Hapa naona kama ni kudanganyana tu. Hivi ni nani aliyewahi kupata partner/mke/mme kupitia njia hii kwa watu wenye majina bandia na uhusiano huu upo na unadumu mpaka leo?
Cheki huyu naye anataka "kuolewa" lakini kwa sharti la kutotaka walimu bila hata kueleza sababu at same times yeye hasemi ni nani (polisi, mjeshi, jini au mama lishe japo kajisema kuwa ni student with no justifications!)
Inawezekana huyu ni "dume" anataka kutuchora na tu hapa na kupoteza muda wa watu hapa. Nashauri uweke vyema request yako ionenye clarity ili kila asomaye akujue kuwa you are serious, pia usijiwekee mipaka ya aina ya mwanaume in terms of professional (i.e kubagua walimu) kwani siku zote mume/mke bora anatoka kwa MUNGU WETU MUUMBA WA MBINGU NA NCHI NA VYOTE VILIVYOMO TUKIWEMO SISI BINAADAMU!!
Sorry, kama nitakukera kwa comment yangu!