Tuambizane Ukweli

Tuambizane Ukweli

RASCO BOY

JF-Expert Member
Joined
Jul 29, 2018
Posts
428
Reaction score
485
Kwa pande zote mbili Mwanaume na Mwanamke...Unaonaje hii

Kufunga ndoa na mtu unaemjua..ama kufunga ndoa na mtu usiemjua..ipi ina ladha sana najua ushanielewa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unafungaje ndoa na mtu usiyemjua?

Imetokea kwa binamu, aliolewa na jamaa yuko Dubai hakuwahi kumuona kabla, zaidi ya kutumiana picha, siku ya harusi alikuja mwakilishi wa yule mume akapiga goti na baada ya siku mbili binamu akatua Dubai kukutana na mumewe, alikuwa ni mlemavu, mwili umeishia ktk kiuno, shida ikaja dogo kumkataa nao wakadai mahari yao na uncle ashaongezea kaagiza fuso, ikabidi atafutwe m babu huko huko amuoe binti wa miaka 18 m bichi, mzee akatoa mahari ikachukuliwa ile mahari ikarudishwa kwa aliyemuoa mwanzo, kufika kwa mzee akakuta kuna wake wawili na yeye akawa wa tatu, huko nako akakuta babu mashine haina kazi, dogo akaona kama anagundu...babu anasema ye akioa hajui kuacha..dogo kavumilia mwisho ikabidi anihadithie yaliyomkuta huko, mi nikakausha tu nakula zangu popcorn nacheki picha linaendaje maana nilimtolea posa wakachomoa cna kitu, dogo karudi bongo..wamempiga na jinni juu....so unapozungumzia kuoa ama kuolewa na mtu usiyemjua vingatia vigezo na masharti

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nifunge ndoa na nisiyemjua nigundue nini?lazima nijionee kwanza kama yaliyomo yamo ili tusisumbuane badae

Ukp sahihi.... habari za kuja kuuziana mbuzi kwenye gunia nani anataka.. sema kuna madhehebu mnapewa wiki moja baada ya ndoa mpeleke majibu kama mizigo mmeielewa yan hakuna dosari kila idara ili kama kuna kitu hakiko sawa mnapewa talaka
 
Ukp sahihi.... habari za kuja kuuziana mbuzi kwenye gunia nani anataka.. sema kuna madhehebu mnapewa wiki moja baada ya ndoa mpeleke majibu kama mizigo mmeielewa yan hakuna dosari kila idara ili kama kuna kitu hakiko sawa mnapewa talaka
Hilo dhehebu nimelipenda
 
Unafungaje ndoa na mtu usiyemjua?

Imetokea kwa binamu, aliolewa na jamaa yuko Dubai hakuwahi kumuona kabla, zaidi ya kutumiana picha, siku ya harusi alikuja mwakilishi wa yule mume akapiga goti na baada ya siku mbili binamu akatua Dubai kukutana na mumewe, alikuwa ni mlemavu, mwili umeishia ktk kiuno, shida ikaja dogo kumkataa nao wakadai mahari yao na uncle ashaongezea kaagiza fuso, ikabidi atafutwe m babu huko huko amuoe binti wa miaka 18 m bichi, mzee akatoa mahari ikachukuliwa ile mahari ikarudishwa kwa aliyemuoa mwanzo, kufika kwa mzee akakuta kuna wake wawili na yeye akawa wa tatu, huko nako akakuta babu mashine haina kazi, dogo akaona kama anagundu...babu anasema ye akioa hajui kuacha..dogo kavumilia mwisho ikabidi anihadithie yaliyomkuta huko, mi nikakausha tu nakula zangu popcorn nacheki picha linaendaje maana nilimtolea posa wakachomoa cna kitu, dogo karudi bongo..wamempiga na jinni juu....so unapozungumzia kuoa ama kuolewa na mtu usiyemjua vingatia vigezo na masharti

Sent using Jamii Forums mobile app
Ni muhimu kujuana kwa undani zaidi ukiona mtu ataki mjuane mpaka ndoa ujue uyo atakua na mapungufu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom