Transfer Window 2014/2015, Special thread

MKONGWE Didier Drogba ametimiza ndoto zake za kurejea Chelsea.
Nyota huyo wa Ivory Coast amesaini Mkataba wa mwaka mmoja Stamford Bridge, na kuwa gwiji wa klabu hiyo baada ya awali kusajiliwa na Jose Mourinho kwa Pauni Milioni 24 mwaka 2004. Na Drogba amesema asingeweza kukataa fursa ya kufanya kazi na Mreno huyo tena.
"Ulikuwa ni uamuzi rahisi - Nisingekataa fursa ya kufanya kazi na Jose tena. Kila mmoja anafahamu uhusiano maalum nilionao na klabu hii na wakati wote nahisi kama nyumbani kwangu.



Amerudi: Drogba amerejea Chelsea baada ya miaka miwili tangu aondoke



Kushoto anapima afya na kulia anasaini mkataba wa mwaka mmoja



Kwa upande wake, Mourinho amesema hana wasiwasi Drogba ataisaidia Chelsea, kwa sababu bado anaamini ni mmoja wa washambuliaji duniani.


"Anakuja kwa sababu ni mmoja wa washambuliaji bora Ulaya. Nafahamu haiba yake vizuri sana na nafahamu kama akirudi hatalindwa na historia au kile alichokifanya katika klabu hii mwanzo," amesema Mourinho.
 
namba ya cotinyo kitendawili njo vile kaficha namba
 
Baada ya kipa David Ospina (25, Colombia) kutua Arsenal kwa kitita cha £3.2m, beki kinda wa Southampton Calum Chambers (19, England) naye anakaribia kutua Arseal kwa ada ya £16m.
Kipa Ospina atakuwa kipa namba 1 wa Arsenal na kumweka benchi Wojciech Szczesny.
 
Dili la Loic Remy (27) kwenda Liverpool limekufa rasmi baada ya Remy kudaiwa kufeli vipimo huko marekani. Dau la £8.5m lilikwishakubaliwa na QPR.
 
Beki kinda wa Southampton Calum Chambers (19, England) ametua Arsenal kwa dau la £16m. Chambers anaweza kucheza kama beki wa kulia au beki wa kati (mkoba).
View attachment 173926
 
hali ya usajili c mbaya kama kawaida unaeza tumia pesa nyingi bado ukatoka mikono nyuma tu kama mcmu uliopita
 

Hata asajil vp ASN nafas yake n ya 4 tu
 
Marouane Fellaini (26) huenda akatimkia Napoli, huku Shinji Kagawa (25) akijipanga kurudi Dortmund baada ya wawili hao kutokuwemo kwenye first 11 ya van Gaal.
 
Chelsea inajipanga kumwaga £40m ili kumng'oa Edinson Cavani (27, Uruguay) kutoka PSG.
 
Mancity imesema IMEFUNGA RASMI faili la usajili kwa msimu huu.
 
Kiungo wa Porto anayetisha duniani Juan Quintero (21, Colombia) anakaribia kutua arsenal kwa dau la £15.8m
 
Inasemekana kiungo anayetisha duniani Arturo Vidal (27, Chile) amekamilisha vipimo huko Chile tayari kwa kutua ManUtd kwa dau nene la £47m, na mshahara wa £120,000 kwa wiki.
 
At last beki wa kati wa arsenal Thomas Vemmalaine ametua Fc Barcelona. Kila kitu kipo sawa.

Source: bbcsports breaking news
 
Wakuu bila kuona vidal akitambulishwa bado nitakuwa cna iman

kwani mkimchukua Vidal ndio mtafanya nini? Man united mpaka sasa main target yao ni kucheza ucl, kitu ambacho ni vigumu kwao kwa sasa. Kumbuka city, chelsea, na live top three ni yao. Huku nafasi ya 4 mkigombea na arsenal, spurs, na everton ambayo tangu impate tactician Roberto Martinez wapo on fire mbaya.

Watakao waharibia c hao niliotaja hapo juu bali ni kina Palece, stock city na aina timu kama hizo. Wao hawahitaji ushindi wanachotaka ni heshima.

USHAURI
jiandaeni kiakili kwa matokeo msiyo yatarajia.
 
Louis Nani (27), Fellaini (26) na Kagawa (25) wamo kwenye mpango wa KUTEMWA na kocha van Gaal.
 
Baada ya kupata vifaa vya ukweli, kocha Wenger sasa mawazo yamemjia ya kuwamwaga Lukas Podolski (29) na dogo Joel Campbell (22) ambao wanatakiwa na Galatasaray; huku dogo Serge Gnabry (19) akitakiwa na Crystal Palace na Newcastle kwa mkopo.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…