chotarasukari
Senior Member
- Jan 6, 2013
- 110
- 23
Sio lazima usomee PCM and PGM hili usome computer science. Mwanafunzi anaweza kutoka O level na kwenda moja kwa moja kuchukua degree yoyote ikiwemo ya computer science.
Kuwa na PCM au PGM ni criteria zilizowekwa na UDSM na vyuo vya Tanzania. Lakini sio muhimu katika masomo ya computer science.
Kuhusiana na maana ya degree zenyewe. Zamani kulikuwa hakuna degree ya computer science. Mpaka sasa pioneers wa computer science ni watu waliosomea electrical engineering, mathematics, material science and physics. Kwa miaka mingi ilikuwa ni sehemu ya department ya Electrical Engineering or Mathematics. Mwishoni mwa miaka ya 80 na mwanzoni 90 kulikuwa na ongezeko kubwa la matumizi computers na mahitaji ya wataalamu yaliongezeka. Hivyo vyuo vingi vilianzisha department ya computer science kupata wataalamu na watafiti.
Katika miaka ya 90 matumizi ya computer na telecommunication yaliongezeka zaidi na kwenye fani mbalimbali. Na vilevile kukaanza kutokea wataalamu wa matumizi ya computer katika fani hizo. Huu ndio ujio wa IT. Hivyo mtu kuwa mtaalamu wa IT sio lazima awe amebobea sana kwenye maths. Inategemea anatumia applications za computer kwenye masuala gani. Matokeo ya utafiti yaliyofanyika miaka ya nyuma yamefanya matumizi ya applications za computer kuwa user friendly.
Kuhusiana na Software Engineering, hii inahusiana na development ya software. Miaka ya zamani computer programmers walikuwa wana-develop programs au applications kwa kufuata utaratibu waliojipangia. Hii ilisababisha gharama za ku-maintain na ku-develop software kuwa kubwa na process kuwa unpredicatability. Hivyo wataalamu wakaamua kutumia mbinu zinazotumika kwenye fields zingine za engineering kuboresha development of software. Kwa mfano kwenye utengenezaji wa magari kuna designer, kuna mechanical engineer, kuna interior designer na watu wengine. Watu hawa wanafanya kazi katika sehemu tofauti na kwa vipindi tofauti lakini wanakuletea kitu cha mwisho chenye kueleweka kwa sababu wanatumia proven methodologies kupata matokeo.
Hivyo kuwa software engineer sio lazima usomee software engineer. Ukiwa unashiriki katika sehemu muhimu za software development life cycle na kufuata proven methodologies, wewe tayari ni software engineer.
Kuna mtu kagusia informatics. Ukiondoa UK, Ireland and Scotland, nchi nyingi za Ulaya zinatumia informatics kama computer science. Wanaosomea wanachukua masomo yote ya computer science.
Kuhusiana na computer engineering, hapa inahusiana na mambo ya computer hardware. Na vilevile wanaochukua CE wanachukua masomo mengi ya computer science.
Kwa ujumla wenye mafanikio mazuri kwenye masuala ya computer ni wale wenye kutumia vipaji na wenye passion. Kuwa na degree inakupa profile tu lakini haikusaidii kama huna talents na passion.
Wenu
Z-10
Nimekuelewa sana kwa maelezo yako. vip upande wa networking hesabu lazima uijue?
Nimekuelewa sana. (mimi napenda sana nisome Networking) je itakua na faida kwangu hata kwa upande wa salary?. kama nikifanya ccnaChotarasukari;
Katika miaka 10 20 iliyopita utafiti mkubwa ulifanyika kufanya matumizi ya computer kuwa user friendly. Network za sasa ni user friendly. Hivyo mtu yoyote anaweza kujifunza au kufanyia administration networks bila kuwa mkali wa hesabu.
Research zinaendelea kufanya network smarter. Hivyo muda si mrefu, network administration will be a dying profession.
Huwezi kusomea software eng Tanzania kwa sasa thats why kuna IT instead! Ndo maana vyuo vya serikali havitoi hiyo software engineering because kwa soko la sasa la ajira Tanzania itakuwa useless.
So kwa watakao soma BIT nw wanauwezo wa kufanya kazi za IT pia na za mambo
Yanayo husiana na accnts
Inaonekana umeingia mahali uka select all kisha copy then uka paste Mzigo kama ulivyo!
Nitafute nikupe modem na laptop na tuition ya ku google bila makato yoyote.
Mimi niliwai kwenda IFM mwaka 2009 wakati nataka nisome IT na wakati huo nilkuwa tayar nimechukua form UDSM na niliambiwa unatakiwa uwe umesoma sayansi "O" au "A" Level. na pia kinaenda TCU kwa uchunguzi zaidi ndo nikapewa full details. QM uwezi fananisha na Mathematics za mlimani za watu wa Computer na Telecom. Nasema hv coz nlkuwa naona na nimemfundsha m2 wa IFM 2010 tukiwa hostel kijitonyamaSio kweli... IFM ili mtu usome computer science au IT Math ni somo la lazima na uwe umefaulj pia lazima uwe umesoma pure science subjects bila hivyo labda uwe umeanza certificate ukaja diploma ndo ukaingia degree. Bila hesabu hayo masomo hayaendi. Kuna binary caliculation Quantitative mathematics na mengine so usidanganye mtu yoyote kua maths si la lazima
Ni kweli tuna mfumo wa elimu usio mzurni na bahati mbaya wanasiasa wanazidi kuuharibu. Lakini hii haimpi uhalali wa yeye kutudharau Watanzania (na sio mfumo wa Tanzania). Ninawajua watu wazuri katika fani hii kupita huyu ndugu na nin hakika tukiweka challenge watamtoa knock out.
Tuwasiliane ili nijue uko wapi kwanza au nikupe nikuonyeshe nilichokifanya na ww unioshe pia! Hamna mtu anadharau ila bongo tunapenda kuona tunaweza kitu ambacho hakiwezekani! Mimi sisomi nje ila nina ishi nje na ntafanya kazi nje so sidharau kitu,mtu wala nchi ila kwa upeo wangu mdogo kama unavyowaz/fikiria Tanzania kutoa wahitimu wa Software engineering kwa sasa ni useless ntasimamia hoja yangu kwani naelewa nachokisema.:bored::bored::cell:
Baada ya kuonekana kuwa department ya it ktk makampuni na mashirika mengi imekuwa kama mzigo (nnaposema mzigo ni kuwa haizalishi..wafanyakazi wengi wa IT katika maofisi mengi wamekuwa wakisubiri computer kuharibika watengeneze,(makampuni mengine wao wanatupa tu computer) au kucheza na server na mambo yanayohusu computer kwa ujumla hivyo kuifanya department ya IT kuwa na matumizi makubwa sana)
Hivyo basi baada ya kuliona hilo ndio wakaamua IT iwe BIT (business information technology)....ili hii department ya It iwe inazalisha pia au kusaidia kuzalisha na si kulishwa tu...ukiangalia nchi zilizoendelea hakuna tena course ya IT bila ya business....nadhani hata vyuo vya Tanzania navyo vitaanza(kama havijaanza maana sina hakika)
Nimekuelewa sana kwa maelezo yako. vip upande wa networking hesabu lazima uijue?
Sio kweli... IFM ili mtu usome computer science au IT Math ni somo la lazima na uwe umefaulj pia lazima uwe umesoma pure science subjects bila hivyo labda uwe umeanza certificate ukaja diploma ndo ukaingia degree. Bila hesabu hayo masomo hayaendi. Kuna binary caliculation Quantitative mathematics na mengine so usidanganye mtu yoyote kua maths si la lazima