TRA tax assistant officers

TRA tax assistant officers

Skyblue

Senior Member
Joined
Jan 3, 2014
Posts
196
Reaction score
55
jamani nimeitwa kwenye written interview TRA tarehe 12/12/2014 pale Diamond jubilee hall kwa post tajwa hapo. wanajf naomba nijuzeni kama kuna mtu anajua maswali huwa yanaulizwaje? ntashukuru kwa mwongozo mtakao nipatia. Niwatakieni siku njema na tulivu kwenu nyote.
 
jamani nimeitwa kwenye written interview TRA tarehe 12/12/2014 pale Diamond jubilee hall kwa post tajwa hapo. wanajf naomba nijuzeni kama kuna mtu anajua maswali huwa yanaulizwaje? ntashukuru kwa mwongozo mtakao nipatia. Niwatakieni siku njema na tulivu kwenu nyote.

Tukutane hiyo siku! Same post
 
mimi pia ni mmoja wapo naomba kuuliza je naweza kwenda na provisional result maana bado sijapata transcript?
 
Kwani wamesema twende na original certificate ama transcripts ama ni vyote mtu unapaswa kubeba!?
 
Ngoja ni apply naweza pata mgawo wa Mtwara Gas Pipelines maana Escrow imenipitia mbali aiseee
 
nimepigiwa simu ila email sijatumiwa. Tafadhali aliyepigiwa simu anipe ile namba yao niweze kufanya followup ya email kama introduction yakuripot kwenye interview
 
Written interview na vyeti mnakwenda navyo?nawatakia kila la heri ila mjiandae maswali mengi
 
jamani nimeitwa kwenye written interview TRA tarehe 12/12/2014 pale Diamond jubilee hall kwa post tajwa hapo. wanajf naomba nijuzeni kama kuna mtu anajua maswali huwa yanaulizwaje? ntashukuru kwa mwongozo mtakao nipatia. Niwatakieni siku njema na tulivu kwenu nyote.

Jiandae kwa hesabu za kawaida (general mathematics ), elimu ya uraia (civics), general education, uelewa wako wa mambo ya kimataifa, n.k. Muda huwa hautoshi hivyo ukilemba hutomaliza! Maswali mengi ni ya "common sense".
 
wewe umesha jitoa. Hata usipoteze muda wako kwenda

Wewe usimtishe mwenzako bana! Utashangaa mwenye provisional analamba job,wewe na gamba lako unabaki nalo!!

Mkuu njoo kwenye usaili,wakikutosa basi but usiache kutimba!!
Karibu tukapambane!!
 
Back
Top Bottom