Tujadiliane biashara zenye faida ya shilingi kwa shilingi

Tujadiliane biashara zenye faida ya shilingi kwa shilingi

Ninacholipendea hili jukwaa watu wako serious, hakuna mizaha mingi, lakini pia tunapata mawazo mapya kila siku humu.

Leo naomba tupeane michongo ya biashara zenye faida ya shilingi kwa shilingi. Yaani ukileta mzigo wa milioni 30, ukimaliza kuuza unapata faida ya milioni 30. (Bila kuzingatia ni muda gani utachukua kumaliza mzigo, pia Ceteris paribus.)

Mimi niliwahi kusikia kuwa biashara ya dawa za binadamu ina faida ya shilingi kwa shilingi na wakati mwingine shilingi inazaa shilingi mbili. Wengine wanasema vifaa vya simu hasa ukiweza kuvitoa China kuja kuuza bongo.

Karibuni tupeane michongo zaidi kuhusu biashara za shilingi kwa shilingi.
Biashara ya mazao ukiiotea!,Tunanunua gunia la alizeti elfu themanini,mwezi wa kumi na mbili hadi laki2!
 
Nimefanya na naendelea kufanya biashara tofauti tofauti ila biashara ya vifaa vya simu ukiuza rejareja shilling kuzaa zaidi ya mara mbili ni kitu cha kawaida sana,mfano bidhaa unayonunua elfu 6 kuuza Elfu 18 ni kitu cha kawaida na bidhaa unayonunua Elfu 12 kuuza Elfu 30 ni kitu cha kawaida,imagine protecta unanunua mia tano unauza Elfu 3 hadi Elfu 5 kutokana na sehemu ulipo,biashara zipo nyingi ila zingatia sehemu ambayo bado haina competition kubwa
 
Nimefanya na naendelea kufanya biashara tofauti tofauti ila biashara ya vifaa vya simu ukiuza rejareja shilling kuzaa zaidi ya mara mbili ni kitu cha kawaida sana,mfano bidhaa unayonunua elfu 6 kuuza Elfu 18 ni kitu cha kawaida na bidhaa unayonunua Elfu 12 kuuza Elfu 30 ni kitu cha kawaida,imagine protecta unanunua mia tano unauza Elfu 3 hadi Elfu 5 kutokana na sehemu ulipo,biashara zipo nyingi ila zingatia sehemu ambayo bado haina competition kubwa
Wow, this is very powerful, Asante sana mkuu umesaidia wengi kwa post hii
 
Back
Top Bottom