TRA kupiga mnada nyasi bandia za timu ya Simba kwa kushindwa kulipa kodi

Return Of Undertaker

JF-Expert Member
Jun 12, 2012
4,572
26,868
FB_IMG_1490866002999.jpg
FB_IMG_1490865992408.jpg
FB_IMG_1490866015109.jpg


Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imethibitisha kuwa nyasi bandia za klabu ya Simba zilizopo bandarini zitapigwa mnada endapo Simba watashindwa kulipa kodi wanayodaiwa.

Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi wa TRA, Richard Kayombo amesema Simba pia wananafasi ya kuzipata nyasi hizo endapo watalipa kabla ya tarehe ya mnada.

Kwa taarifa iliyotolewa na Makamu wa Rais wa Simba, Godfrey Nyange amesema “Ni kweli nyasi hizo zimezuiliwa na sababu ya kushindwa kulipia ushuru TRA pamoja na kuomba msamaha serikalini walikataa kufuta ushuru huo.”

Kwa upande wake Kampuni ya ya Udalali ya Majembe (Majembe Auction) wamesema kuwa watazipiga mnada endapo Simba watashindwa kulipa ushuru hadi kufikia tarehe ya mnada.

"Kampuni ya udalali ya Majembe Auction Mart inataka kupiga *mnada* nyasi bandia za SIMBA SPORTS CLUB na magoli yake, sababu kubwa ni uongozi (wamiliki) kushindwa kuzilipia *kodi*.

Mnada utafanyika Eneo la Nyuma ya "The Waterfront Sunset Restaurant and Beach Bar", barabara ya Yatch Club, Masaki, ofisi mnada utakaofanyika zinaitwa *LW9*.

Maoni ya mwandishi:

Kama hili litatokea leo basi ni simanzi si kwa Simba tu bali familia nzima ya soka nchini.

Kabla ya kuutupia lawama uongozi wa Simba SC kwa kushindwa kutafuta njia mbadala za kutafuta fedha za kulipa kodi za nyasi hizi? Serikali kwa wizara yenye dhamana ya michezo na shirikisho la soka nchini iliwapasa kuwasaidia Simba SC katika hili hata kwa mkopo au dhamana fulani katika ile sera ya kuendeleza michezo nchini.

Tukirudi kwa uongozi wa Simba kama mlifikia kukwama kiasi hiki , si mngepitisha bakuli kwa wanachama wenu na wadau wa soka nchini ?! Hili suala lisiwe la aibu maana hizi timu ni za wanachama hivyo wana dhamana na timu yao.

Lakini pia huu ni uwekezaji mkubwa kwa Simba SC katika suala la miundo mbinu hivyo lilipaswa kupewa kipaumbele kuliko jambo lolote ikiwa ni mara ya kwanza kwa timu hii kuthubutu kumiliki uwanja wake . Hizo milioni 800 za kutafutia ubingwa si mngewekeza huku???? Daaah
 
Msiwe na wasi wasi, Simba watafute hela ya Kaisari taratibu tu, nani atanunua nyasi bandia ikiwa hana matumizi nazo?

La pili hili ndio funzo kwa kina tantalila kuwa mabaya hayana mpaka. Imeshindikanwa nini serikali kuiachia Simba Koko majani yake (ukizingatia simba hali majani) halafu kodi ikakatwa kidogo kidogo.

Anyway, wauze tu, maana hata simba yenyewe bandia (kidding)
 
View attachment 488763 View attachment 488761 View attachment 488759

"Kampuni ya udalali ya Majembe Auction Mart inataka kupiga *mnada* nyasi bandia za SIMBA SPORTS CLUB na magoli yake, sababu kubwa ni uongozi (wamiliki) kushindwa kuzilipia *kodi*.
Mnada utafanyika siku ya:
Alhamisi 30/03/2017.
Eneo:Nyuma ya "The Waterfront Sunset Restaurant and Beach Bar", barabara ya Yatch Club, Masaki, ofisi mnada utakaofanyika zinaitwa *LW9*

Maoni ya mwandishi:

Kama hili litatokea leo basi ni simanzi si kwa Simba tu bali familia nzima ya soka nchini.

Kabla ya kuutupia lawama uongozi wa Simba SC kwa kushindwa kutafuta njia mbadala za kutafuta fedha za kulipa kodi za nyasi hizi? Serikali kwa wizara yenye dhamana ya michezo na shirikisho la soka nchini iliwapasa kuwasaidia Simba SC katika hili hata kwa mkopo au dhamana fulani katika ile sera ya kuendeleza michezo nchini.

Tukirudi kwa uongozi wa Simba kama mlifikia kukwama kiasi hiki , si mngepitisha bakuli kwa wanachama wenu na wadau wa soka nchini ?! Hili suala lisiwe la aibu maana hizi timu ni za wanachama hivyo wana dhamana na timu yao.

Lakini pia huu ni uwekezaji mkubwa kwa Simba SC katika suala la miundo mbinu hivyo lilipaswa kupewa kipaumbele kuliko jambo lolote ikiwa ni mara ya kwanza kwa timu hii kuthubutu kumiliki uwanja wake . Hizo milioni 800 za kutafutia ubingwa si mngewekeza huku???? Daaah
Kwani TRA na serikali hawawezi kuwaive kodi kwa hizo products zitakazopromote mpira nchini????? Duh ama kweli hapendwi mtu pochi tu!!!!!
 
Naomba kueleweshwa hizo nyasi ng'ombe wanaweza kula? Huku kwetu kuna njaa ng'ombe hawana malisho kabisa.

Anyway, kwani zinadaiwa shilingi ngapi namie nichangie kidogo.
 
Nani atanunua nyasi! Labda kama wameamua kuzunguka ili wazimiliki wenyewe. Huwezi kuinua mpira kwa kuhitaji kodi kwenye vifaa vya michezo.Hili swala Mwakyembe aliingilie maana tutaendelea kuwa kichwa cha mwehu.
 
Hivi hizi nyasi ilikua ziwekwe wapi? Maana sijawai sikia wakijenga uwanja.
Ilikuwa ziwekwe bunju kwenye uwanjawao walishaanza kuujenga na walianza sehemu ya kuchezea ambapo pamebakia kuwekwa nyasi tu mambo mengine yote Tayari.
Ila juzi nilimsikia mwenyekiti wa kamati ya ujenzi akisema hapewi ushirikiano n'a uongozi kwakuwa amezidiwa hoja n'a wale wanaosema timu itumie Nguvu zote kwa ajili ya ubingwa
Kwahiyo Simba wameweka Bakari ya 800m ils ipate ubingwa wa ligi ambayo zawadi yake hâta 200m sijui kama zinafika.
Ujinga mtupu kwenye soka la bongo unawezaje kuagiza kama huna kodi ? Si zitapigwa manda !!!!!!? Acha ziuzwe.
 
Back
Top Bottom