Tuache Masikhara: Rais Magufuli kwa kiasi kikubwa amefanikiwa kudhibiti ujambazi na wizi katika Mabenki

Peter Madukwa

JF-Expert Member
Sep 20, 2012
3,135
2,471
Habari zenu wana Jf,

Sote tu mashahidi kuwa miaka ya nyuma kabla ya awamu ya 5 ya Mh. Rais John Pombe Joseph Magufuli kulikuwa na matukio ya kila mara ya ujambazi ikiwemo uporaji ktk mabenki na kuleta hofu na taharuki kwa wananchi.

Benki ilikuwa siyo sehemu salama kwa sababu ya matukio ya ujambazi ya kila mara.

Hujuma za hapa na pale za uporaji wa fedha na mali zilikuwa zinaleta hofu kubwa sana.

Ilikuwa ni kawaida ndani ya mwezi kusikia uvamizi ktk benki tena mchana kweupe na kuleta athari kubwa ya kiuchumi na hofu katika jamii. Lakini tangu aingie Mh Magufuli, amejitahidi kiasi kikubwa kudhibiti matukio ya uhalifu na kuimarisha usalama wa wananchi na mali zao.

Majambazi na vibaka kwa kiasi kikubwa wamedhibitiwa na wengi wao wameacha na kuamua kufanya shughuli zingine halali za kujipatia kipato.

Wale ambao walikuwa wabishi wameishia kukaa kolokoroni na wengine hata kufa katika matukio.

Rejea tukio la majambazi waliojaribu kuvamia benki ya crdb usiku huko Igoma Mwanza, hawakufanikiwa badala yake wameambulia kifo na kuuawa.

Pia kwa kiasi kikubwa Serikali ya awamu ya 5 imefanikiwa kudhibiti uingizaji, uuzaji na utumiaji wa madawa ya kulevya ambayo kwa kiasi kikubwa ilikithiri na kuharibu vijana wetu wengi ambao ni nguvu kazi ya Taifa.

Wengi ambao walikuwa wanajishughulisha na uuzaji wa madawa ya kulevya wameacha biashara hiyo na kuamua kufanya ishu zingine katika hili tunampongeza Mh Rais.

Hii ndiyo Tanzania tunayoitaka. Tanzania yenye uhakika wa usalama wa wananchi na Tanzania watu wanaofanya kazi kwa bidii ktk shughuli halali.

Kama kila mwananchi ataamua kupambana ktk shughuli halali za kiuchumi nchi yetu itapanda kutoka daraja la kati na kuwa ktk daraja la juu zaidi na pia itaendelea kusaidia kupunguza matukio ya uhalifu ambayo hufanywa na watu wenye tamaa ya kupata mafanikio ktk njia rahisi na haramu.

Hongera mh Rais kwa kudhibiti matukio ya Ujambazi na uhalifu.
 
Mkuu ao ndio ule upande wa kupinga pinga pasipo kushirikisha ubongo, msingi wao mkuu hawajui wanataka nini, leo ndege kesho boda boda, leo nchi masikini kesho takwimu hazisaidii....... Kwakuwa ni watz wenzetu tuwe nao tu .
Kakonko ipi mbona kuna amani kabisa mimi nipo hapa murusagamba amani ya kutosha kabisa
 
Kakonko ipi mbona kuna amani kabisa mimi nipo hapa murusagamba amani ya kutosha kabisa
Niko Kambi ya wakimbizi mtendeli na nduta ninaongea ninachokuwa na uhakika nacho. Wiki iliyopita Kuna watu wametekwa mpaka wa kakonko na kibondo uliza ujibiwe.
 
Mambo ya kuiba kwa silaha yalikuwa zamani.majambazi ya sasa hivi wasomi wanakupiga pesa huku wamekaa makwao.
Watu wanaibiwa sana kila siku,utasikia ile hela lusha kwenye namba hii.
Ujambazi bado upo tena umeongezeka sema wamebadili mbinu zakuiba.
 
