GUSSIE
JF-Expert Member
- Dec 2, 2014
- 3,866
- 11,100
Kwa sisi wazee, Tangu utoto wangu sijawahi sikia mtu sehemu yeyote ya Tanzania iwe shule, ofisini au mitaani akiniuliza wewe dini gani? au wewe Kabila gani?. Mambo haya ya ujinga yanaonekana sasa tena kwenye kizazi cha sayansi na digital.
Kuna shida kubwa kwa vijana wetu badala ya kujenga fikra za Maendeleo kwa sayansi na teknolojia iliyopo duniani kwa wakati wao, Wanawaza jina la mtu na kuanza kulitafsiri ni dini gani au Kabila gani Katika kuongoza Taifa.
Mtu wangu wa karibu ninayeishi naye tu wa kuamka na kulala pamoja sikuwahi kumuuliza kabila lake wala dini yake Katika hatua za kumpenda, Kama kuyajua labda Yeye angelisema lakini sio mimi kuuliza ujinga wa dini au kabila.
Yawezekana wazazi wa kipindi chetu walitoa majina yenye maana ya tukio, kitu, ushujaa au hofu na wakati mwingine walipenda tabia ya mtoto fulani na kutoa jina.
Mfano utakutana na watu wanaitwa
Tumaini Ramadhani
Agustino Ramadhani
Mohamed Mawazo
Mohamed Joseph
Mwafilombe Musa Mwakalindile
Maeneo baadhi ya Mwanza na Shinyanga kuna watu Wanaitwa Hamza, Musa, Hussein na Jumanne lakini hawa watu sio waislamu kabisa bali ni majina yanayopendwa sana na baadhi ya watu wa Mwanza, Utawahukumu hawa watu kama waislamu kumbe ni wakristo.
Yapasa watu kutambua jina ni alama tu na alama unaweza kuibadili muda wowote ule.
Jina lako unaweza kulikana muda wowote na kupewa jina ulitakalo na haya yanafanyika kila siku mahakamani na serikalini kwa anayetaka.
Kuna watu Baba zao waliwakana na wanatumia majina za upande wa Mama zao, Wakati Baba na Mama walioana kwa mtazamo tofauti wa ufia dini.
Mfano, Ukoo wa Mama ni wakristo na ukoo wa Baba ni waislamu, Baba kamkana Mama na Mama kapata hasira badala ya kumwita mwanae jina la baba labda Mohamed Hussein Yeye anamwita jina la ukoo wake Mohamed Joseph Kalinga.
Je, utamuhukumu Mohamed kama mwislamu au mkristo?
Je, kwa wale wanaoamini mawazo ya dini hayapo na hivyo vitabu vyenu wa naona ni hadithi tu wasipewe uongozi?
Kuna maelfu ya watanzania hawana mambo ya udini, Kama kila mtanzania angekuwa na dini basi misikiti na makanisa isingetosha kabisa.
Kuna wakati huwa nashangaa vijana wanaongelea Simba na Yanga bila kufanya kazi masaa ishirini na nne na sasa wanaongelea udini masaa ishirini na nne.
Tambua ukiwa na kipaji na ukajituma utaonekana hata Marekani huko utaitwa na wala watu hawataangalia jina lako ni gumu kutamka au jepesi bali wataangalia uwezo ulio ndani yako.
Kuna shida kubwa kwa vijana wetu badala ya kujenga fikra za Maendeleo kwa sayansi na teknolojia iliyopo duniani kwa wakati wao, Wanawaza jina la mtu na kuanza kulitafsiri ni dini gani au Kabila gani Katika kuongoza Taifa.
Mtu wangu wa karibu ninayeishi naye tu wa kuamka na kulala pamoja sikuwahi kumuuliza kabila lake wala dini yake Katika hatua za kumpenda, Kama kuyajua labda Yeye angelisema lakini sio mimi kuuliza ujinga wa dini au kabila.
Yawezekana wazazi wa kipindi chetu walitoa majina yenye maana ya tukio, kitu, ushujaa au hofu na wakati mwingine walipenda tabia ya mtoto fulani na kutoa jina.
Mfano utakutana na watu wanaitwa
Tumaini Ramadhani
Agustino Ramadhani
Mohamed Mawazo
Mohamed Joseph
Mwafilombe Musa Mwakalindile
Maeneo baadhi ya Mwanza na Shinyanga kuna watu Wanaitwa Hamza, Musa, Hussein na Jumanne lakini hawa watu sio waislamu kabisa bali ni majina yanayopendwa sana na baadhi ya watu wa Mwanza, Utawahukumu hawa watu kama waislamu kumbe ni wakristo.
Yapasa watu kutambua jina ni alama tu na alama unaweza kuibadili muda wowote ule.
Jina lako unaweza kulikana muda wowote na kupewa jina ulitakalo na haya yanafanyika kila siku mahakamani na serikalini kwa anayetaka.
Kuna watu Baba zao waliwakana na wanatumia majina za upande wa Mama zao, Wakati Baba na Mama walioana kwa mtazamo tofauti wa ufia dini.
Mfano, Ukoo wa Mama ni wakristo na ukoo wa Baba ni waislamu, Baba kamkana Mama na Mama kapata hasira badala ya kumwita mwanae jina la baba labda Mohamed Hussein Yeye anamwita jina la ukoo wake Mohamed Joseph Kalinga.
Je, utamuhukumu Mohamed kama mwislamu au mkristo?
Je, kwa wale wanaoamini mawazo ya dini hayapo na hivyo vitabu vyenu wa naona ni hadithi tu wasipewe uongozi?
Kuna maelfu ya watanzania hawana mambo ya udini, Kama kila mtanzania angekuwa na dini basi misikiti na makanisa isingetosha kabisa.
Kuna wakati huwa nashangaa vijana wanaongelea Simba na Yanga bila kufanya kazi masaa ishirini na nne na sasa wanaongelea udini masaa ishirini na nne.
Tambua ukiwa na kipaji na ukajituma utaonekana hata Marekani huko utaitwa na wala watu hawataangalia jina lako ni gumu kutamka au jepesi bali wataangalia uwezo ulio ndani yako.