Toyota yazidi kuboresha magari yenye uwezo wa kutumia mafuta au umeme (Hybrid)!

muvika online

JF-Expert Member
Nov 27, 2016
375
283
Makampuni mengi yanazidi kuwekeza katika teknolojia za magari rafiki wa mazingira. Toyota inazidi kuwekeza pia na inategemea moja ya gari zuri na la kisasa zaidi kutoka kwao la Toyota Prius PHV litafanya vizuri sana sokoni.

toyota_prius_phv_1-1024x559.jpeg


Gari la Toyota Prius PHV limeingia sokoni wiki hii nchini Japani, kwa nchini Marekani gari hilo linauzwa kwa jina la Prius Prime na lilianza kuuzwa mwishoni mwa mwaka jana.

Toyota Prius PHV ni gari lenye uwezo wa kutumia mafuta na pia umeme wa kuchaji. Kati ya teknolojia bora za kipekee kwa gari hilo ni pamoja na uwezo wa mtumiaji kuweza kulichaji kwa kutumia umeme wa nyumbani tuu, hii ni tofauti na magari ya umeme kutoka kampuni ya Tesla ambayo yanaitaji kuchajiwa kwenye vituo vyao spesheli.

toyota-prious-phv.jpg


Toyota wanategemea kuuza zaidi ya magari 2,500 kwa mwezi ya toleo la Prious PHV nchini Japani, gari hilo litaanza kupatikana katika masoko mengine duniani kote
Dereva anaweza kuendesha hadi umbali wa kilometa 68.2 kwa kutumia umeme wa betri la gari hilo, hii ni takribani mara tano zaidi ukilinganisha na toleo la zamani la gari hilo (lilikuwa na uwezo wa kwenda umbali wa km 26.4).

Pia kingine kikubwa ni kwamba gari hilo linachukua muda mchache kujaa chaji – takribani masaa 2 na dakika 20 kujaa kwenye chanzo cha umeme wa volti 200, wakati kwenye chanzo cha umeme wa volti 100 itachukua masaa 14.

Ila kama ukitumia mashine yake spesheli ya kuchajia kiwango cha chaji kitaongezeka kutoka 0 hadi asilimia 80 ndani ya dakika 200 tuu.

Toyota wanaamini hadi kufikia mwaka 2050 asilimia kubwa ya magari yatakayokuwa barabarani yatakuwa yanatumia teknolojia flani rafiki kwa mazingira.
 
Nadhani mpaka muda likiingizwa be forward, Japan watakuwa wameanza kutumia gari zinazojiendesha zenyewe.
Fukk the Gov. kwa kutukomesha na kodi kubwa za magari hapa bongo.
 
magari ya umeme yapo mengi sana tatizo kubwa ni mashine hizo za kuchagia pindi yanapoisha chaji? magari mengi ya umeme mm nimekutana nayo hayawaki na ukipima au ukifuatilkia tatizo kubwa ni betri za HIGH VOLTAGE kutokuwa na umeme wa kutosha na tatizo kubwa ni wapi au vipi utalichaji
 
magari ya umeme yapo mengi sana tatizo kubwa ni mashine hizo za kuchagia pindi yanapoisha chaji? magari mengi ya umeme mm nimekutana nayo hayawaki na ukipima au ukifuatilkia tatizo kubwa ni betri za HIGH VOLTAGE kutokuwa na umeme wa kutosha na tatizo kubwa ni wapi au vipi utalichaji
Hii nayo yaweza kuwa fursa kwa wale wenye mipunga mirefu. Ni kuingia mikataba na sheli tu na kufungua hizo charging points.
 
Atakayekuja kuteka soko ni atakayetengeneza gari litakalotumia umeme wa jua.
 
Atakayekuja kuteka soko ni atakayetengeneza gari litakalotumia umeme wa jua.
MBONA ZIPO MKUU ZINA PANEL KWA JUU mfano hizo hybrid kuna zingine zinatumia mafuta na umeme na charg ikipunguwa inajichaji kwa jua kuna kuwa na panel juu ya gari
 
Sisi hata kutengeneza miradi ya maji tunamtegemea yule jamaa aliyepokwa passport. Hapa tunajitoa ufahamu kuwaponda TOYOTA
 
Back
Top Bottom