Mambo ya kuiba kwa silaha yalikuwa zamani.majambazi ya sasa hivi wasomi wanakupiga pesa huku wamekaa makwao.
Watu wanaibiwa sana kila siku,utasikia ile hela lusha kwenye namba hii.
Ujambazi bado upo tena umeongezeka sema wamebadili mbinu zakuiba.
Ni kweli kabisa dunia imebadilika sasa wizi wa kutumia misuli na nguvu nyingi umepungua sana, sasa ni zama za kidigital.

Daah mkuu hapo kwenye "rusha kwenye namba hii" 😂😂😂😂
 
Amefanikiwa sana kwenye propaganda mambo yapo vile vile na mengine ni mabaya zaidi. Jana tu CRDB Mwanza wamevamiwa na majambazi.
 
Ni kweli kabisa dunia imebadilika sasa wizi wa kutumia misuli na nguvu nyingi umepungua sana, sasa ni zama za kidigital.

Daah mkuu hapo kwenye "rusha kwenye namba hii" 😂😂😂😂
Hawa jamaa ni nuksi unaweza ukesema ni kama utani.ila wanapigahela hatari.
Na wakiona mnaanza kuwazoea wanaboresha ujinga wao sasa hivi wamekuja na hii yakukosea kutuma pesa wanapiga sana watu pesa.
Achana nawale wanaojifanya mawakala wale ndio shida balaa ukiingia kwenye 18 zao ujue wanakomba hadi na hazina yako ya bank.
Vinaja hawana ajira wamaemua kujiajiri shida tupu.
 
Amefanikiwa sana kwenye propaganda mambo yapo vile vile na mengine ni mabaya zaidi. Jana tu CRDB Mwanza wamevamiwa na majambazi.
Hawa vijana wanadhani Tanzania Ni Dar Es Salaam tu.

Kama anajiamini aende kusafiri kipande Cha kasulu kibondo kuanzia saa 12 jion halafu alete mrejesho hapa.


Na ajiulize kwanini gari za kutoka dar kwenda kigoma zikifika tabora zinalala na huwa hazisafiri usiku kucha. Ila zikitokea Kigoma kuja Dar zinasafiri usiku mzima. Ujambazi upo atembee aone.
 
Hawa jamaa ni nuksi unaweza ukesema ni kama utani.ila wanapigahela hatari.
Na wakiona mnaanza kuwazoea wanaboresha ujinga wao sasa hivi wamekuja na hii yakukosea kutuma pesa wanapiga sana watu pesa.
Achana nawale wanaojifanya mawakala wale ndio shida balaa ukiingia kwenye 18 zao ujue wanakomba hadi na hazina yako ya bank.
Vinaja hawana ajira wamaemua kujiajiri shida tupu.
😳😳😳 aiseee, kumbe hao wazee wapo vizuri hivyo, mi huwa nawachukulia kama wapuuzi fulani hivi, kumbe inawalipa sanaa?
 
Amefanikiwa sana kwenye propaganda mambo yapo vile vile na mengine ni mabaya zaidi. Jana tu CRDB Mwanza wamevamiwa na majambazi.
Hawakufanikiwa kuiba na walienda usiku wakaambulia kifo

Hapo nyuma ilikuwa mchana kweupe watu wanaiba benki


Sasa hv haiwezekani
 
Amefanikiwa sana kwenye propaganda mambo yapo vile vile na mengine ni mabaya zaidi. Jana tu CRDB Mwanza wamevamiwa na majambazi.
Ukweli ujambazi umepungua sana mkuu, tuwe tu honest. Hajasema ujambazi umeisha, ilà kwa kiasi kikubwa umedhibitiwa. Pamoja na kuwa hata mimi nilivamiwa na majambazi last yr lakini bado nasimama katika hili, ujambazi umepungua.
 
Habari zenu wana Jf,

Sote tu mashahidi kuwa miaka ya nyuma kabla ya awamu ya 5 ya Mh. Rais John Pombe Joseph Magufuli kulikuwa na matukio ya kila mara ya ujambazi ikiwemo uporaji ktk mabenki na kuleta hofu na taharuki kwa wananchi.

Benki ilikuwa siyo sehemu salama kwa sababu ya matukio ya ujambazi ya kila mara.

