Tuandae mustakabali (future) nzuri kwa watoto wetu

Tuandae mustakabali (future) nzuri kwa watoto wetu

Darvon

Member
Joined
Apr 14, 2018
Posts
93
Reaction score
74
Habarini za asubuhi.

Wakati tunakwenda makazini tujukumbushe yafuatayo.

Mambo yamebadilika kwa sasa na dunia imekuwa kijiji ambacho mwenye nguvu ndio anakula mema na tunawaandaa watoto wetu kuja kuishi na mwanakijiji mwenzie kutoka huko kwenye kona nyingine ya kijiji, hivyo basi tuwape maarifa kupitia elimu nzuri, kwa dunia hii wewe jiandae tu kutawaliwa milele endapo utashindwa kuwatengenezea mazingira mazuri wanao yatakayokuja kuwasababisha wawe na nguvu katika jamii wazungu wana msemo wao "Survival of the fittest"

Nakuambia niamini mimi kila kitu kizuri duniani ni gharama, mtoto hatakiwi afaulu tu mzee anatakiwa yaani ukikaa nae unaiona dunia nyingine nyumbani kwako. Nenda tu hapo kenya utagundua tofauti yetu na wakenya kwenye hiyo idara unaweza kuwa na makampuni au majumba mazuri lakini nakuhakikishia kuwa na mtoto aliyeandaliwa katika kiwango cha dunia ya kwanza ili asitafute kazi ila kazi zimtafute ni gharama sana.

Endapo pia gharama huna hilo sio tatizo muweke mtoto katika misingi mizuri itayomfaa katika maisha yake, mpe maarifa tofauti tofauti huku ukihakikisha kuwa haendi kuungana na makundi mabovu ya kumfundisha tabia za hovyo.

Thamani tunayowapa watoto wetu ndio watakayokuwa nayo maisha yao yote, maisha uliyonayo wewe ndio yanayowapa heshima wao pia mtaani, kizazi chetu kisije kuwa cha kudharaulika, nakuhakikishia kuwa ukishindwa kumuandaa mtoto wako aje kuwa "fit" zaidi ya wengine atadharaulika yeye, wewe, na wengine wote waliohusika katika future yake.

Sipendi ile tabia mzazi kumuambia mwanae mbona mimi nilitembea peku? Mbona nilivaa nguo zilizotoboka? Ni kama mtu vile anapambana kulipa visasi kwa mtoto, dunia ya leo ukimuandaa mtoto kwa aina hiyo ya maisha kumuacha kama vile hana wazazi, utakuta amechomwa moto, dunia ya leo sio ile ya 70, 80, na 90s.

Binafsi ninamuomba Mungu aniwekee kizazi changu, sina jina wala uwezo kivile wa kuwafikia watu kama kina @djkhaled na wenzake, ila muda si mrefu wajiandae kuona upendo wa masikini kwa mwanae unakuwaje.


Mlee mtoto katika njia impasayo naye hataiacha..!


Muwe na siku njema.
 
Ndio kwakua maisha ni mfumo,kama wazazi wako hawakukuachia mfumo mzuri usilalamike..we pambana ili uache mfumo mzuri kwa wanao ili siku moja wasije kulalamika.
Wanangu ngada wasile..vingine ruksa


IMG_20180415_155501.jpg
 
Nishasema, kila mmoja atabeba msalaba wake. Mtoto atayeshindwa masomo atapelekwa VETA angalau akajifunze kuosha magari. Atayefaulu atakwenda shule ya kata na kingereza atajifunzia kwenye Isidingo.

Siwezi kuishi kwa shida na kwenda kuteketeza rasilimali pesa kisa mtoto akafundishwe kingereza. Pesa zangu ni za kutumbua mimi na mke wangu. Wengine ni by the way. Nishawaambia watoto wangu. Hapa ni kama wamepanda daladala ambayo konda asipoweza kukimbilia na kudandia, anaachwa kituoni.

Wenye pesa za kuchezea endeleeni kuziteketeza. Mimi nimesoma shule za kata, ila nikikaa na Max Melo tukaongea kiingereza, utadhani tumeshuka kutoka Marekani.

