sammosses
JF-Expert Member
- Jan 24, 2011
- 1,734
- 1,150
Ibara ya 8 -,(1) ya katiba ya Jamhuri ya Muungano inasema (b) lengo kuu la serikali litakuwa ni ustawi kwa wananchi wake.
Kwa kuzingatia hili hapo juu katika kustawisha wananchi wake, serikali imeona umuhimu wa kuwatambua wananchi wake kwa utambulisho wa kupitia kitambulicho cha utaifa (national identity).
Zoezi hili limeratibiwa na NIDA na limeibua upungufu mkubwa sana kiutendaji kutokana na kukosa ufanisi, ambao wa kulaumiwa ni serikali.
Pamoja na Bunge kutenga bajeti ya kukamilisha zoezi la kusajili vitambulisho hivi, bado Watanzania wengi hawana vitambulisho hivi, pamoja na kuwa bajeti yake ilipangwa.
Hii ni kiashiria kingine cha harufu ya ufisadi kwenye zoezi zima.
Leo badala ya kuzungumzia vitambulisho, Watanzania wana hangaika kutafuta namba za vitambulisho vyao toka NIDA, vitambulisho ambavyo utaratibu wake na structure yake hautofautiana na vitambulisho vya mpiga kura.
Ikiwa zoezi la upatikanaji vitambulisho vya mpiga kura lilifanyika na watu kuondoka na vitambulisho vyao, hili la vitambulisho vya Taifa lilipata ukakasi gani.
Wapo Watanzania wengi hawana vitambulisho hivi kutokana na ukiritimba ulio sababishwa na NIDA, lakini kwanini sasa serikali kabla haijafikiria kutekeleza zoezi la usajili wa laini za simu kwa alama za vidole, lisinge kuwa na haraka kuhakikisha ugawaji wa vitambulisho hivi unapatiwa uvumbuzi wa haraka kuliko kuwashughulisha wananchi kuhangaikia namba za vitambulisho vyao ilihali hawana vitambulisho hivi.
Hii ni sawa na kumuuzia mfugaji kamba ya kumfungia mbuzi, ukimuaminisha mbuzi atazaliwa muda si mrefu.
Kwa kuzuia udhaifu wa zoezi zima la usajili usionekane, serikali kupitia NIDA kwa ushirika wa TCRA imeanzisha biashara ya tozo mpya ya 100/- kusaka namba za kitambulisho cha utaifa, kitambulisho ambacho bado kipo kwenye mikono yao,kwa kuanzisha zoezi la usajili mpya wa laini za simu kwa alama za vidole.
Imeelekezwa na serikali ukitaka kupata Namba ya kitambulisho chako cha utaifa piga namba *152*00# hapo utakutana na maelekezo jinsi ya kupata namba yako toka NIDA kwa gharama ya 100/- kupitia mpesa, tigopesa na makampuni mengine ya simu yenye huduma kama hiyo.
Lakini ndani ya sekunde zisizo 20s utapata majibu ya makato ya fedha 100/- yakiambatana na ujumbe wa aina mbili, ujumbe wa risiti ya serikali ya muamala ulioufanya na ujumbe unao kutaarifu kuwa taarifa zako hazipatikani.
Huu ni uhuni usiokubalika kwa walipa kodi kuwatoza tozo wakati kodi yao ndiyo iliyo tumika kuratibu zoezi zima, hii ni biashara mpya isiyo rasmi na hatujui ni sheria ipi iliyopitishwa na bunge kuruhusu yanayo fanyika sasa.
Hebu fikiri kwa kina;
Watanzania mathalani milioni 1 wanamiliki laini za simu labda kwa kampuni ya vodacom,ukiwatoza 100/- maanake ni kwamba;
Watu 1,000,000 * 100/- = 100,000,000/-
Hizi zinaingia kwenye mfuko wa serikali, lakini hatuambiwi zinawekwa kwenye fungu gani kwa mujibu wa sheria ya makusanyo.
Serikali itueleze ni kwanini imeamua kutuletea biashara isiyo rasmi ya kupata taarifa zisizo andaliwa wakati ikitutoza fedha, tukisema huu ni uhuni au ufisadi tutakuwa tumekosea!!!
Serikali iache kutuumiza wananchi kununua huduma zisizo julikana kwa mgongo wa kusajili laini ikiwa utaratibu wa vitambulisho haujakidhi malengo.
Tuamke, hiki ni kizazi cha kuhoji, tutahoji mpaka dakika ya mwisho.
Kwa kuzingatia hili hapo juu katika kustawisha wananchi wake, serikali imeona umuhimu wa kuwatambua wananchi wake kwa utambulisho wa kupitia kitambulicho cha utaifa (national identity).
Zoezi hili limeratibiwa na NIDA na limeibua upungufu mkubwa sana kiutendaji kutokana na kukosa ufanisi, ambao wa kulaumiwa ni serikali.
Pamoja na Bunge kutenga bajeti ya kukamilisha zoezi la kusajili vitambulisho hivi, bado Watanzania wengi hawana vitambulisho hivi, pamoja na kuwa bajeti yake ilipangwa.
Hii ni kiashiria kingine cha harufu ya ufisadi kwenye zoezi zima.
Leo badala ya kuzungumzia vitambulisho, Watanzania wana hangaika kutafuta namba za vitambulisho vyao toka NIDA, vitambulisho ambavyo utaratibu wake na structure yake hautofautiana na vitambulisho vya mpiga kura.
Ikiwa zoezi la upatikanaji vitambulisho vya mpiga kura lilifanyika na watu kuondoka na vitambulisho vyao, hili la vitambulisho vya Taifa lilipata ukakasi gani.
Wapo Watanzania wengi hawana vitambulisho hivi kutokana na ukiritimba ulio sababishwa na NIDA, lakini kwanini sasa serikali kabla haijafikiria kutekeleza zoezi la usajili wa laini za simu kwa alama za vidole, lisinge kuwa na haraka kuhakikisha ugawaji wa vitambulisho hivi unapatiwa uvumbuzi wa haraka kuliko kuwashughulisha wananchi kuhangaikia namba za vitambulisho vyao ilihali hawana vitambulisho hivi.
Hii ni sawa na kumuuzia mfugaji kamba ya kumfungia mbuzi, ukimuaminisha mbuzi atazaliwa muda si mrefu.
Kwa kuzuia udhaifu wa zoezi zima la usajili usionekane, serikali kupitia NIDA kwa ushirika wa TCRA imeanzisha biashara ya tozo mpya ya 100/- kusaka namba za kitambulisho cha utaifa, kitambulisho ambacho bado kipo kwenye mikono yao,kwa kuanzisha zoezi la usajili mpya wa laini za simu kwa alama za vidole.
Imeelekezwa na serikali ukitaka kupata Namba ya kitambulisho chako cha utaifa piga namba *152*00# hapo utakutana na maelekezo jinsi ya kupata namba yako toka NIDA kwa gharama ya 100/- kupitia mpesa, tigopesa na makampuni mengine ya simu yenye huduma kama hiyo.
Lakini ndani ya sekunde zisizo 20s utapata majibu ya makato ya fedha 100/- yakiambatana na ujumbe wa aina mbili, ujumbe wa risiti ya serikali ya muamala ulioufanya na ujumbe unao kutaarifu kuwa taarifa zako hazipatikani.
Huu ni uhuni usiokubalika kwa walipa kodi kuwatoza tozo wakati kodi yao ndiyo iliyo tumika kuratibu zoezi zima, hii ni biashara mpya isiyo rasmi na hatujui ni sheria ipi iliyopitishwa na bunge kuruhusu yanayo fanyika sasa.
Hebu fikiri kwa kina;
Watanzania mathalani milioni 1 wanamiliki laini za simu labda kwa kampuni ya vodacom,ukiwatoza 100/- maanake ni kwamba;
Watu 1,000,000 * 100/- = 100,000,000/-
Hizi zinaingia kwenye mfuko wa serikali, lakini hatuambiwi zinawekwa kwenye fungu gani kwa mujibu wa sheria ya makusanyo.
Serikali itueleze ni kwanini imeamua kutuletea biashara isiyo rasmi ya kupata taarifa zisizo andaliwa wakati ikitutoza fedha, tukisema huu ni uhuni au ufisadi tutakuwa tumekosea!!!
Serikali iache kutuumiza wananchi kununua huduma zisizo julikana kwa mgongo wa kusajili laini ikiwa utaratibu wa vitambulisho haujakidhi malengo.
Tuamke, hiki ni kizazi cha kuhoji, tutahoji mpaka dakika ya mwisho.