Sajenti
JF-Expert Member
- Apr 24, 2008
- 3,651
- 412
Zikiwa zimebakia tabribani saa 8 ili ule mpambano wa watani wajadi Simba na Yanga ufanyike, kumekuwa na tambo za kila aina kutoka pande zote mbili. Kinachonifanya nione mpambano wa leo kuwa mtamu si tu kuwa Simba na Yanga wanacheza bali ni aina ya mechi ya leo. Kwa mujibu wa kanuni za mashindano ya Tusker hii ni hatua ya nusu fainali hivyo leo vyote vyote iwavyo lazima mtu apigwe bao ili apatikane mshindi wa kuingia fainali hatimaye kukutana na Sofapaka ya Kenya. Hilo ndio kubwa linalofanya pambano la leo kuwa tamu tofauti na mengine tuliyozoea ambapo timu zikitoka sare ndani ya dakika 90 kila mtu anaenda nyumbani na maumivu nusu. Leo mpaka kieleweke.
Mimi binafsi naipa Simba nafasi kubwa ya kuibuka na ushindi ndani ya dakika 90. Piga uwa mnyama atatafuna kandambili 2-0.
Mimi binafsi naipa Simba nafasi kubwa ya kuibuka na ushindi ndani ya dakika 90. Piga uwa mnyama atatafuna kandambili 2-0.