Timu ya kampeni ya Mizengo Pinda hii hapa

Timu ya kampeni ya Mizengo Pinda hii hapa

Kuna suala la mize kukiri
kuongoza nchi ni ngumu je ataweza 2.Suala la kulialia je urais ataliaje si atapiga yowe 3.Kuna suala wapigwe tu tumechoka sasa mtu amechoka mnampa kazi kubwa tena 4.Kuna suala la zanzibar sio nchi na 5.Hajui tz kwanini ni maskini
 
Kambi ya lowasa pinda anawatia jamba jamba ha ha ha ha ha ha ha keshaaa wapiku Mzee yule
 
sio kweli kaka, kupenda pesa ni hulka ya mtu binafsi na sio falsafa ya kambi....... kwa mfano hata humu kwa Pinda mtu kama Bulembo au Masaburi au sara msafiri utasemaje........

nachakieleza hapa kuwa kambi ya EL imejaa watoa mikwanja na watu ambao hawana ushawishi wa siasa za majukwaani hivyo wao wanaamini pesa ndo itawapeleka magogoni.
 
Katika watu wajinga na Malaya wa kisiasa ni pamoja na wewe ocampo, yaani kwa trend ya thread zako unaonyesha ni jinsi gani ulivyo mjinga,limbukeni na hopeless mind kind of person... Fanya yako acha kumpamba Lowassa alishachafuka siku nyingiiiii tuu... Ni mpumbavu tuu na juha Kama wewe anayeweza kuamini watanzania mil 45 ni wajinga Kama wewe na kuamini mgonjwa na mwizi Kama Lowassa anaweza kuwa rais, chuma chako kwa huyo fisadi kwa kumpaka mafuta mgongo wa chupa kwenye mitandao.. Na pia nadhani wewe pia sio riziki...!!

boya kwa akili yako unadhani kambi ya mauaji ni bora kulik ya kifisad
 
- Ujinga na umbeya wa ajabu sana uniandike vipi na mimi sina kambi nimesema na nimewaaambia wahusika waote kwamba mpaka katiba ikiisha ndio nitajitosa kwenye mbio za URais na nitasema wazi ninamuunga mkono nani na nitampigia kampeni bila kuogopa mtu,

- Ulichoandika ni ujinga mtupu mimi nashindwa kumuona Pinda kaka na majuzi nilikuwa naye kwenye Diaspora Serena Hotel, nilipokuwa ninatangaza matangazo ya Mkutano wa Diaspora niliombwa na nani kaka? Wewe ni mtu wa hatari sana kama kweli unaweza kuandika majungu kama haya yakaonekana kama ni ukweli,

- I mean mimi nina shida ya bajeti ya kumsaidia Pinda unaamini ninahitaji kupitia kwa Bulembo? Really? ha! ha! ha! Un aandika maneno ya kichonganishi ulitegemea mimi hapa nitamtukana Pinda kwa kuamini majungu yako? ha! ha! ha! Majuzi mmeniita wenyewe kuniomba nisiwashambulie sasa mmeanza powa subiri katiba iishe kaka wewe na hiyo kambi yako mtanisoma sana tena kwa kila rangi!!

Le Mutuz
Le Mutuzi kapewa za uso na Ocampo four kwiiii,kwiii! teh!
 
Last edited by a moderator:
Hatutaki watu wenye busara sana hasara yake tunaiona sasa
 
Hii kambi haina mvuto; hailipi; ebu tupe kambi nyingine tuchangamkie fursa sie...
 
Kumbe ma court jesters mko wengi nilifikiri ninanii tu,tangu umeanza hekaya zako ni kambi ya manvi niliona unaifagilia,maanake mafisadi uliwapamba kisawasawa,ilipofika zamu ya wengine kila mmoja ni kumponda tu,wahenga walishasema mwenye kumlipa mpiga zumari ndie uchagua wimbo kaza butu kijana mihela yao iko njenje.
 
Le Mutuzi kapewa za uso na Ocampo four kwiiii,kwiii! teh!

- Huyo ni nguvu ndogo sana katika hiyo Kambi kaka majuzi waliniita pale Helenic Club nilienda kukutana na Samaki wakubwa huyu anayeandika hapa ni samaki mdogo sana, sio hata level yangu leo nimeongea na Samaki mkubwa wa hiyo kambi nimemmwambia humu kuna wajinga wanaowaharibia so wanayo habari!!

Le Mutuz
 
Hii kambi haina mvuto; hailipi; ebu tupe kambi nyingine tuchangamkie fursa sie...
Ni kweli kambi hailipi. Hivi Pinda anataka kuwa Rais ili aendelee kutulilia? Sidhani kama tunahitaji rais anayelia badala ya kukabiliana na changamoto za nchi. Nilisoma kuwa "Nyani" Wasira anautaka urais! Kambi yake ni ya akina nani? Duh! ama kweli urais wa Tz ni rahisi!!!! Na Wasira naye?!! Watoto si watakuwa wanalia kwa kuogopa sura yake!!!
 
- Huyo ni nguvu ndogo sana katika hiyo Kambi kaka majuzi waliniita pale Helenic Club nilienda kukutana na Samaki wakubwa huyu anayeandika hapa ni samaki mdogo sana, sio hata level yangu leo nimeongea na Samaki mkubwa wa hiyo kambi nimemmwambia humu kuna wajinga wanaowaharibia so wanayo habari!!

Le Mutuz

Habari wanayo.....utawapandisha BP zao ndugu.
 
