TMJ acheni kutesa wagonjwa!

TMJ acheni kutesa wagonjwa!

Amina Thomas

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2008
Posts
272
Reaction score
130
Niko hapa tmj toka saa tatu asubuhi(muda ambao nilipangiwa kufika) dokta ameingia saa tano na robo.! Yaani tumekaa mpaka tunasinzia. Hivi kwa nini umpangie mgonjwa kuja mapema wakati muda wa kuja dokta unajulikana. Maana tukiulizwa tunaambiwa zaa hizi dokta anakuaga hajafika. Yani inakera maana wengine wako hoi, Njaa zinawauma na ukijumlisha na maumivu ndio usiseme. Acheni hizo. Kuweni na mpangilio mzuri.
 
ndo ujue watanzania tunaburuzwa tu mwanzo mwisho polen sana kwa wale wote mliofika hospital na kuendelea kupata matibabu
 
Niko hapa tmj toka saa tatu asubuhi(muda ambao nilipangiwa kufika) dokta ameingia saa tano na robo.! Yaani tumekaa mpaka tunasinzia. Hivi kwa nini umpangie mgonjwa kuja mapema wakati muda wa kuja dokta unajulikana. Maana tukiulizwa tunaambiwa zaa hizi dokta anakuaga hajafika. Yani inakera maana wengine wako hoi, Njaa zinawauma na ukijumlisha na maumivu ndio usiseme. Acheni hizo. Kuweni na mpangilio mzuri.

sasa haya uliyoandika umewambia wao, naona kama unatuambia sisi vile

pole sana mkuu
 
Kuna Box la maoni hapo kati wanapo pima joto,uzito
 
sasa haya uliyoandika umewambia wao, naona kama unatuambia sisi vile

pole sana mkuu

tumeshawaambia lakini hawa manesi wanaona ni kawaida. mpaka saa hizi hatujamuona daktari. nikitoka hapa lazima niwatafute wahusika maana nina hasira. mgonjwa wangu anateseka
 
tumeshawaambia lakini hawa manesi wanaona ni kawaida. mpaka saa hizi hatujamuona daktari. nikitoka hapa lazima niwatafute wahusika maana nina hasira. mgonjwa wangu anateseka

wote hao ni wahusika tafuta utawala na ushitaki huko. kama vp wambie nimeshapost katika mitandao ya kijamii mambo yenu kidogo watasikia vibaya
 
Nini TMJ ? Agakhani bana unaenda unaumwa hoi wanaanza kukufanyisha mazoezi ya kupanda NA KUSHUKA NGAZI ZAO na kila unapotoka dirisha moja kwenda lingine ni foleni yakufa mtu

Ukienda saa mbili hesabu siku nzima unafanya kazi Agakhani.

Halafu hao wahudumu wao wananyodo ile mbaya!

WaTZ tuko wapole sana kwa kifupi raia tunaonewa kila upande ndani ya nchi yetu wenyewe!
 
asante mkuu nimeliona
masanduku ya maoni yako sehemu nyingi sana,ila maoni yanayotolewa yanafanyiwa kazi?sitaki kuamini kuwa uongozi wa hospitali hawajui tatizo.sasa kama wanajua tatizo na hawatatui,unadhani ukiwaandikia watatatua?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom