Trucking business

Enny

JF-Expert Member
May 26, 2009
962
130
Habari wana jamii forum. Kuna mzee mmoja nafahamiana naye siku nyingi anataka kuingia kwenye biashara ya usafirishaji (malori). Kwa vile sina ajira kwa sasa ameniomba nimsaidie kusimamia biashara yake hiyo lakini mimi sina uzoefu kwenye hiyo biashara, ingawa nimesomea masomo ya biashara.

Kama kuna mtu anaweza kunipa ideas jinsi ya kuendesha biashara ya malori na market yake kubwa ipo wapi? naomba mnisaidie, ili ajira yangu iweze kusimama vizuri ndugu zangu.

Asante
 
Biashara ya malori kwa sasa transit goods zinalipa sana especially kuelekea Congo (Lubumbashi),Zambia,Rwanda,Burundi na Malawi.

Unahitajika kujenga uhusiano mzuri na clearing agents, unaweza kupata contacts zao kutoka kwenye website ya TRA. Fanya mawasiliano nao either by visiting them and make your company known to them.

Fanya research ya kutosha kuhusu yafuatayo
.Bei za kusafirishia mizigo kwenda destination mbalimbali
.Bai na suppliers wa inputs kama matairi na vipuri
.Madereva wazuri na waaminifu na uwalipe vizuri
.Gari gani zinahitajika sana,box body au za kubeba container?
.Angalia washindani wako wakubwa katika biashara na athari zao kwa biashara yako.
.Mafundi ambao ni full time kwa ajili ya magari yako



Faida ya biashara hii ni kubwa lakini inahitaji involvement ya hali ya juu. Unatakiwa ufuatilie kila details kwa sababu unaweza ukajikuta unawafanyia biashara madereva wako,especially mafuta wanauza sana njiani.

Ikiwezekana safiri na magari yako angalau kila route mara moja ili ujue ni kiasi hali halisi ya barabarani kwa sababu umesema hujawahi kuwa katika biashara hii.



KILA LAHERI MKUU
 
Biashara ya malori kwa sasa transit goods zinalipa sana especially kuelekea Congo (Lubumbashi),Zambia,Rwanda,Burundi na Malawi.

Unahitajika kujenga uhusiano mzuri na clearing agents, unaweza kupata contacts zao kutoka kwenye website ya TRA. Fanya mawasiliano nao either by visiting them and make your company known to them.

Fanya research ya kutosha kuhusu yafuatayo
.Bei za kusafirishia mizigo kwenda destination mbalimbali
.Bai na suppliers wa inputs kama matairi na vipuri
.Madereva wazuri na waaminifu na uwalipe vizuri
.Gari gani zinahitajika sana,box body au za kubeba container?
.Angalia washindani wako wakubwa katika biashara na athari zao kwa biashara yako.
.Mafundi ambao ni full time kwa ajili ya magari yako



Faida ya biashara hii ni kubwa lakini inahitaji involvement ya hali ya juu. Unatakiwa ufuatilie kila details kwa sababu unaweza ukajikuta unawafanyia biashara madereva wako,especially mafuta wanauza sana njiani.

Ikiwezekana safiri na magari yako angalau kila route mara moja ili ujue ni kiasi hali halisi ya barabarani kwa sababu umesema hujawahi kuwa katika biashara hii.



KILA LAHERI MKUU
Asante sana kwa maelezo yako mazuri angalau umenipa mwanga wapi pa kuanzia.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom