kingadvisor
Senior Member
- Dec 21, 2011
- 109
- 30
Wachimbaji wengi wadogo miaka nenda rudi wawe wachimba Tanzanite mererani au dhahabu popote wamekuwa hawalipi kodi kwa kisingizio kuwa hawapati kitu wakati pembeni wanatamba wanapata mabilioni.Kutolipa kodi kwao ndiko kunaifanya serikali itafute wageni wafanye uchimbaji mkubwa kwenye hayo maeneo ya wachimbaji wadogo ili serikali ipate chochote.
Wachimaji toka nje wakubwa wakishaanza kuchimba ndipo siri zinaanza kufichuka wachimbaji wadogo wanaanza kulalama kuwa wageni wanabeba mabilioni ya madini na kuacha wazawa hoi.Lakini kabla walikuwa wanajifanya hapo wanapochimba wanahangaika tu hamna kitu.
Dawa ni machimbo ya wachimbaji wadogo yakianza tu TRA ihamishie makao makuu hapo na wawambie kama hamtalipa kodi tunaenda ishauri serikali iwaondoe aje mwekezaji atakayelipa kodi.wawaambie kwanza mnapoteza muda tu kwenye hayo machimbo kama hampati kitu fungeni virago mkafanye shughuli zingine.
Sehemu kubwa kwenye machimbo waliko wawekezaji kulikuwa na weusi kibao wazawa wa nchi hii wanachimba miaka nenda rudi lakini uzalendo wa kulipa kodi hawana huku wakiwa wakali kwenye kudai huduma za jamii wapelekewe na serikali kwa kodi zinazokusanywa sehemu nyingine.
Kama tunataka maendeleo wachimba madini wanaoitwa wadogo wabanwe nao kuna mabilioni kule wanapata wakisema hawapati tafuta FFU jaribu kuwatimua uone vita yake ya kukataa kutoka ndipo utajua serikali inavyoibiwa kodi na hao maruhuni wanaojiita wachimbaji wadogo.
kingadvisor@yahoo.com
Wachimaji toka nje wakubwa wakishaanza kuchimba ndipo siri zinaanza kufichuka wachimbaji wadogo wanaanza kulalama kuwa wageni wanabeba mabilioni ya madini na kuacha wazawa hoi.Lakini kabla walikuwa wanajifanya hapo wanapochimba wanahangaika tu hamna kitu.
Dawa ni machimbo ya wachimbaji wadogo yakianza tu TRA ihamishie makao makuu hapo na wawambie kama hamtalipa kodi tunaenda ishauri serikali iwaondoe aje mwekezaji atakayelipa kodi.wawaambie kwanza mnapoteza muda tu kwenye hayo machimbo kama hampati kitu fungeni virago mkafanye shughuli zingine.
Sehemu kubwa kwenye machimbo waliko wawekezaji kulikuwa na weusi kibao wazawa wa nchi hii wanachimba miaka nenda rudi lakini uzalendo wa kulipa kodi hawana huku wakiwa wakali kwenye kudai huduma za jamii wapelekewe na serikali kwa kodi zinazokusanywa sehemu nyingine.
Kama tunataka maendeleo wachimba madini wanaoitwa wadogo wabanwe nao kuna mabilioni kule wanapata wakisema hawapati tafuta FFU jaribu kuwatimua uone vita yake ya kukataa kutoka ndipo utajua serikali inavyoibiwa kodi na hao maruhuni wanaojiita wachimbaji wadogo.
kingadvisor@yahoo.com