white wizard
JF-Expert Member
- May 18, 2011
- 8,618
- 13,890
Jana nimekwenda ofisi ya TRA, kwa ajili ya kukata TIN, nafika nakutana na mkadiliaji kodi, ana kadiria kodi ninayotakiwa kuilipa, nakubaliana nayo tena kwa kuvutana kweli, Ngoma ikaja anataka mkataba wa pango, nikampa anasema kuwa eti hiyo kodi ya pango ambayo kwa mwaka ni 1.2 milioni, natakiwa nilipe asilimia 10!!!! Ambayo ni 120,000!! Nikamwambia mimi hiyo pesa nimemlipa mwenye nyumba na yeye ndio anatakiwa kulipa kodi kwenye pesa hiyo sio mimi tena nimlipie?? Anasema eti kwa wenye nyumba imekuwa ngumu kulipa kodi hiyo, hivyo mi ndio nilipe kisha nikamwambie mwenye nyumba anirudishie!! Jamani huu si uhuni, serikali inaogopa kukusanya kodi hiyo toka kwake mi ndio niwakusanyie?? Tumebishana sana nikaona ngoja niondoke zangu kwani naweza leta balaa jingine tena nikampa sifa MGONJA!!! Kweli hii nchi ni shidaaa!!! Wanashindwa kukusanya kodi huko IPTL, Sisi ndio watukamue, haya mambo ndio yanasababisha mtu akwepe kulipa kodi kabisa !!! Hata hicho kidogo kinakosekana kabisa!! Kwani hii sheria imekaaje na mbona huko nyuma haikuwepo??? Yaani mapato amepata mwenye nyumba kodi nilipe mimi jamani!!!! Kisa wenye nyumba huwa hawakubali wanapofuatwa na mamlaka ya kodi!!!