Kibinafsi napata kichefuchefu ninapoona ushabiki wa vyama unaendana na kuvaaa nguo zenye rangi ya bendera za vyama.. Jamani hivi kasumba zimepitwa na wakati. hata hao wachina wa enzi za Mao Tsetung wanavaa suti wakati wa mikutano yao na hata kampeni za uchaguzi. Naomba mtu yeyote atupe majina ya nchi ambazo zinaushabiki huu katika ngazi ya kitaifa. Tuache hizi.. ni uozo katika kizazi hiki kujivisha magwanda ya rangi za chama. CCM ndo kabisa wanapotosha jamiii. Mimi nimetembea sana nchi za wenzetu nasijaona haya. Kwa kweli mtindo huu hauna maana yoyote kwa maslahi ya nchi. Vaaa unavyo vaaa ila kirasmi pembeni peperusha bendera ya chama chako.