Hujuma za hapa na pale za uporaji wa fedha na mali zilikuwa zinaleta hofu kubwa sana.

Ilikuwa ni kawaida ndani ya mwezi kusikia uvamizi ktk benki tena mchana kweupe na kuleta athari kubwa ya kiuchumi na hofu katika jamii. Lakini tangu aingie Mh Magufuli, amejitahidi kiasi kikubwa kudhibiti matukio ya uhalifu na kuimarisha usalama wa wananchi na mali zao.

Majambazi na vibaka kwa kiasi kikubwa wamedhibitiwa na wengi wao wameacha na kuamua kufanya shughuli zingine halali za kujipatia kipato.

Wale ambao walikuwa wabishi wameishia kukaa kolokoroni na wengine hata kufa katika matukio.

Rejea tukio la majambazi waliojaribu kuvamia benki ya crdb usiku huko Igoma Mwanza, hawakufanikiwa badala yake wameambulia kifo na kuuawa.

Pia kwa kiasi kikubwa Serikali ya awamu ya 5 imefanikiwa kudhibiti uingizaji, uuzaji na utumiaji wa madawa ya kulevya ambayo kwa kiasi kikubwa ilikithiri na kuharibu vijana wetu wengi ambao ni nguvu kazi ya Taifa.

Wengi ambao walikuwa wanajishughulisha na uuzaji wa madawa ya kulevya wameacha biashara hiyo na kuamua kufanya ishu zingine katika hili tunampongeza Mh Rais.

Hii ndiyo Tanzania tunayoitaka. Tanzania yenye uhakika wa usalama wa wananchi na Tanzania watu wanaofanya kazi kwa bidii ktk shughuli halali.

Kama kila mwananchi ataamua kupambana ktk shughuli halali za kiuchumi nchi yetu itapanda kutoka daraja la kati na kuwa ktk daraja la juu zaidi na pia itaendelea kusaidia kupunguza matukio ya uhalifu ambayo hufanywa na watu wenye tamaa ya kupata mafanikio ktk njia rahisi na haramu.

Hongera mh Rais kwa kudhibiti matukio ya Ujambazi na uhalifu.
oh yes, pongezi kwake kwa kila kitu.
umesahau kuongezea kuwa watu siku hizi wamepunguza kujamba kwenye daladala - pongezi kwa JPM!

kama kuna mwingine anayekumbuka pongezi nyingine aongezee hapa wandugu.
 
😳😳😳 aiseee, kumbe hao wazee wapo vizuri hivyo, mi huwa nawachukulia kama wapuuzi fulani hivi, kumbe inawalipa sanaa?
Mkuu bongo tuna wajinga wengi mno.
Hao jamaa nimoja ya sababu ya kusajili laini na vitambulisho vya NIDA ila wapi wanaendelea vilevile na hawawakamati.
 
Ukweli ujambazi umepungua sana mkuu, tuwe tu honest. Hajasema ujambazi umeisha, ilà kwa kiasi kikubwa umedhibitiwa. Pamoja na kuwa hata mimi nilivamiwa na majambazi last yr lakini bado nasimama katika hili, ujambazi umepungua.
Ni vigumu sana kuamini serikali hii iliyojikita kwenye propaganda na matumizi ya dola kuficha ukweli. Pengine kinachofanyika tu ni kutokutangaza visa vya ujambazi. Kuna mengi hayatangazwi utafikiri hayapo kumbe habari zinachujwa kama maji ya chupa. Wote mnajua ile habari ya corona na kesi zake imezimwa tu kibabe basi. Thubutu kuzungumzia corona leo kama ni kiongozi basi nafasi yako ndio imeondoka. Nani anathubutu kuzungumzia ile dawa ya corona kutoka Madagascar, thubutu. Nani anathubutu kuzungumzia ATCL kama inapata faida au la miaka miwili baada ya kununua midege ya matrillioni, thubutu. Endeleeni kuishabikia ccm kwa kuwa mnapata faida binafsi ila mjue umma unaumia.
 
Back
Top Bottom