TUCTA mumepumbazwa vya kutosha amkeni

TUCTA mumepumbazwa vya kutosha amkeni

kamtesh

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2014
Posts
1,395
Reaction score
514
Nchi hii sio ya mtu mmoja wala wachache kufurahi. Hela za umma zakununua madiwa zipo. Huko nikuchezea hela za walipa kodi. Hela zakuanzisha vimiradi hovyo hvyo bila mpangilio zipo. Yaani serekari imefika mahala hata kufwat budget haitaki. Rais kawa paymaster general mwenyewe, waziri wa fedha mwenyewe, na mambo mengine yote kuhusu pesa mwenyewe. An an amria tuu, kitugani kifanyike bila wakumpinga kwamba hapa ni kinyume na utaratibu.
Uhaki wa watumishi mkubwa ulishaisha, leo hukakiki umekua kisingizio chakuanyima haki na stahiki zao watumishi.
Watanzani na watumishi wa nchi ni wapole sana na waelewa na wavumilivu. Ila tunakoenda uvumilivu utawashinda. Huu ni uonevu kwa watumishi. Watumishi wanawategemezi wengi tuu. Hilo mdo hii serekali inafumbia macho.
Uchumi kukua ni pale mzunguko wa pesa unakuwepo mzuri. Usiwe unakamua tuu makodi kwa watumishi na wafanyabiashara wakati hakuna biashara.
Viongozi tembeleeni maduka masoko muone kama kuna biashara.
Kwenye uchumi ni toa pesa kama serekari, kisanya kodi sababu biasha itakuwepo. Watu wakipata pesa, patakua maujenzi mbali mbali nchi nzima, watu watafanya biashara vizuri tuu, wewe kama serekari, nikuweka mifumo mizuri yakukusana kodi na kuziba mianya ya ukwepaji wa kodi. Tukifika hapo, nchi itasonga vema. Sio kuhodhi pesa kwakufikiri wananchi wanastarehe. Hela ilikua inavuja kwasababu ya mifumo mibaya iliyo kuwepo ya ukusanyaji kodi.
Kwahio basi, mbona maendeleo yalikuwepo kabla ya yeye kua rais. Na biashara zilistawi sana, leo nitofauti sana. Wananchi biashara zaziendi, huu niukweli.

Wakati wa Rais JK, with little makusanyo na wafanyakazi hewa, vyeti feki, mishahara ilikua inanyongeza ya kila mwaka. Na watumishi waliweza kupata mikopo mizuri kwenye mabenki nakufanya mambo ya maana ya maendeleo.
TUCTA na vyama vingine kazeni kamba huu ni uonevu wa mchana kweupe kwa watumishi wa umma. Tuache siasa kwenye maisha ya watu, ni haki ya watumishi wote kupata nyongeza na sio ombi nyongeza ya mwaka. Ni miaka miwili sasa bila bila.
 
Subiria pakuche kama hichi ulichokiandika utakikuta!
 
Lakini kwa upande mwingine wakome utakuta hawa hawa watumishi wamevaa manguo ya kijani ya laana ya ccm na kuimba ccm mbele kwa mbele juzi mkulu anasema sitapandisha mishahara watu wanapiga makofi yaani ndio maana tunaambiwa asilimia kubwa ya watanzania walishasomewa albadiri hawajielewi
 
Mazoea hujenga Tania nayo tabia hukuza stadi na stadi huleta ujuzi ambo
 
Iwapo hulka IPO KTK watumishi,pasi shaka ongezelo la maslahi ni njia kuu pekee ya kuongeza ufanisi,
 
Wamelala fofofo, watumishi wengi hutumiwa na wanasiasa ili kufanikisha malengo yao ya kisiasa, kuna majitu nayakumbuka jinsi yalivyokuwa yanashabikiashabikia kampeni za Juma,,,, leo wanalialia tu, makato ya bodi na bado mikopo mingine benki na bado hakuna nyongeza ya mshahara. Na bado, hadi akili ziwasogee ndo mtakoma.
 
Ni hatua zipi mtumishi anaweza kuchukua ili kujitoa katika vyama kama TUGHE, CWT au TALGWU? havina umuhimu wowote kwa mtumishi.
 
Jana msomaji wa serikali kasema TUCTA inapotosha umma Mh Rais akusema eti hapandishi mshahara
 
TUCTA jibuni taarifa ya serkali bila kuogopa kwani taarifa yenyewe ina majibu mepesi na iliyojaa takwimu ya kupika,watumishi wangapi wamelipwa hiyo bilioni 70 na ni katika halmashauri zipi? Salary slip ya watumishi inaonyesha hakuna increments zozote toka 2015/16 na 2016/17.
 
Mkuu, TUCTA wakimjibu msema ovyo Wa serikali unishitue maana sitegemei hilo kutokea. Kuna kiongozi anaitwa Oluoch huko chama cha Walimu alionekana bonge la kiongozi wakati wa bunge la katiba, alivyolambishwa vya kulamba!! Lo! Acha bwana!
 
Watumishi wa bongo wakapimwe mkojo. Wanaambiwa hakuna increment wanashangilia. Ivi wangeambiwa increment ipo sijui wangefanyaje
 
TUCTA imetekwa na ccm, ndo maana haina meno. Nyongeza ya kila mwaka ni haki ya mtumishi na sio ombi.
 
Back
Top Bottom