Musa Kadiko
Member
- Jun 15, 2022
- 16
- 18
Shirika la Reli Tanzania – TRC kwa kushirikiana na Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi, Mamlaka ya Reli Tanzania na Zambia – TAZARA, Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini – LATRA, Wakala wa Barabara Tanzania – TANROADS, Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini – TARURA wameadhimisha kilele cha wiki ya usalama wa reli Kamata jijini Dar es Salaam Oktoba 13, 2022.
Aidha, Wiki ya Usalama wa reli huadhimisha tarehe 10 hadi 13 mwezi Oktoba kila mwaka kwa wanachama wa vyama vya reli kusini mwa Afrika (SARA) ikiwa na lengo la kuendelea kusisitiza na kutoa elimu kwa wananchi kuhusu usalama wa reli. Mwaka 2022 Tanzania imekuwa mwenyeji ambapo kaulimbiu ni “CHUKUA TAHADHARI, TRENI ZINA MWENDO WA HARAKA, NI HATARI”.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Mgeni rasmi Mhe. Atupele F. Mwakibete Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi amebainisha kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inatambua vyema umuhimu wa ulinzi na usalama wa miuondombinu ya reli ndiyo maana inaendelea kutoa fedha kujenga na kuboresha miundombinu ya reli ili kuwezesha uendeshaji wa shughuli za reli.
Sambamba na hivyo, Mhe Waziri ametoa wito kwa wafanyakazi wa TRC na Taasisi zingine wajiendeleze kwa kutoa mafunzo ili kuwapa ujuzi waumishi, “nilivyokua napita kwenye mabanda nimeona TRC na LATRA wamepeleka vijana wao nje kupata elimu na ujuzi mpya kwahiyo na taasisi zingine ziige taasisi hizi ili kuweza kuendesha na kusimamia miradi mikubwa kama SGR’’ amesema Mhe. Atupele.
Aidha, Wiki ya Usalama wa reli huadhimisha tarehe 10 hadi 13 mwezi Oktoba kila mwaka kwa wanachama wa vyama vya reli kusini mwa Afrika (SARA) ikiwa na lengo la kuendelea kusisitiza na kutoa elimu kwa wananchi kuhusu usalama wa reli. Mwaka 2022 Tanzania imekuwa mwenyeji ambapo kaulimbiu ni “CHUKUA TAHADHARI, TRENI ZINA MWENDO WA HARAKA, NI HATARI”.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Mgeni rasmi Mhe. Atupele F. Mwakibete Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi amebainisha kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inatambua vyema umuhimu wa ulinzi na usalama wa miuondombinu ya reli ndiyo maana inaendelea kutoa fedha kujenga na kuboresha miundombinu ya reli ili kuwezesha uendeshaji wa shughuli za reli.
Sambamba na hivyo, Mhe Waziri ametoa wito kwa wafanyakazi wa TRC na Taasisi zingine wajiendeleze kwa kutoa mafunzo ili kuwapa ujuzi waumishi, “nilivyokua napita kwenye mabanda nimeona TRC na LATRA wamepeleka vijana wao nje kupata elimu na ujuzi mpya kwahiyo na taasisi zingine ziige taasisi hizi ili kuweza kuendesha na kusimamia miradi mikubwa kama SGR’’ amesema Mhe. Atupele.