Ninaandika hivi nikisikitika, baada ya kumuona ndugu yangu mwenye maisha ya kuunga unga akiteketeza pesa yake English media. Milioni mbili kwa mwaka ni pesa ya matofali ya block elfu mbili, kwa watoto watatu ni matofali elfu sita. Mpaka wamalize darasa la saba ni matofali elfu 42! (Iyo p/m, bado hujazungumzia sekondari). Hiyo pesa si bora ujenge majumba wakae?

Kupeleka mtoto kufundishwa kiingereza English media kwa pesa ya kuungaunga ni sawa na kumlipia mtu fedha aishi hotelini ihali wewe unalala kwenye nyumba ya nyasi.




 
kweli tuandae kijanja kama waarabu wanavyofanya na wahindi..

mzee gulam dewji kawalea kina MO vizuri.. shule kawasomesha IST na chuo kawapeleka marekani wote... mazingira waliyolelewa kina MO hata tabia mbaya za uswahilini na uhuni au mademu wa uswahilini ni ngumu kukutana nao... hadi ndoa zao ni kama zinapangwa na mzazi kutokana na mazingira anayokulia na hata watoto anaocheza nao..

Au wale wenye Azania unga kina Awadh.. wote shule IST na vyuo marekani.. angalia wanavyoshindana biashara huyu kiwanda cha unga, huyu Lake oil huyu malori kibao..

angalia sumaria group, kina LN shah, murzah group jinsi wanavyolea watoto wao.. huwezi kukutana nao kizembe zembe uwafundishe tabia mbaya

mtoto akilelewa vizuri akili inakuwa nzuri na future yake inakuwa nzuriii hadi wajukuu na wajukuuu wanakuwa na future..

Toyota ni kampuni ya ukoo ipo miaka zaidi ya 100 tangu mtoto anazaliwa huo ukoo analelewa ki toyota toyota tu kuanzia shule hadi watoto wa kucheza nao anacheza na washua wenzake tu wanaojielewa,,, hata girlfriend hawezi kukutana na mpuuzi aliyeyelewa kiujanja ujanja..

shule na mitaa ya kukulia mtoto wako ni muhimu sana kuitambua


na tukumbuke zama hizi urithi kwa mtoto sio elimu peke yake bali family business na elimu nzuri
 
kweli tuandae kijanja kama waarabu wanavyofanya na wahindi..

mzee gulam dewji kawalea kina MO vizuri.. shule kawasomesha IST na chuo kawapeleka marekani wote... mazingira waliyolelewa kina MO hata tabia mbaya za uswahilini na uhuni au mademu wa uswahilini ni ngumu kukutana nao... hadi ndoa zao ni kama zinapangwa na mzazi kutokana na mazingira anayokulia na hata watoto anaocheza nao..

Au wale wenye Azania unga kina Awadh.. wote shule IST na vyuo marekani.. angalia wanavyoshindana biashara huyu kiwanda cha unga, huyu Lake oil huyu malori kibao..

angalia sumaria group, kina LN shah, murzah group jinsi wanavyolea watoto wao.. huwezi kukutana nao kizembe zembe uwafundishe tabia mbaya

mtoto akilelewa vizuri akili inakuwa nzuri na future yake inakuwa nzuriii hadi wajukuu na wajukuuu wanakuwa na future..

Toyota ni kampuni ya ukoo ipo miaka zaidi ya 100 tangu mtoto anazaliwa huo ukoo analelewa ki toyota toyota tu kuanzia shule hadi watoto wa kucheza nao anacheza na washua wenzake tu wanaojielewa,,, hata girlfriend hawezi kukutana na mpuuzi aliyeyelewa kiujanja ujanja..

shule na mitaa ya kukulia mtoto wako ni muhimu sana kuitambua


na tukumbuke zama hizi urithi kwa mtoto sio elimu peke yake bali family business na elimu nzuri
Umenena suala la msingi sana, njia pekee ya kuibadilisha kesho ni kupitia younger generation maana mali tutakazotengeneza hazitojiendesha zenyewe inabidi zipate wasimamizi ambao wanatoka ndani ya familia.
 
Back
Top Bottom