TRA Tanga ni majasusi

Madam vivian original

JF-Expert Member
Joined
Jul 14, 2018
Posts
503
Reaction score
998
Ndugu zangu JF habari za masiku mengi. Nina ndugu yangu amekuja kutafuta maisha Tanga nimempa bodaboda anaendesha na maisha yanaenda.

Leo jioni akanipigia kuna inshu nimsaidie, anasema kuna mpemba katoka zake zenji ana madungu ya mafuta anauzani mafuta ila anauza bei chei dungu elfu60 kwa moja nayeye angeuza 75 kwa moja akanishawishi nimpe hela ili auze chap then angenirudishia pesa yangu.

Nikajipinda nikampa pesa, akanunua kwa mpemba walikua na wenzake kama watatu na wote wakanunua mafuta mpemba akasepa no lisit Wala nini, na wenyewe kwa kuwa hawajui hawakudai risiti wao wakaanza kutafuta wateja sokoni huku na huku TRA Hawa hapa, wakayaona yale mafuta alikua ameweka dukani mawili jamaa kufika wakadai risiti ya yale mafuta, jamaa hawana wakakamatwa na madungu yao hao mpaka TRA na kuanza kufanyiwa umafia huko.

Waliitiwa watu waliovaa mask na kupigwa na kuteswa mpka wamtaje aliye wauzia na wenyewe hawamjui na wamesema hawajui lakini hawakuamini wala kuelewa wanaomba msamaha kwamba hatukujua Kama ni magendo sisi tumenunua tu, ili kupata ridhiki kidogo za familia lakini pia hawakuelewa mpka tunapoongea ndugu yetu yupo bombo hospitali sijui Kama atapona maana wanasema ameumia Sana kwa ndani na anapumulia oxygen.

Swali langu kwa TRA. Je, mamlaka ya kukamata watu na kutesa na kuwapiga wameitoa wapi au ndo wanavyofanya watu wakikamatwa na magendo nikupigwa mpka kufa, baada ya kupelekwa polisi wao wanawapiga na kuwatupa barabarani, hii ni sawa ndugu zangu?

Na hapo wamemwambia aende jumatatu kufata faini ya madungu yake na huku mtu yupo ICU hii ni sawa?

Mwingine wamempiga mpka wamemvunja mkono hii ni sawa kwenu TRA?
 
Hizo hips kwenye avatar ni zako mkuuu 😅
 
Aisee hii mbona ni hatari sana sema tamaa za kupata fedha za juu nazo mbaya sana
Ni kweli wanakosa Ni wangefata Sheria wsngepelekwa police na wangelipa faini kuliko walivyo wafanya je ikitokea wamepoteza maisha na mtu ana familia inamtegemea. Ni kosa ndio he Ni halali kwao kuua na kudhuru mtu
 
Sa hao TRA walimpiga wao kama akina nani!!!
Kama waliona kuna uvunjifu wa sheria si wangewapeleka idara husika!!
By the way walipaswa kukamata mzigo ambao uliowahusu tu,
Unayo haki ya kwenda kuwashitaki kwa walichokifanya
 
Katiba mpya!
 
Ila watz tuna nn hatupendi kufuata sheria tukikutwa na vimeo tunaanza lalamika. Hapo jirani Rwanda hadi shoe shine ana EFD MACHINE kosa upewe huduma usiombe risiti utajuta siku iyo. Fata sheria ua kubali kipigo. TRA ingekuwa jeshi kamili tuu ili tulipe kodi
 

Mamtu masomi ila mapumbavu, unampigia nini mtoto wa watu? Ila mwisho wao huwa wa mateso sana na majuto
 
Aisee,ingekua ni awamu ya tano yangeongelewa mpaka UN hayo,lakini kwa sababu ni awamu pendwa ya sita hutoweza kusikia kiumbe yeyote anayakemea zaidi watasema ni uongo wenye lengo la kuichafua serikali ya mtakatifu Hangaya.
 
Wenye mamlaka ya kufanya uchunguzi ndo walewale pesa mbele na wenye kufata maelekezo ata kabla ya uchunguzi
 
kama ni tra jambo hili ni la kufuatilia, ila isijekuwa ndugu yako kanunua mzigo wa wizi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…