Tozo ya kodi za simu ni janja ya nyani

Tozo ya kodi za simu ni janja ya nyani

TOMEE

JF-Expert Member
Joined
Sep 17, 2013
Posts
588
Reaction score
118
Ndugu zanguni swala la tozo ya kodi za simu limeibuka tena baada ya TRA kutaka makampuni ya simu kuanza kukata elfu moja kwa kila line ya simu kwa mwezi,swali nalokuja kujiuliza ni hili,tuliambiwa haya makato ni kwa ajili ya kuweka umeme vijijini,sasa je umeme utawekwa kwenye nymba za nyasi,hivi hamuoni kuwa hizi fedha wanataka kukusanya kwa ajili ya kampeni 2015?

NAWASILISHA
 
Harafu kuweka umeme kwa nyumba lazima ulipie pia hiyo miradi wamesema inafadhiliwa na marekani
 
Ndugu zanguni swala la tozo ya kodi za simu limeibuka tena baada ya TRA kutaka makampuni ya simu kuanza kukata elfu moja kwa kila line ya simu kwa mwezi,swali nalokuja kujiuliza ni hili,tuliambiwa haya makato ni kwa ajili ya kuweka umeme vijijini,sasa je umeme utawekwa kwenye nymba za nyasi,hivi hamuoni kuwa hizi fedha wanataka kukusanya kwa ajili ya kampeni 2015?NAWASILISHA

Ni kwamba TRA imeandika barua kwa makampuni ya simu kukata pesa kuanzia mwezi July, August na September kwa mantiki hiyo wewe mleta uzi unadaiwa elfu 3000 na buku la mwezi huu wa kumi..jumla elfu 4! kazi ni kwako,..hayo ndio mammbo ya serikali yenu "sikivu"
 
Umeme na simu vinahusianaje? Hizo bajeti zinazopitisha na serikali sikivu ya CCM uoande wa REA zinafanya nini?
Kweli hadi 2015 ifike tutaona mengi.
 
Ni kwamba TRA imeandika barua kwa makampuni ya simu kukata pesa kuanzia mwezi July, August na September kwa mantiki hiyo wewe mleta uzi unadaiwa elfu 3000 na buku la mwezi huu wa kumi..jumla elfu 4! kazi ni kwako,..hayo ndio mammbo ya serikali yenu "sikivu"

sio 3000 tu nina laini tatu so 9000 alafu wanatuambia maisha bora nina hasira sana na miccm
 
Hili suala la Kodi za simu linavyofanywa na Serikali kupitia TRA ni wizi Mtupu, Kwa takwimu nilizonazo zaidi ya Asilimia 45% ya Watanzania watakatiwa Simu zao. Walikuwa wapi wamesubiri miei mitatu imepita wanataka wakate zote. Niliona taarifa iliyotolewa na kampuni za simu ilisema zaidi ya Watumiaji wa simu milioni 8 hawana uwezo wa kuweka shilingi elfu 1000 kwa mwezi. Au kuna kamradi ka mtu kamekwama.

Sijui kwa nini Serikali hii imekosa huruma kwa wananchi wake, Inauma sana, Maisha ni Magumu sana sasa wanatuongezea mizigo mingine, Kampuni za simu zenyewe zimeona hatuwezi kupiga simu kwa umasikini mkubwa tulionao wameleta vi ofa vya kutuwezesha angalau kuzungumza its Sad wao wanataka tena watukate.

Ninaumia sana.
 
Ndugu zanguni swala la tozo ya kodi za simu limeibuka tena baada ya TRA kutaka makampuni ya simu kuanza kukata elfu moja kwa kila line ya simu kwa mwezi,swali nalokuja kujiuliza ni hili,tuliambiwa haya makato ni kwa ajili ya kuweka umeme vijijini,sasa je umeme utawekwa kwenye nymba za nyasi,hivi hamuoni kuwa hizi fedha wanataka kukusanya kwa ajili ya kampeni 2015?NAWASILISHA

Subiri ujibiwe mbona pub nyingi ni za nyasi?
 
Hili suala la Kodi za simu linavyofanywa na Serikali kupitia TRA ni wizi Mtupu, Kwa takwimu nilizonazo zaidi ya Asilimia 45% ya Watanzania watakatiwa Simu zao. ..................

.

Kila mahali kodi. Chochote nachonunua kama mkate, sabuni nk vinakatwa kodi (18% VAT), mshahara unakatwa kodi kubwa, maji wanakata kodi, hata nikinunua umeme wanakata 22%, kila kitu ni lazima kikatwe kodi, sasa wamehamia kwenye laini za simu.

Lakini nimeshazoea, naishi kwa amani sababu ndio maisha waliyoyataka Watanzania wengi, nawasikitikia wale waliokuwa na imani ya maisha bora waliyoahidiwa sasa wamegundua maisha bora hakuna.
 
Serikali yetu ni ya ajabu wakati mwingine. Kuna kodi nyingi sana Tanzania, cha ajabu kabla hatujafikia uwezo wa kukusanya zote kwa ufanisi tunaongeza na nyingine. Ukitazama vizuri unaweza kujikuta unalipa kodi kibao bila sababu za msingi. Uliponunua simu ulilipa kodi, ukinunua laini kodi, ukinunua vocha kodi, ukiongea, ukasurf au ukatuma text kodi. Hapo ni simu tu kodi zote hizo mtu mmoja. Kwa mahesabu rahisi kipindi chote utachomiliki simu utakuwa umelipa kodi sawa na 60% ya huduma uliyopata.
 
Mpaka tugonge 2015 hakika majanga yatakuwa kedekede!

Halafu bado tuna Imani na serikali iliyoko madarakani.
Nina swali............Hivi haya makampuni ya simu huwa hawalipagi kodi serikalini? Kwani sasa tukiwa kama wateja wao watukate pesa zote hizo ingali bado wao ndiyo wanatuuzia vocha na laini zao? Ama ni kwamba serikali inaona yakwamba kila mwenye simu ana uwezo?

Kuna haja ya kuangaliwa hili kwa jicho la pili tena.

Hao ndio mafisadi bhana!
 
kwanini makali haya yachamie kwny madini?? wavuna mbao, wawindaji wenye vbali coz huko kuna prsa zetu nyingi sana aisee znapotea!! iv kweli kabisa tunaweza kukaa chini na kujipongeza et mrahaba wa serikali kataka sekta ya madini ni asilimia 3 hizo 97 znaenda wapi?? na madini yanaisha?! nchi zinazozalisha mafuta muwezkezaji huacha 60% kwa serikali yeye akiambulia 40%!! dah Tanzania unaenda wapi Tanzania nambie nijue basi kila cku naumia mm wanakula wengine!!!!
 
Back
Top Bottom