Treni yaanza kwa hujuma

Treni yaanza kwa hujuma

mgomba101

JF-Expert Member
Joined
Oct 21, 2011
Posts
1,822
Reaction score
711
UZINDUZI wa safari za treni ya abiria jijini la Dar es Salaam, nusura uingie dosari jana wakati kibaka aliyetambuliwa kwa jina la Vincent Michael alipoamua kuiba vyuma vya breki katika moja ya mabehewa yaliyoegeshwa katika kituo cha Yombo.

Tukio hilo lilifanyika muda mfupi kabla ya treni iliyombeba Waziri wa Uchukuzi Dk. Harrison Mwakyembe haijafika katika kituo hicho.

Msafara wa Dk. Mwakyembe aliyeambatana na waandishi wa habari pamoja na maofisa wa Sumatra na wale wa Shirika la usafirishaji la Tanzania na Zambia (TAZARA), ulikuwa unarejea stesheni ya Dar es Salaam, ukitokea katika kituo cha Mwakanga nje ya jiji.

Safari hiyo ilikuwa ni baada ya Waziri Mwakyembe kuzindua usafiri wa aina hiyo kwa treni ya Shirikla la Reli nchini (TRL), uliofanyika eneo la Ubungo Maziwa.

Mmoja wa maofisa wanaolinda katika eneo hilo la Yombo, aliyeomba jina lake lihifadhiwe kwa kuwa si msemaji, alisema kuwa walimkamata kibaka huyo wakati akitekeleza uhalifu wake pasipo kuhofia athari zitakazojitokeza endapo behewa hilo lingeanza kufanya safari zake.

Kufuatia tukio hilo kibaka huyo alibebwa katika moja ya mabehewa yaliyombeba Waziri Mwakyembe na kisha kufikishwa katika Kituo cha Polisi Tazara kwa hatua zaidi.
 
Hayo ndiyo matunda ya Serikali mbovu inayoongoza watu maskini waliokidhiri.
 
Watanzania wote tuwe walinzi wa treni yetu najua wapo watu wanamuonea gere mwakyembe kwa uthubutu wake.
Pia nawaomba EL,RA na AC waje wapande hii treni yetu.
 
dawa ni kuinvest kwenye CCTV kwenye kila behewa lakini hii pia haitamaliza wizi sababu wezi wakubwa ni wafanyakazi na wataiba wakati mabehewa yamepaki
 
dawa ni kuinvest kwenye CCTV kwenye kila behewa lakini hii pia haitamaliza wizi sababu wezi wakubwa ni wafanyakazi na wataiba wakati mabehewa yamepaki

Hata yakipaki, CCTV ni masaa 24 yenyewe haipaki.. CCTV ni lazima,,sio swali.
 
UZINDUZI wa safari za treni ya abiria jijini la Dar es Salaam, nusura uingie dosari jana wakati kibaka aliyetambuliwa kwa jina la Vincent Michael alipoamua kuiba vyuma vya breki katika moja ya mabehewa yaliyoegeshwa katika kituo cha Yombo.

Tukio hilo lilifanyika muda mfupi kabla ya treni iliyombeba Waziri wa Uchukuzi Dk. Harrison Mwakyembe haijafika katika kituo hicho.

Msafara wa Dk. Mwakyembe aliyeambatana na waandishi wa habari pamoja na maofisa wa Sumatra na wale wa Shirika la usafirishaji la Tanzania na Zambia (TAZARA), ulikuwa unarejea stesheni ya Dar es Salaam, ukitokea katika kituo cha Mwakanga nje ya jiji.

Safari hiyo ilikuwa ni baada ya Waziri Mwakyembe kuzindua usafiri wa aina hiyo kwa treni ya Shirikla la Reli nchini (TRL), uliofanyika eneo la Ubungo Maziwa.

Mmoja wa maofisa wanaolinda katika eneo hilo la Yombo, aliyeomba jina lake lihifadhiwe kwa kuwa si msemaji, alisema kuwa walimkamata kibaka huyo wakati akitekeleza uhalifu wake pasipo kuhofia athari zitakazojitokeza endapo behewa hilo lingeanza kufanya safari zake.

Kufuatia tukio hilo kibaka huyo alibebwa katika moja ya mabehewa yaliyombeba Waziri Mwakyembe na kisha kufikishwa katika Kituo cha Polisi Tazara kwa hatua zaidi.

Dah huu umaskini wetu matatizo... umaskini wa akili unatufanya tusifikilie maendeleo,, na umaskini wa fedha ndoo kabisaaa unaongeza tatizo.
 
Vincent michael kwa nini wewe hujasoma kama wenzako waliomo humu ndani wanaojisifia jamii yao wanaakili kuliko jamii nyingine
 
dawa ni kuinvest kwenye CCTV kwenye kila behewa lakini hii pia haitamaliza wizi sababu wezi wakubwa ni wafanyakazi na wataiba wakati mabehewa yamepaki

for sure CCTV na Simu ni muhimu pia spika for announcement in train.
 
Watapata hasara mara mbili kaka. Wabongo wataiba hadi hizo kamera aisee.
 
Kwanza kabisa ni vizuri kila mmoja wetu akaelewa tunawajibika kwa utunzaji wa mali zetu. Hizi ni jitihada tu za wachache wasiopenda kuona wenzao wakifanya vizuri lakini pia jamii ieleweshwe kila mara inapopatikana nafasi juu ya umuhimu wa kujiona wamiliki wa mali za umma. Umaskini ni jambo lingine pia uangaliwe uwezekano wa kuwasaidia vijana wetu hasa kwa elimu na kujitambua maana si kweli kwamba vibaka wote hawana uwezo wa kufanya kazi au wale wanaoomb mchana kutwa si kweli kwamba wote wana matatizo ni kutokujitambua na uvivu ambao umeendekezwa na jamii pamoja na serikali yetu. Kila anayepata nafasi ya kutoa elimu popote afanye hivyo. Ukimpa mtu shilingi 500 tuseme haitamsaidia sana kuliko angeelimishwa akajua kujitafutia hata zaidi ya hapo. Tusibaki kulaumu serikali kila wakati nasi tutumie nafasi zetu
 
Hayo ndiyo matunda ya Serikali mbovu inayoongoza watu maskini waliokidhiri.

Wezi mpaka USA wapo....wizi nitabia mbaya tu alonayo mwanadamu ..wangapi wezi unawajua na wametoka family bora...think before u talk
 
Vincent michael kwa nini wewe hujasoma kama wenzako waliomo humu ndani wanaojisifia jamii yao wanaakili kuliko jamii nyingine

Daah itabidi Vincent wamchangie akasome maana hii jamii wote wamesoma..
 
Vincent michael kwa nini wewe hujasoma kama wenzako waliomo humu ndani wanaojisifia jamii yao wanaakili kuliko jamii nyingine

mkuu nimekugongea bonge la like, chukua jingine "LIKE" angekuwa sio mwenzao ungeona comment zingesomeka kama hivi( alitaka akauze akanunue ubwabwa)
 
Hivi huyo Vincent Michael sio kuwa kuna wasiopenda maendeleo walimpandikiza kweli?...najaribu kufikiria kuwa alijiamni vipi hata akaenda kujaribu kung'oa hicho chuma ulichobainisha mleta mada...
 
Back
Top Bottom