kutoa haki na kwanini ataki kuitoa hiyo haki? Tutaipate na tutajuaje kwamba tumeipata?

3. Maendeleo. Dunia yote inataka maendeleo ila maendeleo endelevu....je tunakosa maendeleo au tunakosa maendeleo endelevu? Nini wanataka kukifanya kuleta maendeleo? Ila pia yapo maendeleo ya watu na maendeleo ya vitu, je tunayo yote au kimoja hakipo? Kipi tunatokosa?

CHADEMA wameleta Jambo hili kwetu, tulijadili
 
Kauli mbiu ya chadema haikosoleki,
Mataga wanajaribu kuikosoa wanashindwa
 
CCM kwakweli haifai tena kuongoza nchii hii wamekuwepo kwa miaka 60 na hakuna la maana walilofanya. Tunahitaji mabadiliko na mabadiliko ya kweli yatatoka nje ya ccm kwa chama chenye mtazamo mpya na endelevu kama CHADEMA.
 
Uhuru: kwa maana kwamba ktk awamu hii kumekuwa na hofu kubwa sana katika jamii yetu kwani ukiokosoa tu unageuziwa kibao kuwa umetukana.

Watu wamekuwa wakishurutishwa kusifu tu vinginevyo unaweza kukamatwa na kupakaziwa kuwa wewe sio raia, mchochezi au hata kutekwa na watu wasiojulikana.

Haki: kumekuwa na manyanyaso mengi dhidi ya watu wenye mitizamo tofauti ya kisiasa pia kwa wengine kama wafanya biashara, wana harakati, waandishi wa habari nk. Kuna watu wengine hadi leo hii haijulikani walipo.

Maendeleo: kiwango cha maendeleo kilichofikiwa hakiendani na rasilimali tulizonazo wala na kiasi cha fedha tulizokopa na serikali hubaki kutumia propaganda nyingi kama kinga dhaifu ya utetezi kwa hii hali.
 
Back
Top Bottom