- Ujinga na umbeya wa ajabu sana uniandike vipi na mimi sina kambi nimesema na nimewaaambia wahusika waote kwamba mpaka katiba ikiisha ndio nitajitosa kwenye mbio za URais na nitasema wazi ninamuunga mkono nani na nitampigia kampeni bila kuogopa mtu,

- Ulichoandika ni ujinga mtupu mimi nashindwa kumuona Pinda kaka na majuzi nilikuwa naye kwenye Diaspora Serena Hotel, nilipokuwa ninatangaza matangazo ya Mkutano wa Diaspora niliombwa na nani kaka? Wewe ni mtu wa hatari sana kama kweli unaweza kuandika majungu kama haya yakaonekana kama ni ukweli,

- I mean mimi nina shida ya bajeti ya kumsaidia Pinda unaamini ninahitaji kupitia kwa Bulembo? Really? ha! ha! ha! Un aandika maneno ya kichonganishi ulitegemea mimi hapa nitamtukana Pinda kwa kuamini majungu yako? ha! ha! ha! Majuzi mmeniita wenyewe kuniomba nisiwashambulie sasa mmeanza powa subiri katiba iishe kaka wewe na hiyo kambi yako mtanisoma sana tena kwa kila rangi!!

Le Mutuz

Unahangaika sana kama kuku mtetea... Mgombea wa CCM ni Lowasa!
 
Rais ni lowassa ndani ya ccm hana mpinzani wamebaki kupika majungu na kumchafua mzee wa watu
 
URAIS wa PINDA - VIBALI VYa SUKARI na UMEME KINYEREZI

Waziri Mkuu Pinda ameiingia rasmi kwenye mchakato wa URAIS kwa kasi kubwa sana kwa kipindi cha Miezi miwili sasa, haswa baada ya kuokoka kujiuzulu kwenye Operation Tokomeza.

Mawaziri wote wanne waliojiuzulu kwenye operation took meza inasemekana waliandika barua kwa Mhe Rais kwamba walitoa taarifa lakini Mhe Pinda hakufanyia utekelezaji madokezo yao, na wanaamini mpaka kesho aliyetakiwa kujiuZulu ni Pinda kwa uzembe.

Katika mpango was serikali kufidia upungufu wa sukari nchini, serikali iliamua kutoa vibali vya sukari kwa wafanyabiashara wachache ili waruhusiwe kuagiza kutoka nje na kutoka na umuhimu wa jambo lenyewe likapelekwa ofisi ni kwa Waziri Mkuu na siyo Viwanda na Biashara. Ikumbukwe kwamba Mzee Iddi Simba alifukuzwa na Bunge kutokana na udalali wa vibali vya sukari miaka ile. Inasemekana Mke wa Waziri Mkuu Mama Tunu Pinda akisaidiwa kwa karibu na Mama Janet Masaburi ,ndiyo anaongoza udalali kwa wafanyabiashara WAKWEPAJI KODI wakubwa kama Zacharia , Home shopping centre na wengineo. Kikao cha kwanza cha kampeni ya urais wa Pinda ilifanyika nyumbani kwake ikiongozwa na wafanyabiashara hawa na wakiahidiwa mfanyabiashara mkubwa Nigeria , Dangote, naye atatoa pesa kwa Pinda.

Pesa hizi za wafanyabiashara zimeonekana kutumika kwa Nguvu na Mhe Pinda kwa wabunge Dodoma na wajumbe wa mkutano Mkuu . Maadili ya Chama cha CCM inasemekana wameshtushwa sana na utoaji huo wa pesa wa vurugu kutoka kwa anayejiita 'Mtoto wa Mkulima'.

Mradi mkubwa wa umeme wa Kinyerezione inaonekana ndiyo karata kubwa atakayoitumia Pinda kujijenga kifedha kwa kuwasaidia Home Shopping Centre na Harun Mula kupata huo mradi unaotegemea Fedha kutoka kwa Wajapan. Mh Pinda amesikika akipiga simu mwenyewe kwenye ofisi za Wizara ya Fedha na ofisi ya Mwanasheria Mkuu kuharakisha huo mradi ili upitishwe haraka.

Wananchi wengi na wafuatialiaji wanajiuliza vigeZo vya Pinda alivyojipima na kujiona anafaa kugombea URAIS, wengi wanamkumbuka kwa kuwalilia Albino pale Bungeni na kuitukana Zanzibar. Tusubiri yatakayojiri
 
Dah kuhusu munde tambwe baba uko juu. Miaka ya 2007 hivi nilikuwa crdb pale tabora ni kweli hajui hata kuandika vizuri. Walikuwa wanaishi pale cheyo b kuna mwanae mmoja wa kike alikuwa na miaka kama 6 anavaa gold balaa halafu huyu mama roho mbaya sana kuna wanae wa kufikia akina bakari na saleh SAA hizi wako hoi huko dar aliwatimua. Mama khalfani alikuwa best ake sana ila wakaiba mahela wakatimuliwa. Aisee jf kiboko.
 
Haya ulotuletea yana mizizi au ni hisia tu! Nikiaangalia wasifu wa PM mwenyewe umechanganywa na ni nani anafaa zaidi kati ya Lowasa na Pinda; na hata kwa hao wengine bado mambo yamekuwa hivyo hivy yaani awali alikuwa huku sasa baada ya ... Amehamia huku.

Vipi hiyo akaunti yenyewe ipo benki ipi; mwaga yote tuelewe zaidi kabla ya kupiga kura
 
Back
Top Bottom