Tella Mande
JF-Expert Member
- Jun 2, 2018
- 494
- 674
Kumekuwa na tabia sugu ya TRA kufanya kazi kama Trafiki wa Tz. Wanaamka, wanaweka kizuizi njiani eti wanakagua mapato ya malori. Mbaya zaidi kazi hiyo wanaifanya baada ya muda wazi, baada ya ofisi za TRA yenyewe kufungwa. Unapigiwa simu saa 3 usiku na dereva anakuambia TRA wanasema unadaiwa. Nipo Dar, amekamatiwa mikumi. Unaambiwa njoo na ushahidi kuwa hudaiwi !!
Kwanini kama mtu anadaiwa asiandikiwe barua ya wito akasuluhisha (reconcile) account yake.
Mtu akisema ni mitego ya rushwa atakuwa amekosea?
Halafu hata kama wamekosea wao, walikolaza gari nao wanataka kulipwa maegesho, tena hela ya ajabu, efu 75 kwa masaa 12. Wizi huu mpaka lini? Na risit hawatoi!!
Ningetamani kuwaona TRA wakikamata mchana ili mtu aweze kufika TRA lilipo file lake la kodi na kama ni deni basi awe amepewa barua ya wito zaidi ya mara 2 kama sheria na kanuni na busara zinavyoelekeza.
Wadau JE, na ninyi mmeyaona haya? Mnasemaje?
Kwanini kama mtu anadaiwa asiandikiwe barua ya wito akasuluhisha (reconcile) account yake.
Mtu akisema ni mitego ya rushwa atakuwa amekosea?
Halafu hata kama wamekosea wao, walikolaza gari nao wanataka kulipwa maegesho, tena hela ya ajabu, efu 75 kwa masaa 12. Wizi huu mpaka lini? Na risit hawatoi!!
Ningetamani kuwaona TRA wakikamata mchana ili mtu aweze kufika TRA lilipo file lake la kodi na kama ni deni basi awe amepewa barua ya wito zaidi ya mara 2 kama sheria na kanuni na busara zinavyoelekeza.
Wadau JE, na ninyi mmeyaona haya? Mnasemaje?