Speaker bwana akili kama za YO YO,......... ina maana majukwaa mengine tunatumia makalio?Kama kuna majukwaa watu wanatumia akili zao basi ni
JF Doctor,Business forum,na jukwaa la Tech,....
Mkuu, kwanza nikushukuru kwa kunizindua, Pili nakushukuru kwa Lugha nzuri ambayo licha ya kuwa ni malalamiko umeifikisha kwa namna inayokubalika. Ahsante. Mwisho nakushukuru kwa kuniomba ufafanuzi au kuomba radhi.Mkuu Gazeti,
Naheshimu sana mawazo yako na uhuru wa kujieleza. Tatizo la uhuru huwa ni mipaka na unapovuka inaleta sintofahamu.
Nimekusoma na kuelewa mantiki yako, ujumbe ulioukusudia umefika mahali husika. Kwa bahati mbaya umefanya hivyo kwa kwa gharama ya kudhalilisha majukwaa mengine.
Watu wanatembelea majukwaa na wanamachaguo yao.Ubora wa majukwaa ni suala binafisi na ubora unatafsiri nyingi. Unaweza kuwa ni kutokana na wingi wa wasomaji, wachangiaji, aina ya wachangiaji, impact yake kwa jamii n.k.
Umeliangaliaa jukwaa la SIASA(JLS) kwa mtazamo hasi sana, ukituhumu kuwa ni sehemu ya malalalmiko bila ufumbuzi na kejeli kadhaa.
Kwa mintaarafu hii, maoni yako hayakuwa na sababu yoyote ya kuhusisha jukwaa la siasa kwani yalilenga kwa vijana wadogo.
Maoni yako yamepokelewa na wadau wa jukwaa la SIASA kwa mitazamo ya maudhi, kejeli na dharau.
Labda ufafanue point ya 4 na 5 ili ueleweke, au uombe radhi kwa usumbufu uliowapata washiriki wa JLS.
Ahsante
Mkuu, kwanza nikushukuru kwa kunizindua, Pili nakushukuru kwa Lugha nzuri ambayo licha ya kuwa ni malalamiko umeifikisha kwa namna inayokubalika. Ahsante. Mwisho nakushukuru kwa kuniomba ufafanuzi au kuomba radhi.
Awali ya yote napenda kuwaomba radhi wadau wa jukwaa la siasa kwa usumbufu uliojitokeza kutokana na kueleweka vibaya kwa kauli yangu.
Nilichokusudia katika nukta namba 4 na 5 si kudhalilisha, nilichokusudia hapa ni kuwa mengi ya mambo yanayozungumzwa katika jukwaa hilo ni Ishu nyeti za taifa kama vile ufisadi, rushwa n.k lakini wanaozungumziwa wenyewe ni kama kumpigia mbuzi gitaa.
Leo unazungumza hivi kesho yeye anapanda ndege kwenda Ulaya ndo hapo nilipoeleza kuwa sisi tumeshika makali yaani tunaumia tu na tukisema tuvute zaidi ndo tutakatwa kabisa na makali hayo.
Pia nimezungumza ubora wa majukwaa, nafikiri nilishaweka wazi kuwa ubora huo ni kwa mtazamo wangu binafsi. Si kwamba ninalikejeli jukwaa la siasa, pindi ninapoamua kufuluiliza kwenye jukwaa la siasa basi najikuta hata furaha inapotea. Nikiingia kwenye jukwaa hilo najikuta kama niko gerezani kwani mambo yanayoelezwa ni mazito na ni vigumu kupata ufumbuzi wa moja kwa moja hapa jukwaani lakini MMU majibu na utatuzi ni papo kwa papo - Hilo ndilo nililokusudia.
Mwisho nawaomba radhi wadau wa SIASA kama nimewakwaza kwa namna moja au nyingine.
Ahsante.
mimi nahamia jukwaa la bussiness bwana ngoja nipungue humumimi ningeweza ningepunguza watu jukwaa la mmu....
Na kuongeza watu jukwaa la bussiness...na jukwaa la tech and gadgets....
Halafu tunashangaa why hatupigi hatua...