herikipaji
JF-Expert Member
- Aug 23, 2016
- 1,198
- 1,345
Hivi kuna tofauti gani kubwa kati ya vyama hivi vya siasa kati ya CCM na CHADEMA?
Hapa tuwapime kwa maneno na matendo yao wanachokiamini na kukisimamia kwa misingi ya itikadi, falsafa na ajenda kubwa wanazozifuata ili kutimiza malengo na kuhakikisha vyama hivyo vinaleta tija kwa jamii na taifa.
CCM wana ajenda ipi kwa sasa, na CHADEMA je?
Katiba za vyama hivi kuna mengi mazuri yameandikwa lakini je wanayasimamia na kuyaishi?
Mie binafsi nimejaribu kufanya uchunguzi wa kina na nikahitimisha kuwa hivi vyama CCM na CHADEMA ipo tofauti moja tu kubwa ni kuwa CCM wana tawala nchi kwa sasa tena utawala wa kidhalimu tu[Siyo kuongoza], na CHADEMA bado hawajafankiwa kupata nafasi ya madaraka makubwa.
Lakini CHADEMA ni kama CCM tu wanafanana wote ni WACHUMIA TUMBO tu.
Sasa raia wafanye nini kama wote ni wachumia tumbo!
Jibu: Mateso hayatoisha kwa watawaliwa hadi watawaliwa wenyewe waamue kuwadhibiti watawala dhalimu->hii haijalishi nani au chama gani kinatawala binadamu akipata mamlaka lazima adhibitiwe usipofanya hivyo utakiona cha mtema kuni.
Nini mtazamo wako na wewe?
Hapa tuwapime kwa maneno na matendo yao wanachokiamini na kukisimamia kwa misingi ya itikadi, falsafa na ajenda kubwa wanazozifuata ili kutimiza malengo na kuhakikisha vyama hivyo vinaleta tija kwa jamii na taifa.
CCM wana ajenda ipi kwa sasa, na CHADEMA je?
Katiba za vyama hivi kuna mengi mazuri yameandikwa lakini je wanayasimamia na kuyaishi?
Mie binafsi nimejaribu kufanya uchunguzi wa kina na nikahitimisha kuwa hivi vyama CCM na CHADEMA ipo tofauti moja tu kubwa ni kuwa CCM wana tawala nchi kwa sasa tena utawala wa kidhalimu tu[Siyo kuongoza], na CHADEMA bado hawajafankiwa kupata nafasi ya madaraka makubwa.
Lakini CHADEMA ni kama CCM tu wanafanana wote ni WACHUMIA TUMBO tu.
Sasa raia wafanye nini kama wote ni wachumia tumbo!
Jibu: Mateso hayatoisha kwa watawaliwa hadi watawaliwa wenyewe waamue kuwadhibiti watawala dhalimu->hii haijalishi nani au chama gani kinatawala binadamu akipata mamlaka lazima adhibitiwe usipofanya hivyo utakiona cha mtema kuni.
Nini mtazamo wako na wewe?