Matukio yanayotokea sasa katika nchi yetu ni mchanganyiko wa mambo mengi na la msingi zaidi nionalo<br />
kwetu sisis watanzania kulalamika kwamba hali ngumu na viongozi hawawajibiki. Ok yawezekana kweli hawawajibiki wanakula rushwa au <br />
wanajali maslahi yao kuliko ya nchi yao na wananchi wao. <br />
Sasa wananchi sisi tunaolalamikia kila kitu tunawajibika vipi? Utakuta mtu yupo mitaani badala ya kuwa kwenye meza yake saa za kazi na<br />
wakati mwingine mtu yuko kazini lakini yupo kwa sababu yupo hafanyi kazi ipaswavyo ni soga tu na matokeo yake kazi zinarundikana <br />
hazimaliziki on time! mwisho wa siku kunakuwa kuna viporo na mwisho wa yote tunaingiza hasara katika makampuni na mashirika.<br />
Tufanyeni kazi tuche kulalamikia kila kitu bila kazi uchumi wetu utakuwaje na maisha bora yanapatikanaje bila kukuza uchumi?