Tujadili Tamthiliya ya Sultan

Okay, endeleeni kutupa updates, maana mimi pressure za tamthiliya au movie huwa siziwezi, nasoma mbele ilikuwaje basi naachana nazo au nabaki naangalia huku nishajua conclusion.
ayaa na hivi hurrem ndio anaongoza harrem sijui itakuaje na ibrahim pasha
 
Kwa hiyo nani atakuwa sultan sasa au ndio itaishaa au watoto wao ,mustafa alifanya kosa gani jamani mpaka kuuawa?
 
na kwa nn sultan atahisi hadija kamteka hurrem?? Mana ndio hapo hadija atakapojiua!
 
na kwa nn sultan atahisi hadija kamteka hurrem?? Mana ndio hapo hadija atakapojiua!

madam s hadija atajishuku yeye mwenyewe kwa kuzani kuwa sultan atafahamu kama yeye ndo kamua hurem kumbe hurem hajafa

So kwa ile khofu tu hadija atajiua kwa kuogopa kuuliwa na sultan
 
Wewe ni muongo,
Ibrahim atauliwa na Sultan kwa kumtumia Watu (Wasiojulikana) wakamnyonge usiku wakati amelala.

Hapo Sultan atakua amewaua waume wawili wa dada zake (mashemeji zake), maana hata yule dada yake mwengine pia alimuulia mumewe.

Hata Mustafa hatokaa aurithi U-Sultan maana hata nae atakufa kabla ya Sultan, hao hao Watu Wasiojulikana Watamnyonga Shehazad Mustafa mbele ya Sultan kwa maagizo yake.

Nigal Kalfa atagundulika usaliti alioufanya kwa Hadije, adhabu yake itakua ni kupigwa mishale juu ya Mlima ili aangukie korongoni, lakini ataamua kujirusha mwenyewe (kujiua).

Baada ya Sultan Suleiman kufa (Shehazade Mustafa akuwa ashatangulia kabla yake) atakaerithi U-Sultan ni Shehazad mwengine mtoto wa Hurem.
 
Sultan ndiyo nani?
Sultan Suleiman Khan anaingiaaaaaaaa,
Pisha njiaaaaaaaa...!!!

Ukisikia hivyo basi inabidi msimame na muinamishe vichwa chini. Na kama mlikua mnapiga story basi mkae kimya maana mkulu anapita hapo mida hiyo.

Huyu ni aliekua ntawala wa Ottoman Empire, Himaya iliyotawala Mabara Matatu, wenyewe walimuita Mtawala wa Dunia. Himaya hii chimbuko au makao makuu yake ni Uturuki.

Ilikua ni himaya nyingine kuchagua either kua chini ya himaya hii au kuchapana mkono (vita). Na kwa vile himaya/dola/utawala huu ulikua na nguvu basi wengine walikubali bila vita, na waliokaidi walichapwa.

Sultan alikua ni Mtawala Strong, anaeogopwa na mataifa/himaya zingine. Na hata ndani kwake pia watu walimuheshimu na kumuogopa pia, ila udhaifu wake tu ni pale alipoingia kwenye penzi la Suriya Mtumwa wa Kirusi aitwae Alexander (Baadae alikuja kubadili dini na kuitwa Hurem- Mburudishaji).

Sultan alikua akimuona huyu mdada hapindui kabisa, kufikia kuachana na Mwanamke aliezaa nae awali (Mahdevran) na kumuoa huyu. Huyu Mahdevran pamoja na kuachwa still aliendelea kuishi kwrnye Kasri.

Mama yake Sultan (Afsa Hattum) au Validen kwa cheo aliupinga kwa nguvu zote uhusiano huu lakin Sultan hakusikia la yoyote. Ikawa ni mashindano kati ya Alexander (Hurrem) vs Validen & Mahdevran kwa pamoja. Ila sababu Hurrem ana backup ya Sultan mpenzi wake, aliweza kuruka vihunzi.

Hurrem alikua na wafuasi wake miongoni mwa vijakazi, walinzi, mamesenja, etc. Vivyo hivyo kwa Valide& Mahdevran, so haikua bifu au vita ya kitoto between them.

kifupi ni hivyo.
 
Hicho kipengele cha 5 naona umeamua kutunga script ya kwako.... Ukilisikiliza tangazo la hiyo Tamthiliya ya Sultana kuna maneno huwa yanasemwa kwamba, "Penzi lilikomuibua mtumwa na kuwa mwanamke mwenye Nguvu zaidi duniani". Anyway ngoja tuone....
 
Ni kweli mkuu ubaya wa tamthilia hii Ni kuwa inatabirika mno yaana unawwza ukat aviri kipande kijaacho kitakuwaje hii sio dalili au sifa ya tamthilia nzuri
Good. Point. Ndio ubovu wa hii tamthilia,unaweza kabisa kuitabiri na ikawa hivyo. Mimi mara nyingi nawatabiria,ni chache nabug. Usipoiangalia siku moja haikusumbui kichwa kama zilivyokuwa ACAPRUCOBEY
 
Hicho kipengele cha 5 naona umeamua kutunga script ya kwako.... Ukilisikiliza tangazo la hiyo Tamthiliya ya Sultana kuna maneno huwa yanasemwa kwamba, "Penzi lilikomuibua mtumwa na kuwa mwanamke mwenye Nguvu zaidi duniani". Anyway ngoja tuone....
Mkuu,hapo mimi hakuna ninachokijua mbele,kila nilichoongea hapo ni vya kutunga tu kama ulivyoongea, kwa minajiri ya kubashiri tu. Sina ninachokijua mbele. Japo kwa hii tamthilia mara fulani fulani nilizotabiri ikawa,hata kwa 60%. Inatabirika
 

Atakae kuwa sultan ni selim yule mtoto wa hurem
 
ibrahim ndio kafariki sioni uzuri wake tena
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…