Tujadiliane biashara zenye faida ya shilingi kwa shilingi

Tujadiliane biashara zenye faida ya shilingi kwa shilingi

hsnaturalfertility

JF-Expert Member
Joined
May 14, 2022
Posts
918
Reaction score
1,946
Ninacholipendea hili jukwaa watu wako serious, hakuna mizaha mingi, lakini pia tunapata mawazo mapya kila siku humu.

Leo naomba tupeane michongo ya biashara zenye faida ya shilingi kwa shilingi. Yaani ukileta mzigo wa milioni 30, ukimaliza kuuza unapata faida ya milioni 30. (Bila kuzingatia ni muda gani utachukua kumaliza mzigo, pia Ceteris paribus.)

Mimi niliwahi kusikia kuwa biashara ya dawa za binadamu ina faida ya shilingi kwa shilingi na wakati mwingine shilingi inazaa shilingi mbili. Wengine wanasema vifaa vya simu hasa ukiweza kuvitoa China kuja kuuza bongo.

Karibuni tupeane michongo zaidi kuhusu biashara za shilingi kwa shilingi.
 
Leo naomba tupeane michongo ya biashara zenye faida ya shilingi kwa shilingi. Yaani ukileta mzigo wa milioni 30, ukimaliza kuuza unapata faida ya milioni 30. (Bila kuzingatia ni muda gani utachukua kumaliza mzigo, pia Ceteris paribus.)
Zipo nyingi sana as long as upo tayari kuwa adui wa Jamhuri na polisi.
 
Naona umeanza kujihami kwanza kuhusu mizaha ya watu kwa kuwasifia kuwa hawana mizaha vizuri sana ume win!

Tatizo hawa wanaochangia na wengine watakaochangia wanaelezea biashara ambazo hawajawahi kuzifanya ni vile tu wanasimuliwa ama wamepita pita kidogo sana kwenye hizo biashara

Mfano hapo juu #12 bwana Masangutu amejitahidi kuielezea biashara ya real estate, ipo hivi mm siwezi kuieleza biashara yangu maana nitaharibu soko, mfano nauza nguo na mteja wangu akajua kuwa nguo nayomuuzia kwa Tsh 30,000/- mm napata faida mara mbili atafanya namna alijue soko na itampa hasira kuwa nampiga, lkn pia hata kwa wafanyabiashara sio wote wanayajua machimbo ya bei rahisi ya bidhaa wanazoziuza kwenye biashara zao, namaanisha hata hao wafanya biashara hawapati faida sawa hivyo nikiweka siri hapa sitawapa hasira wateja wangu tu, hata hao wafanya biashara wenzangu pia nawapa mda wakufukua data zaidi ili wajue mm mzigo napata wapi, nitaongoza ushindani mkuu wacha kila mtu ale kwa urefu wa kamba yake kama

Kiufupi siwezi kuielezea biashara yangu nitakuwa nimetoa siri za kambi biashara ina vitu vingi sana
 
Real estates kwa maana biashara ya kujenga nyumba za kisasa na kuuza,unaweza kupata hadi mara 2 na nusu ya gharama ulizowekeza kwa maana ujenzi.lets say nyumba ya milioni 100 unaweza kuiuza hadi 250m kawaida!
Asante sana mkuu, bonge la idea🙏
 
Back
Top Bottom