Kuna wakati Rais wa Marekani aliulizwa kwa nini Iran hairuhusiwi kumiliki silaha za nyuklia wakati kuna mataifa yanazo?
Rais wa Marekani alijibu kwa kuuliza swali, Hivi ukimwona mtu mzima mwenye busara ameshika kisu unaweza kuwa na wasiwasi wowote? Na vipi ukimwona kichaa anatembea na kisu?
Hii vita inayoendelea, hakika imethibitisha kuwa Iran inaongozwa na vichaa ambao ikitokea wakawa na silaha hatari, Dunia nzima itakuwa kwenye hatari ya kuangamizwa.
Fikiria kuwa Israel na USA ndiyo nchi zinazoishambulia Iran, lakini Iran inarusha makombora hovyo kuelekea mataifa yote ambako makombora yake yanafika. Hao viongozi vichaa wa Iran wanasema wanashambulia taifa lolote rafiki wa Marekani au Israel. Hii ina maana kama Iran ingekuwa na makombora ya kuweza kufika hata huku Afrika, ingeshambulia nchi zote ambazo zina mahusiano ya urafiki na Marekani!
Hakika, ni vyema nchi hii isiwe na silaha yoyote hatari inayovuka mipaka ya Taifa lake. Tuombee hii vita inayoendelea ihitimishe na kuua kabisa uwezo wa Iran kuyashambulia mataifa jirani zake. Israel na Marekani waliona mbali, maana kama Iran ingekuwa na makombora ya nyukilia, sahizi ingekuwa tayari imesharusha.
Maombi yetu makubwa kwa Marekani na Israel, wajitahidi sana kuzuia mauaji ya wananchi raia wa Iran, na hasa watoto. Wananchi wa Iran wamepitia magumu mengi chini ya Ayatollah, hawastahili kuuawa bali kuonewa huruma na kuwathibitishia kuwa uhai wao ni wenye thamani kubwa. Wakiuawa ovyo, wananchi hawa watashindwa kutofautisha matendo ya Ayatollah vs ukombozi unaofanywa na Marekani.
Tunawapa pole wananchi wa mataifa ya Kuwait, Bahrain, UAE, Saudi Arabia ambao kwa kiwango fulani wameumizwa na makombora na drones za Iran.
Hakika, kwaajili ya udalama wa Dunia, Iran isimiliki silaha hatari.
Rais wa Marekani alijibu kwa kuuliza swali, Hivi ukimwona mtu mzima mwenye busara ameshika kisu unaweza kuwa na wasiwasi wowote? Na vipi ukimwona kichaa anatembea na kisu?
Hii vita inayoendelea, hakika imethibitisha kuwa Iran inaongozwa na vichaa ambao ikitokea wakawa na silaha hatari, Dunia nzima itakuwa kwenye hatari ya kuangamizwa.
Fikiria kuwa Israel na USA ndiyo nchi zinazoishambulia Iran, lakini Iran inarusha makombora hovyo kuelekea mataifa yote ambako makombora yake yanafika. Hao viongozi vichaa wa Iran wanasema wanashambulia taifa lolote rafiki wa Marekani au Israel. Hii ina maana kama Iran ingekuwa na makombora ya kuweza kufika hata huku Afrika, ingeshambulia nchi zote ambazo zina mahusiano ya urafiki na Marekani!
Hakika, ni vyema nchi hii isiwe na silaha yoyote hatari inayovuka mipaka ya Taifa lake. Tuombee hii vita inayoendelea ihitimishe na kuua kabisa uwezo wa Iran kuyashambulia mataifa jirani zake. Israel na Marekani waliona mbali, maana kama Iran ingekuwa na makombora ya nyukilia, sahizi ingekuwa tayari imesharusha.
Maombi yetu makubwa kwa Marekani na Israel, wajitahidi sana kuzuia mauaji ya wananchi raia wa Iran, na hasa watoto. Wananchi wa Iran wamepitia magumu mengi chini ya Ayatollah, hawastahili kuuawa bali kuonewa huruma na kuwathibitishia kuwa uhai wao ni wenye thamani kubwa. Wakiuawa ovyo, wananchi hawa watashindwa kutofautisha matendo ya Ayatollah vs ukombozi unaofanywa na Marekani.
Tunawapa pole wananchi wa mataifa ya Kuwait, Bahrain, UAE, Saudi Arabia ambao kwa kiwango fulani wameumizwa na makombora na drones za Iran.
Hakika, kwaajili ya udalama wa Dunia, Iran isimiliki silaha hatari.